Wednesday, March 28, 2018

UNAMJUA MNYAMA NA NABII WA UONGO ALIYE TABIRIWA KWENYE UFUNUO?


Nabii wa uongo wa nyakati za mwisho ameelezwa katika Ufunuo 13: 11-15. Yeye pia hujulikana kama "mnyama wa pili" (Ufunuo 16:13, 19:20, 20:10).

Ufunuo 13,11-17 - Kisha nikaona mnyama mwingine akipanda juu kutoka katika nchi alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo lakini aliongea kama joka. Hubeba nguvu zote za mnyama wa kwanza mbele yake na kuwa nchi na watu wake kuabudu mnyama wa kwanza, ambaye jeraha la kifo lililokuwa limepona. Anafanya maajabu makubwa, ina hata mbele ya watu moto ukashuka kutoka mbinguni na duniani. Mambo haya ya ajabu, ilikuwa ni kutokana na kuchukua mbele ya mnyama, zidanganyazo wale wanaoishi duniani. Anasema wakazi wa nchi na kuunda sanamu ya mnyama, aliyekuwa na jeraha la upanga, lakini akafufuka.

Hali ya mnyama - nguvu Hii ni kikubwa tofauti na mnyama kutoka baharini. Siyo wa dini sana. Ibada si kwa madhumuni yake (Ufunuo 13,12.15). Kinyume chake, inaelezwa kama nguvu ya kiuchumi - huathiri kununua na kuuza (Ufunuo 13.17), na nguvu ya kisiasa - inaweza kuuwa (Ufunuo 13.15).

Hivyo basi, Mnyama na Nabii wa uongo watauongoza mfumo wa mwisho wa kidini-na-kiselikali wenye nguvu ulioonyeshwa kwenye Ufunuo 17 na 18, ambao Kristo ataupondaponda na kuchukua mahala pake katika Kurudi Kwake. Ufunuo 16:13-14 huelezea roho za mashetani kama zikiwa na nguvu ya “kufanya miujiza” kupitia mfumo huu. Mnyama akiwa ndiye kiungo kikuu cha mfumo huu, atakuwa mtu mkuu atawalaye ulimwengu.

Kazi za Nabii wa uongo ni zipi?

Nabii wa uongo naye, ataongoza ulimwengu kumwabudu mnyama kama Mungu (Ufunuo 16:2; 19:20)! Udanganyifu huu utaenea sana (18:3)—kwa ukamilifu—kiasi kwamba watawadanganya wanadamu wote kufikia kupigana na Kristo katika Kuja Kwake Mara ya Pili (16:9, 13-16; 17:13-14)!

UTHIBITISHO:
Sasa angalia 2 Wathesalonike 2:3-4 na 8. Fungu la 3 humrejelea yule anayeitwa “mtu wa kuasi” na “mwana wa uharibifu; yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu.” Nabii wa uongo naye pia hudai kwamba ni Mungu.

UTHIBITISHO:
Linganisha hiki na Ezekieli 28:2 na kielelezo cha “mfalme wa Tiro”—mwanadamu. Ezekieli aliandika kwamba “mfalme” huyu husema “Mimi ni Mungu, naketi katika kiti cha Mungu,” 2 Wathesalonike 2:8 humwelezea huyu “mtu wa kuasi” kama “[yule] mwovu” ambaye “atafunuliwa” namna vile alivyo wakati Kristo anaporudi na kumwangamiza pamoja na mnyama katika ziwa la moto (Ufu. 19:20). Isaya 14:4 humrejelea nabii wa uongo kama “Mfalme wa Babeli.” Huyu ndiye yule yule “Mfalme wa Tiro,”

Ukiendelea katika 2 Wathesalonike 2, fungu la 9 hutoa kauli ya kushangaza juu ya nabii wa uongo. Inasema kwamba “kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo.” Fungu la kumi huonyesha kwamba anaweza kumdanganya kila mmoja “asiyependa kweli.” Fungu la 11 hufunua kwamba Mungu ataleta “nguvu ya upotevu” kwa wote ambao kwa utashi wao huamini uongo wake.

Viongozi wa mfumo huu mkuu wa uongo watakuwa wamepagawa moja kwa moja na shetani! Hali hii itampatia nabii wa uongo nguvu nyingi sana za kudanganya na kutenda miujiza. Shetani, ambaye wakati wote ametamani kumpindua Mungu na kuchukua mahali pake, atanena kupitia mtu huyu ambaye ni kiongozi wa kidini na kuutangazia ulimwengu wote kwamba, hakika yeye ni, MUNGU! Onyo hili la Biblia halina utata. Miujiza atakayotenda itawadanganya walio wengi sana miongoni mwa watu!

Ufunuo 19:20 Yule mnyama akakamatwa, na yule nabii wa uongo pamoja naye, yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama, nao walioisujudia sanamu yake; hao wawili wakatupwa wangali hai katika lile ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti;

Shalom,

Max Shimba Mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na mwokozi wetu. Tito 2:13

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW