Sunday, April 22, 2018

WAPAGANI WA KALE WALIMWABUDU ALLAH MUNGU JUA NA MKE WAKE MUNGU MWEZI

Image may contain: text


Wapagani wengi wa kale walimwabudu mungu jua na mungu mke mwezi aitwae Allah. Waarabu wa magharibi walikuwa tofauti kwa kumwabudu mungu mwezi na mkewe, mungu mke jua. Kuna sanamu za kabla ya Uislam za alama yake: mwezi mwandamo. Sanamu hii inafanana sana na mwezi mwandamo wa wa Waislam wa Shia, isipokuwa Washia wameongeza nyota ndogo. Wayemen/Sabaeans walikuwa na mungu mwezi kwa mujibu wa Ensaiklopidia ya Uislamu uk.303. Wakureshi wanawezakuwa walimpata mungu huyu kutoka kwao.
Allah alikuwa na mabinti watatu walioitwa Lat, 'Uzza na Manat. Siku moja "Nabii wa Allah" aliafiki na kusema katika Quran (Sura 53:19) kuwa maombezi yao yanapaswa kutumainiwa. Kwa maneno mengine alisema tunapaswa kutumaini msaada wa miungu hawa watatu.
Wafuasi wa Muhammad walishangazwa kuwa amesema hivi. Baadaye, Muhammad alibadilisha mawazo yake na kusema shetani alimdanganya. Kwa vile palikuwa na kosa lililofanyika, aya hizi "zilibatilishwa" au kuondolewa. Aya hizi zinajulikana kama "aya za shetani." Inashangaza kusoma jinsi ambavyo Allah angeweza kuwa na "aya zilizobatiishwa" katika Sura za 13:39, 16:101; juzuu ya 2:106. Sura 41:37 zinataja kwa kutokuafiki watu wanaoabudu jua na mwezi.
Kwa muhtasari, Maka wakati wa Muhammad ulikuwa mji wenye watu toka mataifa mbalimbali. Wasabaiani (Sabaeans), na kabila la Muhammad yaani Wakureshi waliabudu sanamu mwezi iliyoitwa Al-ilah au Allah, pamoja na mabinti zake watatu. Kurani inakataza kuabudu miungu, lakini wanazuoni wa kislam wanakiri kuwa mwanzoni Muhammad aliweka aya zinazosema kuwa maombezi ya mabinti wa Allah yanapaswa kutumainiwa.
Shalom,

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW