Thursday, February 11, 2016

UHUSIANO NA KUFANANA KATI YA WASABATO NA MASHAHIDI WA YEHOVA

Wasabato "SDA" na Mashahidi wa Yehova wote wawili walianzia katika muamko ulio kuwa katika miaka ya 1800 ambao msingi wake ulikuwa ni unabii wa Miller. Mafundisho yao yalianzia kutoka kwenye huu utabiri wa Miller na unafanana katika mambo mengi.
Huu muamko ulianza kupitia utabiri wa kifalme katika mwaka wa 1844, na ulikuwa na waamini wachache sana, ambao wengi wao walitoka katika Makanisa ya Kiroho baada ya kufukuzwa huko kwa sababu ya kufuata utabiri wa Miller.
Baada ya kufukuzwa, walianza kufikiri jinsi ya kuazisha kanisa au mkusanyiko, ingawa hawakuwa na "Mfumo wa hilo kanisa", lakini walipata muamko mkubwa zaidia baada ya kupa ujumbe mwengine uliandikwa na Ellen G. White. Barua hii ya Ellen G. White ndio iliyo anzisha kanisa la Wasabato, na Mwaka 1860 ndio jina la "Seventh Day Adventist" lilichaguliwa na kuwa na kanisa la kwanza.
Mafundisho mengi ya MSINGI ya Wasabato ni yaleyale ambayo yanafundishwa na Mashahidi wa Yehova. Tofauti kubwa ni ile ya Wasabato kuamini kuwa Jumamosi ndio siku pekee ya kuabudu, wakati Mashahidi wa Yehova wao hawashikirii hiyo siku kuwa ni ya muhimu sana.
Wote hao wawili Wasabato na Mashahdi wa Yehova wanakata kushiri Vita ikiwa nchi ipo kwenye matatizo, ingawa wanakubali kufanya kazi za kijeshi ambazo sio za kivita, kama ambavyo Mashahdi wa Yehova walivyo goma kwenda kwenye Vita Kuu ya kwanza ya dunia.
KIFO: Wanaamini kuwa mtu "mwili, roho na nafsi" akifa basi hubakia kwenye kaburi.
Mwanzo 2: 1 Basi mbingu na nchi zikamalizika, na jeshi lake lote.
2 Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya. 3 Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya.
Ingawa, hakuna aya hata moja kwenye Biblia inayo sema Mungu alimwambia Adama aitunze siku ya Saba" SABATO" kila wiki. Lakini Wasabato wanashikiria kuwa hiyo ndio siku halali ya kusali.
1. Je, Adam alikuwa anafanya na au tenda dhambi kwa kutoa itunza Sabato?
2. Je, baba wa Imani, Ibrahimu, alikuwa anatenda dhambi kwa kuto itunza Sabato, ingawa hakuambiwa afanye hivyo?
3. Je, wana wa Israel walipo kuwa Misri, walikuwa watenda dhambi, maana sheria ya kutunza Sabato ilikuwa bado hawana?
YESU NI MALAIKA MIKAELI
Wote, Wasabato na Mashahidi wa Yehova wanaamini kuwa Yesu Kristo ndie Malaika Mkuu Mikaeli. Ingawa hakuna aya hata moja inayo sema hivyo.
ROHO MTAKATIFU
Wote, SDA-WASABATO na Mashahidi wa Yehova hawaamini kuwa Roho Mtakatifu ni Mungu. Mashahidi wa Yehova wanaami kuwa Roho Mtakatifu ni kama NISHATI FULANI,
Ellen G. White yeye anasema kuwa Roho Mtakatifu ni nguvu fulani ya Mungu, lakini amekataa kusema kuwa Roho Mtakatifu ni "Person" -mtu./Mungu kamili kama alivyo Baba yetu aliye Mbinguni na ana adhama/attributes zote za Mungu
KIFO NI KULALA KWA NAFSI
Wote, Wasabato na Mashahidi wa Yehova wanaamini kuwa kifo ni kulala kwa nafsi kaburini na hubakia kaburini mpaka siku ya kiyama.
JEHANNAM
SDA-Wasbato wanaamini kuwa kuna Jehannam lakini wenda dhambi hawata kaa huko milele bali kwa muda tu, huku Mashahidi wa Yehowa wanaamini kuwa Jehannam itawaangamiza watu mara moja, na hawato kuwepo tena.
Mahusiano yao mengini ni kuwa, Mwanzilishi wa Mashahidi wa Yehova Charles Taze Russell, aliingiza mafundisho ya Wasabato kuhusu siku ya mwisho. Wakati Russell alipo kuwa na miaka 23 alifundishwa mafundisho ya Nelson H. Barbour ambaye ni Msabato na kwamba Yesu atarudi bila ya kuonekana mwaka 1874, ingawa Msabato William Miller alidai hapo nyuma kuwa Yesu atarudi kwa mara ya pili mwaka wa 1843.
Wote wawili Russell na Barbour wanaamini kuwa Yesu alirudi bila ya kuoneka mwaka wa 1874 na kwamba katika "Spring" ya mwaka 1878 kutatokea kunyakuliwa kwa Kanisa. Kunyakuliwa kwa Kanisa kulipo shindikana kutokea, Barbour alikuja na utabiri mwengine "new light" na mafundisho mengine mengi kusaidia ujumbe wake, lakini Russell alikataa kuyakubali.
Russell ndio akajitoa kutoa Kanisa la SDA-WASABATO ambalo ndio lilianzishwa na Ellen G. White. Ilipo fika mwaka wa 1874 Russell alianzisha kikundi kinacho itwa Wanafunzi wa Biblia. Na Julai ya 1879 Russell alichapisha jarida la Watch Tower and Herald of Christ's Presence. Mwaka 1882 Russell alikana UTATU wa Mungu, na ilipo fika 1916 Russell alifariki.
Leo tumejifunza kuhusu kushabihana na kufanana kwa hawa wawili, Mashahidi wa Yehova na SDA- Wasabato. Wote hawa walianzia katika vuguvugu la mwaka wa
Mungu awabariki sana,
Max Shimba
For Max Shimba Ministries Org.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW