Sunday, February 14, 2016

MUHAMAMD AMESEMA SHETANI ANAISHI KWENYE PUA ZA WAISLAM WOTE NA NZI WACHAFU NI DAWA.

1. ETI, SHETANI ANAISHI KWENYE PUA YAKO
2. ETI NZI WACHAFU NI DAWA

Ndugu msomaji,
Huu ni msiba:
1. ETI, SHETANI ANAISHI KWENYE PUA YAKO
Shetani Puani Mwako?
"Abu Huraira alisimulia: Nabii alisema, ‘Kama mtu yeyote kati yenu akiamka toka usingizini na kutawadha [kaida ya kujitakasa], anapaswa kuosha pua yake mara tatu kwa kuingiza maji na kuyatoa kwa kuhema kwa sababu Shetani alikuwa kwenye sehemu ya juu ya pua yake usiku mzima."(1) Maelezo ya mwenye kutafsiri (1) yanasema, "Tunapaswa kuamini kuwa ni kweli kwamba Shetani anakaa kwenye sehemu ya juu ya pua ya mtu hata kama hatuwezi kuelewa kwa sasa, kwani jambo hili linahusika na ulimwengu usioonekana ambao hatujui lolote kuhusiana nao isipokuwa yale ambayo Mwenyezi Mungu ametuambia kupitia Mtume wake." Bukhari sura ya 4 kitabu cha 54 (Mwanzo wa Uumbaji) sura ya 10 na.516 uk.328.
Huu nu uongo mkubwa sana ambao Muhammad amesema katika umma yake.
[Moja]: Shetani hana uwezo wa kuwa kila mahali kwa wakati mmoja [omnipresence]
[Mbili]: Shetani ni roho na hana geographical location katika mwili wa bindamu.
[Tatu]; Labda Shetani anaishi kwenye pua za Waislam pekee. Maana ukimpokea Yesu na kujazwa na Roho Mtakatifu, Shetani hawezi kuwa anaishi kwenye pua yako kama anavyo ishi kwenye pua za Waislam wote.
2. ETI NZI WACHAFU NI DAWA
Kumwamini Muhammad Wakati Nzi Wanakuwepo:
"Abu Huraira alisimulia: Nabii alisema, ‘Kama nzi ameangukia kwenye kinywaji cha mtu yoyote kati yenu, na amchovye (kwenye kinywaji), kwani bawa lake moja lina ugonjwa na lingine lina tiba ya huo ugonjwa." Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 54 (Mwanzo wa Uumbaji) sura ya 16 na.537 uk.338. Tazama pia Abu Dawud juzuu ya 3 kitabu cha 21 (Kitabu cha Vyakula) na.3835 uk.1080.
"Abu Huraira alisimulia: Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema, ‘Kama nzi ameangukia kwenye chombo cha yoyote kati yenu, mtu huyo na amchovye huyo nzi (kwenye chombo) kisha amtupe, kwani kwenye bawa lake moja kuna ugonjwa na kwenye lingine kuna uponyaji (1) (kiuasumu), yaani tiba ya ule ugonjwa." Bukhari juzuu ya 7 kitabu cha 71 (Kitabu cha Dawa) sura ya 58 na.673 uk.452-453.
Maelezo ya mwenye kutafsiri 

(1) yanasema, "Katika taaluma ya uganga inafahamika sana siku hizi kwamba nzi hubeba vijidudu vinavyosababisha magonjwa [pathogens] kwenye baadhi ya sehemu za mwili wake kama alivyosema Nabii (karibu miaka 1400 iliyopita wakati ambapo binadamu walikuwa na ufahamu mdogo sana wa uganga wa kisasa.) Vivyo hivyo, Mungu aliumba vumbe na namna za utendaji vinavyoua hivi vijidudu vyenye kusababisha magonjwa mf. Kuvu ya penicillin (penicillin Fungus) huua vijidudu kama Staphalococci na vinginevyo. Hivi karibuni majaribio yaliyofanywa chini ya usimamizi yameonyesha kuwa nzi hubeba ugonjwa (pathagens) pamoja na viuasumu vya vijidudu hivyo. Kwa kawaida nzi anapogusa chakula kinachomiminika huathiri kimiminika kwa vijidudu vyake, hivyo ni lazima kumchovya ili aweze kutoa viuasumu vya vijidudu hivyo kwa lengo la kusawazisha vijidudu hivyo. Kuhusiana na somo hili pia niliandika kwa rafiki yangu kupitia kwa Dr. Muhammad M. El-SAMAHY, mkuu wa idara ya hadithi ya Chuo Kikuu cha Al-Azhar CAIRO (Misri) ambaye ameandika makala kuhusu Hadithi hii na kuhusiana na taaluma ya uganga amesema kuwa wataalamu wa vijidudu vidogo (microbiologists) wamethibitisha kuwa kuna chembe chachu zenye kukata kwa urefu zinazoishi kama vimelea ndani ya tumbo la nzi na chembe hizi chachu hujichomoza kupitia mishipa ya kupumulia ya nzi na kama mtu akimchovya nzi kwenye kimiminika, chembe hizi hupasuka kwenye kimiminika na vitu vilivyomo kwenye chembe hizi ni viuasumu vya vijidudu ambavyo nzi huvibeba."
Karibu madaktari wote, kama si Waislam, hudhihaki wakisika kuhusu kumchovya nzi kwa makusudi kwenye kinyaji chako.
Mungu awabariki sana,
Katika Huduma Yake,
Max Shimba Ministries Org.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2015. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW