Friday, June 2, 2017

USIOGOPE TENA: YESU KRISTO NI DHABIHU YA UPATANISHO

Image may contain: 1 person, standing, mountain, outdoor, nature and text
“Mungu, ambaye huwafariji wale walioshushwa chini, alitufariji.” —2 WAKORINTHO 7:6.
Mungu amefanya mengi kuwasaidia na kuwafariji wanadamu. Wanadamu wote wamerithi dhambi, hivyo hakuna anayeweza kufuata viwango vya Mungu kikamili. Hata hivyo, Mungu “alitupenda akamtuma [Yesu Kristo] Mwana wake kuwa dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi zetu.” (1 Yohana 4:10) Kupitia kifo cha kidhabihu cha Yesu, Mungu amefanya iwezekane kwa wanadamu kupata msamaha wa dhambi, dhamiri njema, na tumaini la uzima wa milele katika ulimwengu mpya wenye amani. * Je, dhabihu hiyo ni kwa ajili ya wanadamu wote, au pia inaweza kukunufaisha wewe binafsi?
Mfikirie mtume Paulo. Alichochewa sana na dhabihu ya Yesu hivi kwamba akaandika: “Naishi kwa imani ambayo ni kumwelekea Mwana wa Mungu, aliyenipenda mimi na kujitoa mwenyewe kwa ajili yangu.” (Wagalatia 2:20) Kwa kweli, Yesu alikufa kabla Paulo hajawa Mkristo. Hata hivyo, Paulo aliona dhabihu hiyo kuwa zawadi ya Mungu kwake binafsi.
Kifo cha kidhabihu cha Yesu ni zawadi ya kibinafsi kwako wewe pia. Zawadi hiyo inaonyesha jinsi Mungu anavyokuthamini. Inaweza kukupatia “faraja ya milele na tumaini jema” na hivyo ‘kukuimarisha wewe katika kila tendo na neno jema.’—2 Wathesalonike 2:16, 17.
Shalom,
Max Shimba Mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW