Friday, December 2, 2016

YESU NI MUNGU


Kama kawaida Waislam wanazidi kushikiria na kupinga kuwa Yesu ni Mungu! na Kinacho nishangaza wakipewa maandiko kuhusu u Mungu wa Yesu, wanachofanya ni kubadilisha maada!
Utasikiaaa "Oooh!!! Paulo sio Mtume wa Mungu. Mara ooooh Yesu hakufa!! Ooooh Wakristo mnakula Mashonde"na wanakuletea hoja nyingi ili kupoteza mada husika na Wakristo wanapowajibu kwa kutumia maandiko na kutaka kuendelea na maada husika wanabaki kuchanganyikiwa na kukimbia maada!
HUKO NI KUJIDANGANYA WENYEWE NDUGU ZANGU WAISLAM!!!! SISI Wakristo kazi yetu kuelimisha!! Maana Bwana Yesu alituagiza KUHUBIRI INJILI
"*************"
Marko 16:15-16(Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. ).
LAKINI HOJA YAO KUU NI IPI???
Leo mwislam mmoja alikuja inbox kwangu na hii hoja tena kwa ujasili wote akasema haya leta Biblia yako unijibu hoja hii
AYUBU 36 aya 26
Tazama, Mungu ni Mkuu Nasi hatumjui. Hesabu yake haitafutiki
Haya sasa umeona hapo Juu! Hesabu ya Miaka ya Mungu hakuna aijuaye..tangu kuwepo kwake Yesu miaka yake inaesabika!! Itakuwaje Yesu awe Mungu?
Ebu soma hii
Luka 3:23
Na Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa amepata umri wake kama miaka thelathini, akidhaniwa kuwa ni mwana wa Yusuph, wa Eli!
Haya kwa mujibu wa maandiko niliyokupa hapo juu niambie JE YESU ANASIFA YA MUNGU?
Mwislam akacheka kwa kebehi
hahaahaahaaaha ni jibu bhana! Usinikimbie.
Ukiangalia hoja kama ya huyo hapo ndugu!amejitahidi kuisema kwa ujasiri wote lakini amesahau kwamba nasisi tunaijua Biblia vizuri sana na inamajibu yote.
Kwa kuangalia hoja ya huyo ndugu hapo juu, na mjibu kama ifuatavyo:
Kamata Biblia yako twende sawa hapa!
Imeandikwa:
Wafilipi 2:5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; 6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; 7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; 8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.
Ukiangalia maandiko hapo juu, unaona Yesu alikuwa namna ya Mungu lakini kwa upendo wake mkuu aliamua kuja ulimwengu kutuokoa (Yohana3 aya 16)
Alijifanya kuwa hana utukufu akatwaa namna ya mtumwa akawa anamfano wa Mwanadamu.
Imeandikwa kwamba: Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, na binadamu hata umwangalie? Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu; umemvika taji ya utukufu na heshima; umemtawaza juu ya kazi za mikono yako; umevitia vitu vyote chini ya miguu yake. (Zaburi 8:4-6).
Mtunga Zaburi anasema mtu ni kitu gani paka umuangalie.
Hapo kuwa Yesu alitupenda paka akatoka kwenye kiti chake cha enzi ili aje kutuokoa toka dhambini.
Imeandikwa: Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (Yohana 3:16).
JE WEWE USIYEMWAMINI YESU una uzima wa milele? (tafakari) Ukisoma Yohana 8:56 Yesu anawaambia Wayahudi. Ibrahim, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu: naye akaiona akafurahi 57 Basi Wayahudi wakamwambia, wewe hujapata bado miaka Hamsini, nawe umemwona Ibrahimu? 58 Yesu akawaambia amin, Amin, nawaambia YEYE IBRAHIM ASIJAKUAKO,MIMI NIKO.
Yesu ni Mungu alikuwepo kabla ya kuumbwa kwa dunia. YEYE NI ALFA NA OMEGA.
Imeandikwa
Hapo mwanzo kulikuwako Neno naye Neno alikuwa kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu (Yohana1:1)
Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu: nasi tukauona utukufu wake.utukufu kama wa mwana atokaye kwa Baba: Amejaa neema na kweli. (Yohana1:14)
Nadhani hadi hapo Waislam wanaanza kuelewa somo!!
Ilibidi Yesu Mungu Mkuu kufanyika mwili ili kufidia dhambi zetu mimi na wewe! (Warumi5:8)
Imeandikwa
Yeye asiyejua dhambi alimfanya dhambi kwa ajili yetu ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika yeye.
Kuna baadhi ya Waislam wanasema "kwahiyo nyinyi Wakristo mna Mungu watatu"
Jibu ni kwamba! Mungu wetu ni mmoja tu!
Mungu Baba
Mungu Mwana
Mungu Roho Mtakatifu
=Mungu mmoja!!
Ila amegawanyika katika Utatu. (Kumb 6;4)
Maana ya Nafsi Tatu angalia mwenyewe
Mwanzo1:1, 1:26, 3:22
Isaya 6:8
Mathayo 3:16-17
Soma Yohana 10:30
Imeandikwa
1Timotheo2:5
Kwasababu Mungu ni mmoja na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja mwanadamu kristo Yesu 6 ambaye alijitoa mwenyewe kwa ukombozi kwa ajili ya wote, utakaoshuhudiwa kwa majira yake.
Ukiangalia kwenye andiko hilo unaona kazi ya kila nafsi!
Mungu Baba katika uumbaji
Mungu Mwana katika ukombozi
Mungu Roho Mtakatifu katika ualimu!
Majukumu
Baba-Mwana-Roho Mtakatifu!!
Wakorintho 8:6
Lakini kwetu sisi Mungu ni Mmoja tu aliye Baba ambaye vitu vyote vimetoka kwake: Yuko na Bwana mmoja Yesu Kristo ambaye kwake vitu vyote vimekuwako na sisi kwa yeye huyo!
Ukiangalia andiko hilo utagundua Yesu ana sifa zote za ki Mungu!
-Yeye ni muumbaji
-Mkombozi
1Timotheo 3:16
Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu.
MUNGU ALIDHIHIRISHWA KATIKA MWILI, Akajulika kuwa na haki katika roho, akaonekana na Malaika, akahubiriwa katika mataifa,
Akaaminiwa katika ulimwengu, akachukuliwa juu katika utukufu.
Ni Mungu gani aliyedhihirishwa katika mwili? Jibu liko wazi. Ni Yesu Kristo peke yake.
Tito 2:13
….tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa KRISTO YESU, MUNGU MKUU NA MWOKOZI WETU
Yesu Kristo ni Mungu Mkuu!!
Shida KUU ya Waislamu ni hii:
Wanampima Mungu kwa vigezo vya kibinadamu. Mungu anasema: Tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa wote wenye mwili; je! Kuna neno gumu lo lote nisiloliweza? (Yeremia 32:27)
Jibu liko wazo. HAKUNA!
Lakini utakuta Waislamu wanauliza maswali ya ajabu sana. Eti, kama Yesu ni Mungu, wakati amekufa, nani alikuwa anaangalia dunia?
Hili ni swali linalofaa kuulizwa juu ya kiumbe. Kama tungesema kuwa mwanadamu fulani alikuwa amekufa, ndipo kuna mantiki kuuliza kwamba, wakati amekufa nani alikuwa anatunza familia yake? Maana hili ni swali linalohusu tabia za kibinadamu kwa kuwa mwanadamu hawezi kuwa mahali kuwili au zaidi kwa pamoja. MUNGU SI MWANADAMU! ANAWEZA YOTE – NA HASA MUNGU WA IBRAHIMU, ISAKA NA YAKOBO!
YESU NI MUNGU MILELE NA MILELE!!
HALELUYA!!
HITIMISHO
Yohana 8:31 Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini. NINYI MKIKAA KATIKA NENO LANGU Mmekuwa wanafunzi wangu kwelikweli 32 tena mtaifahamu kweli nayo hiyo ITAWAWEKA HURU.
Ndugu zangu Waislam njooni kwa Yesu mpate kujua kweli na hiyo kweli itawaweka huru!
-itawaweka huru na dhambi
-itawaweka huru na vifungo vya Shetani
Ndugu yangu kwanini un'gan'gani kubaki kwenye vifungo vya Shetani wakati Yesu anakuita kwa sauti ya upole!!
Mimi ndimi njia ya kweli na uzima HAKUNA AJAYE KWA BABA ILA KUPITIA MIMI (Yohana 14:6)
Sasa basi unategemea kwenda mbingu ipi kama unamkataa Yesu?
Tafakari
Hoji mambo
Chukua hatua
IJUE KWELI NAYO ITAKUWEKA HURU!!
YESU NI MUNGU.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW