Saturday, December 3, 2016

Imam wa Msikiti wa Mayaha, Kisisi apokea Uponyaji kwa Jina la Yesu!



Mchungaji Michael Peter Imani wa WAPO Mission International Tawi la Mbagala Maji Matitu akiwa amemshikia kipaza sauti Mzee Musa Hombe (Idd Hussein Seba) (73) Imam wa Msikiti wa Mayaha, Kijiji cha Kisisi, Kata ya Ekhanoda Wilaya ya Singida Vijijini.

Aliyekuwa Imam wa Msikiti wa Mayaha, akishuhudia jinsi Yesu alivyomponya baada ya kuugua kwa miaka 15 “Sasa ninatafuta wa kuninunulia Biblia, Yesu anaponya mimi nimepona, ninyi waislamu wenzangu mnapoteza muda”

Pichani ni mtoto wa aliyekuwa Imam baada ya kupokea uponyaji na kumpokea Bwana Yesu

Christopher ambaye pia ni mtoto wa Juma Kombe, akifurahia kuuona Utukufu wa Mungu baada ya kuokoka, alikuwa amepagawa mapepo na biashara zake zikawa haziendi baada ya kuokoka kwa wiki tatu akaanza kuona mabadiliko ya biashara yake kushamiri kwa kasi.  “Nilipofanyiwa maombi ya wiki 3, nikakaa sawa, nikaingia darasani kusoma, nilipojazwa Roho Mtakatifu, usiku nimelala walikuja wachawi, wakaniita jina la zamani, Abdallah, lakini sauti ya upole ikaniambia, usiitike”.

Kijana Christopher ndiye aliyesababisha baba yake Kumpokea Bwana Yesu.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW