Tuesday, April 10, 2018

Waislamu waanzisha fujo baada ya Wakristo katika kijiji cha Buseresere kuchinja Ng'ombe na Mbuzi huku Mtu mmoja akifariki na watu 10 wakijeruhiwa vibaya kwa mapanga

SAM_4110


Picha:Nyamba ambayo inadaiwa Wakiristo  walikuwa wamechinja ng’ombe mmoja na mbuzi wawili eneo la kanisani kabla ya kuipeleka nyama hiyo katika bucha hiyo iliyoko eneo la Buseresere Sokoni na ndipo walipokumbana na kadhia.



Katika Vurugu  hizo  kubwa za kidini kati ya Waislamu na Wakristo, zimezuka katika kijiji cha Buseresere, wilaya ya Chato, mkoani Geita, na kusababisha kifo cha Mchungaji wa Kanisa la Pentekoste Assemblies of God, Mathayo Kachila (45), huku watu wengine 10 wakijeruhiwa vibaya kwa mapanga.


SAM_4113

Waraka unaotajwa kuwahamasisha wakristu kushiriki katika uzinduzi wa uchinjaji.
SAM_4112

FFU kazini katika eneo la Buseresere  wilaya ya Chato, mkoani Geita katika hatua za kurejesha Amani na Utulivu.

SAM_4119

Mkuu wa Wilaya ya Chato,Bw. Ludorick Mpogolo, aliyefika eneo la tukio muda mfupi baada ya polisi kuwasili, mbali na kusikitishwa na kitendo hicho aliwataka wananchi kuwa watulivu wakati serikali ikiangalia njia sahihi za kutatua mgogoro huo ambao unakua kwa kasi kila kukicha.


Hivi karibuni mgogoro huo wa kidini umezidi kukua wilayani humo kwa pande hizo mbili kila upande ukidai ndiyo wenye haki ya kuchinja nyama inayouzwa buchani.
majeruh+ramadan+wod+8+geita+hosp

Majeruhi Ramadan aliyejeruiwa wakati wa vurugu za waislam na wakristu wachache zilizotokea leo katika kijiji cha Buseresere wilayani Chato mkoani Geita na kusababisha fukuto kubwa la vurugu zilizosababisha shughuli mbalimbali kusimama.-

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW