Wednesday, February 10, 2016

WASABATO WANASEMA KUWA YESU KRISTO NDIE MALAIKA MIKAELI


Kanisa na Imani au dini ya Wasabato inafundisha kuwa Yesu Kristo na Malaika Mkuu Mikaeli ni mtu mmoja. Hata hivyo, watu wengine kimakosa wanafikiria kuwa SDA wanafundisha kuwa, Yesu ni Malaika aliye umbwa, na kwahiyo hakuwa mtakatifu "divine" . Lakini, hivyo sio Wasabato wanavyo amini. Badala yake, wanasema katika Agano la Kale kuwa, udhihirisho wa Malaika Mkuu Mikaeli ulikuwa ni utambulisho wa Yesu Kristo kabla hajaja duniani na kwamba Malaika Mkuu Mikaeli hakuumbwa. KATIKA MADAI HAYA, wamekosea katika kulinganisha kwao, lakini katika kukubali kuwa hana na hakuumbwa, wanakubali kuwa Yesu ni Mungu.

Hebu tosome Biblia kwanza:
Yohana 8: 58 Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.

Hapa kuna matatizo makubwa kwa Wasabato, kwasababu neno la Kigiriki ego eimi linamaanisha " MIMI NIKO". Hili neno liliwafanya Wayahudi wachukie sana , pale Yesu alipo sema yeye ni NIKO "I AM" kiasi cha kutaka kumuua kwasababu alikua anatumia aya ya KUTOKA 3:14 pale Mungu alipo sema kuwa Jina lake ni NIKO" 14 Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO; ["akasema,Ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli;MIMI NIKO amenituma kwenu"]. Angalia vile vile katika Yohana 10: 30-33 kwa uhakikisho wa haya maneno.

Wasabato wanakubali kuwa Yesu ni Mungu, lakini kigeugeu chao kinawafanya wawe sawa na Mashahidi wa Jehovah na kupingana na aya za Biblia Takatifu na kualzimisha kuwa eti, Malaika Mkuu Mikaeli ni Yesu.


DAI LA KWANZA LA WASABATO KUWA YESU NI MALAIKA MIKAELI
1 Wasesalonike 4: 16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.

Wasabato wanafurai sana hii aya, kwa kuweka ufafanuzi wa kithiolojia. Wasabato wanafundisha kuwa Yesu Kristo ni Malaika Mkuu Mikaeli, na hivyo kubadilisha maana halisi ya hii aya ili kusaidia theolojia ya imani yao kuwa Yesu ni Malaika Mkuu Mikaeli. Madai ya Wasabato ni makosa maana wanaizuia Biblia kuzungunza katika context/mazingira yake.

HOJA::::
Katika aya hapo ju, ipo wazi kuwa: Moja, Bwana atashuka, Pili, tunasoma kuhusu sauti ya Malaika Mkuu. Tatu, Tunajifunza kuwa kumbe Bwana wetu Yesu sio Malaika Mkuu, maana hiyo aya imewatenganisha hao wawili.


DAI LA PILI LA WASABATO KUWA YESU NI MALAIKA MIKAELI
Yuda 1: 9 Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee.

Huu ni mfano mwingine wa thiolojia ya Wasabato inayo linda dai lao la Yesu ni Malaika Mikaeli. Ukizungumza kwa kutumia Biblia, YESU SIO MALAIKA MIKAELI. Hao ni wawili tofauti kabisa, na kuwaunganisha na kusema kuwa Yesu ni Mikaeli ni MAKOSA ambayo Wasabato wanafanya kwa kutengeneza hii aya ili isaidia thiolojia yao.

HOJA:::::
KATIKA AYA HAPO JUU, tunajifunza kuwa Malika Mkuu anasema kuwa NUKUU "Bwana akukemee" Sasa inafahamika kuwa Yesu ni Bwana. kivipi basi Mikaeli aseme Bwana akukemee kama yeye ndie huyo huyo Bwana Yesu? Kwanini hakusema NAKUKEMEA......



DAI LA TATU LA WASABATO KUWA YESU NI MALAIKA MIKAELI
Ufunuo 12:7 Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;

Ona tena hapa, jinsi Wasabato wanavyo itumia thiolojia kusaidia dai lao la Yesu ni Malaika Mikaeli. Hii haya haisemi hivyo wala saidia thiolojia ya Wasabato kuwa Yesu ni Mikaeli.

HOJA::::
Hiyo aya hapo juu inazungumzia Malaika Mikaeli akipigana na Joka, na ahakuna sehemu yeyote ile inamzungumzia Yesu.



BIBLIA INAKUJIBU KAMA IFUATAVYO
Waebrania 1: 5 Kwa maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa? Na tena, Mimi nitakuwa kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana?

Mungu Baba katika Waebrania 1: 5 anauliza, wapi kasema katika Biblia kwa Malaika yeyote yule kuwa wewe ni Mwanangu? Mungu anapinga dai la WASABATO KUWA Malaika Mkuu Mikaeli ni Yesu. Mungu anasema kuwa hajawai muita Mailaka yeyote yule kuwa yeye ni Mwanae.

MUNGU ANAENDELEA KUSEMA katika Waebrania 1 aya 13 Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako?

Hatusome sehemu yeyote ile kuwa Malaika Mkuu Mikaeli aliambiwa akae mkono wa Kuume wa Mungu Baba. Hivyo basi, dai la Wasabato kuwa Yesu ni Malaika Mikaleli limeshindwa kwa mara nyingine hapa.

MUNGU ANAWAAMURU MALAIKA WOTE WAMSUJUDU YESU
Waebrania 1: 6 Hata tena, amletapo mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, asema, Na wamsujudu malaika wote wa Mungu.

Je, katika hiyo aya ya 6, ni nani huyo anaye sujudiwa? Hakika Biblia ipo wazi na inapinga thiolojia ya Wasabato kuwa Yesu ni Malaika Mkuu Mikaeli.

Max Shimba

For Max Shimba Ministries Org

1 comment:

Unknown said...

Sauti ya malaika inaweza ikafufua wafu? Lakini Walio kufa katika bwana wataisikia sauti yake (YESU) nao watakuwa hai tena.Yohana 5:25,28,29. Hivyo sauti ya malaika mkuu katika 1wathesalonike 4:16 ni sauti ya Yesu mwenyewe.KAMA UNA SWALI TUMA NAMBA 0764555446

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW