Thursday, February 11, 2016

ALLAH KUPITIA MUHAMMAD AMEHARIMISHA KUVAA PETE YENYE DHAHABU


Ndugu msomaji,
Kuharamishwa uvaaji wa dhahabu kwa wanaume kumethibiti katika hadithi nyingi sahihi zilizopokelewa kutika kwa Mtume wa Allah –Rehema na Amani zimshukie.
Amepokea (riwaya) Imamu Bukhaariy, Muislam na Ahmad kwamba Mtume wa Allah “Amekataza (kuvaa) pete ya dhahabu”.
Imepokelewa kutoka kawa Ibn Abbaas-Allah awawiye radhi-kwamba Mtume wa Allah aliiona pete ya dhahabu kidoleni mwa mtu, akamvua na kuitupa (huku) akisema
“ Mmoja wenu analikusudia kaa la moto na kulivaa mkononi?” Mtu yule akaambiwa baada ya kwenda zake mtume “ Itwae pete yako unufaike nayo. Akawajibu Wallah hapana, kamwe sitaichukua ikiwa aliyeitupa ni Mtume wa Allah –Rehema na Amani zimshukie.” Muislam
Na katika jumla ya riwaya zilizopokelewa kwamba Mtume wa Allah –Rehema na Amani zimshukie amesema : “ Ye yote mwenye kumuamini Allah na siku ya mwisho basi asivae hariri wala dhahabu.” Al-musnad {Musnadul–Imam Ahmad}
Huu ni msiba kwa Waislam. Maana siku hizi hawa Waislam wanavaa nguo za harirti pamoja na pete ya dhabu. Ona picha ya Usma Bin Laden na yeye amevaa pete ya dhabu. Astgahfurillah.

Max Shimba Ministries Org

No comments:

Mohammad’s Myths vs. Biblical and Scientific Reality: A Scholarly Debate on Laughter, Heart, and Divine Truth

By Dr. Maxwell Shimba, Shimba Theological Institute Introduction In evaluating the truth-claims of any religion, the alignment between i...

TRENDING NOW