Tuesday, May 24, 2016

UONGO NDANI YA QUR'AN



*NILIHAIDI KUUKOMESHA UONGO WA QURAN NA WAISLAMU*
Jana nilisema kwa habari za uongo katika Quran walakini kama ilivyo hada waislamu siasa wakaja na maneno lukuki sasa siku zote njia za muongo fupi leo kamba waliokuwa wameishikilia isikatike imekatika atamaye wameanguka
Quran 19:28 ilisema uongo kwa kumwita Mariamu mama yake Yesu kuwa ni dada wa Haruni jambo ambalo sio kweli tutathibitisha ili, Quran 66:12 ikaja kuthibitisha uongo huo pale ilipomwita Mariamu mama wa Yesu kuwa ni binti Amran/ Imran jambo ambalo sio kweli
Mariamu mama yake Yesu akutokea kwenye ukoo wa Lawi hivyo uenda Quran imechanganya Mariamu mama yake Yesu na Miriamu dada wa Haruni{Kuto 15:20}
Na pia Quran kumtambulisha kuwa Mariamu mama yake Yesu kuwa ni binti Amran itakuwa ilimchanganya na Miriamu binti Amran soma {Hesabu 26:59.........maana Miriamu pekee ndiye aliyekuwa binti Amran maana yake waislamu wanajua kuwa Quran imesema uongo ila wameamua kudanganyika wenyewe
Sura ambayo waislamu wamekubali itafsriwe kimatakwa yao ili iendane na matakwa yao na kuhalalisha juu ya uongo wao ni Luka 1:36 panapo mtaja mariamu kuwa alikuwa ni jamaa wa Elizabethi neno jamaa hapa lina maana ya watu waliokaribu sio maana ya ndugu yaani ya udada, na jambo ilo sio kweli kuwa watu hawa walikuwa ndugu kwa sababu jambo ilo alithibitishwi Kibiblia wala hata katika historia za kimwili za wayahudi
Maana inatambulika wazi kuwa watu hawa wawili yaani Elizabeth na Mariamu walikuwa ni jamaa walakini jamaa sio lazima awe ndugu, ujamaa uenda ni hali za watu kufahamiana hivyo basi hawa wawili walikuwa wakitokea katika makabila mawili tofauti kabisa
USHAIDI UNAOTHIBITISHA UONGO WA QURAN

Biblia mara zote imesisitiza kuwa Yesu ni mwana wa Daudi na sababu ni kuonyesha alikuwa ni mrithi wa ufalme wa Daudi, hivyo basi laiti kama asingelikuwa mzao wa Daudi asinglikuwa na haki ya kuwa mrithi wa Daudi {Zabur 89:3-4} inaonyesha ahadi ya Mungu juu ya kiti cha Ufalme wa Daudi
Katika Yeremia 23:5 neno la Mungu linaonyesha mpango wa Mungu kurejesha ufalme kupitia Daudi yaani kupitia uzao wa Daudi Mungu atamsimamisha mfalme atakayetenda hekima, naye atafanya hukumu na haki katika nchi........
Katika Matendo 13:22-23 inaonyesha ama kuthibitisha juu ya Yesu kuinuliwa na akiwa ndiye mzao wa Daudi na mrithi wa ufalme wa Daudi, “katika uzao wake mtu huyo (yaani Daudi) Mungu amewaletea Israel mwokozi, Yaani Yesu kama alivyo haidiwa”
Bila shaka tunaona kupitia haya maandiko yote yanathibitisha juu yake Yesu kuzaliwa kupitia Daudi na sio Lawi, zamani watu wengi walikuwa awahesabii watoto wa kike kwenye uzao ndio maana hata katika mlango wa 1:1 Mathayo atajwi Mariamu kwa sababu ndio ulikuwa utamaduni wa zamani uzao ulikuwa ni kwa wanaume tu na ikumbukwe Yusufu na Mariamu hawa walikuwa ni ndugu yaani wote walikuwa wanatoka katika kabila la Yuda sawa na Elizabeth na Zekaria mumewe{Luka 1:5}
Sasa katika kumalizia huu mjadara wa kuthibitisha uongo wa Quran embu tusikilize maneno ya malaika kwa Mariamu katika Luka 1:30-33 tuthibitishe “Tazama , utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanaume,jina lake utamwita Yesu, huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake,ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme utakuwa hauna mwisho”
Hapa malaika anaimaliza kesi hii kwa kuutanabaisha uma wa wanadamu uzao wa Yesu kuwa ni kupitia ukoo wa Daudi ingawa hakuwa mtoto kibaolojia wa Yusufu walakini nguvu ya kuwa mrithi wa kiti cha Daudi imetokana na Mariamu mama yake ambaye naye pia alikuwa ni uzao wa Daudi
Sasa haya ya kusema Mariamu ni mtoto wa Amrani/Imran wapi Muhammad ameyapata, Mungu gani huyo asiyewafahamu watu wake na kujichanganya kwa kiasi kikubwa hicho?
Hii inaturidhisha kuamini kuwa Quran ni kama hadithi zile za fasihi simulizi na tuliosoma kishwaili tunaelewa madhara yanaotokana na fasihi simulizi ,kitu kinaposimuliwa kinaweza kubadilishwa kwa wanaopokea ,kikaongezewa ama kupunguzwa au kusahaulika kwa mambo mengine au kuchanganywa kwa baadhi ya vitu na Mambo's
Sasa je kwa huku kujichanganya kwake quran, swali je Quran imetoka kwa Mungu? Kumbuka sio sifa ya Mungu usahaulifu au kujichanganya hiyo ni sifa za wanadamu

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW