Wednesday, March 21, 2018

UNAJUA MAANA YA JINA LA BETHLEHEM?

Image may contain: sky and outdoor
jina "Bethlehemu" linamaanisha nini kwenye Mat 2:1, 5-8; Luk 2:4-7 na Yoh 7:42?
Bethlehemu inamaanisha "nyumba ya mkate."
Bethlehemu ya Uyahudi ni mji wa zamani sana uliokuwepo kabla ya wana Israeli. Mwanzo 35:19 inasema, "Akafa Raheli, akazikwa katika njia ya Efrathi, ndiyo Bethlehemu." Mwanzo 48:7 inasema kama hivyo. Kwa hiyo jina la awali la Bethlehemu ni Efrathi, na ndiyo sababu kwenye Mika 5:2 mji huu unaitwa "Bethlehemu Efrata."
Maandishi ya Amarna, waliyoandikwa na Wakanaani kwa Wamisri muda mfupi baada ya mwaka 1400 KK wakati wa utawala wa Yoshua, yanasema kuwa "Bit-Lahmi" waliwaasi Waapiru (jina la jumla la watu walioishi maeneo yanayoanzia Mesopotamia hadi mpaka na Misri miaka ya 1800 hadi 1100KK).
Pamoja na hayo, kuna mji mwingine pia, ulio kaskazini unaoitwa Bethlehemu, kwenye eneo la Zabuloni (Yos 19:15).
Shalom

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW