Friday, May 6, 2016

MUHAMMAD AWANYANG'ANYA MALI MASWAHIBA WAKE


Ndugu msomaji,
Kama ulikuwa haujui, basi leo utafahamu kuwa, Muhammad alikuwa anatabia mbaya sana ya kunyang'amya Maswahiba wake mali.
Quran Surat Al Anfaal aya 1. Wanakuuliza juu ya Ngawira. Sema: Ngawira ni ya Mwenyezi Mungu na Mtume. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na suluhisheni mambo baina yenu, na mt'iini Mwenyezi Mungu na Mtume wake ikiwa nyinyi ni Waumini. http://www.quranitukufu.net/008.html#8:1
Tarjuma ya Qur'ani Tukufu Kwa Kiswahili
Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ewe Nabii! Waambie: Hizo ngawira ni za Mwenyezi Mungu kwanza na Mtume wake. Basi wacheni kukhitalifiana kwa ajili ya hayo. Na uwe mtindo wenu ni kumkhofu Mwenyezi Mungu na kumt'ii. Na tengenezeni yaliyo baina yenu, na mfanye mapenzi na uadilifu ndio makhusiano baina yenu. Kwani hakika hizi ndizo sifa za watu wa Imani.
Ndugu msomaji, baada ya kuisoma aya iliyo teremshwa huko Madina, Muhammad anasema kuwa MALI WALIYO ITEKA YEYE NA MASWAHIBA YAKE, ni za kwake yeye na Allah.
Sasa, kama mali iliyotekwa vitani itagaiwaje kwa Allah ambaye Muhammad hakuwai muona?
Kwanini Muhammad alizikwapua mali zote na kuwanyima Maswahiba wake?
Ipo wapi aya ambayo Muhammad anamgawia Allah sehemu yake ya mali walizo ziteka kwenye vita?
Hakika Muhammad alikuwa mroho wa mali na alitumia ujanja ujanja katika kutengeneza dini yake ya Uislam.
MUHAMMAD ANASEMA KUWA MALI NI YA KWAKE NA ALLAH, HIVI TOKEA LINI ALLAH ANASHIDA NA AU HITAJI MALI YA MATEKA NA KUWAACHA MASWAHIBA WA MUHAMMAD MIKONO MITUPU?
Eti Muhammad anawaaambia Maswahiba wake kuwa, wao washike sala tu, lakini kwenye mali, ni zakwake yeye na Allah. Hakika huu ni wizi wa wazi wazi ambao Muhammad alikuwa anaufanya kwa Maswhiba wake.
Poleni sana Waislam kwa kumfuata huyu jamaa aliye kuwa anawaingiza Maswahiba wake Mjini.
In His Service
Max Shimba Ministries Org

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW