Tuesday, June 6, 2017

SAFARI YA KUSISIMUA YA HANA MAMA YAKE NABII SAMWELI -SEHEMU YA PILI-

Image may contain: 2 people, people standing
Mfano wa Hana unatukumbusha nini kuhusu sala?
Kwa hiyo, Hana ni mfano muzuri sana kwa watumishi wote wa Mungu kuhusiana na sala. Mungua anawaomba wajisikie huru kuzungumza naye, bila kusita, wamtupie mahangaiko ya moyo wao kama vile mutoto anayemutumainia baba yake. (Soma Zaburi 62:8; 1 Wathesalonike 5:17.) Mtume Petro aliongozwa na Roho ya Mungu ili kuandika maneno haya yenye kufariji kuhusu sala zetu kwa Mungu: ‘Mtupe mahangaiko yenu yote juu yake, kwa sababu yeye [anawahangaikia] ninyi.’—1 Petro 5:7.
(a) Namna gani na sababu gani Eli anamuwazia Hana vibaya? (b) Namna gani jibu la Hana kwa Eli ni mufano muzuri sana wa imani?
Kwa kawaida, wanadamu hawawaelewe wengine na hawajitie pa nafasi ya wengine kama Mungu. Ndio sababu, Hana anaposali na kulia, sauti ya mtu fulani inamshitua. Ni sauti ya Eli, kuhani mkubwa, aliyekuwa anamtazama. Kuhani huyo anamuambia hivi: ‘Utaendelea kujiendesha kama mlevi mpaka wakati gani? Iondolee mbali divai yako.’ Eli anaona midomo ya Hana inatetemeka, ni mwenye kulia na mwenye uchungu sana. Kuliko kumuuliza magumu yake ni nini, yeye anawaza mara moja kwamba Hana ni mulevi.—1 Samueli 1:12-14.
Kulaumiwa bila sababu yoyote wakati huu wa taabu yake, zaidi sana na mwanaume aliye na cheo chenye kuheshimika, kunamuumiza Hana zaidi! Hata hivyo, mara hii tena, yeye anatuachia mufano muzuri wa imani. Haache kumuabudu Mungu kwa sababu ya uzaifu wa mtu fulani. Na anamujibu Eli kwa adabu na kumuelezea hali yake. Eli anatambua kwamba alikosea, kwa hiyo, labda ndio sababu anamujibu hivi kwa upole: ‘Nenda kwa amani, naye Mungu wa Israeli akupe ombi lako ambalo umemuomba.’—1 Sam. 1:15-17.
(a) Kwa sababu Hana anamufungulia Mungu moyo, na anaendelea kumuabudu kwenye hema ya ibada, anajisikia namna gani?
(b) Namna gani tunaweza kufuata mufano wa Hana tunapolemewa na magumu ao huzuni?
Matokeo yanakuwa namna gani wakati Hana anamufungulia Mungu moyo na anaendelea kumuabudu kwenye hema ya ibada? Biblia inasema hivi: ‘Mwanamuke huyo akaenda zake, akakula chakula, na uso wake haukuwa tena na huzuni.’ (1 Samueli 1:18, La Sainte Bible en Swahili de la R. D. Congo) Hana anajisikia mwenye kutulizwa. Tunaweza kusema kama alitia uzito wa mhangaiko yake kwenye mabega ya mtu mwenye nguvu sana kuliko yeye, ni kusema, Baba yake wa mbinguni. (Soma Zaburi 55:22.) Je, kuna tatizo lolote linaloweza kumshinda? Hakuna hata kidogo: iwe jana, iwe leo ao kesho!
Tunapojisikia kulemewa, magumu yanatupita ao tuna huzuni kupita kiasi, ni vizuri kufuata mufano wa Hana na kuzungumuza na Mungu ‘Msikiaji wa sala’ bila kusita. (Zab. 65:2) Tukifanya hivyo kwa imani, kuliko kuwa na huzuni, tutakuwa na “amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote.”—Flp. 4:6, 7.
“Hakuna Mwamba Ulio Kama Mungu Wetu”
(a) Ni nini inaonyesha kama Elkana anaunga mukono naziri ya Hana?
(b) Penina hana tena uwezo gani juu ya Hana?
Asubuhi inayofuata, Hana anarudi tena kwenye hema pamoja na Elkana. Hakukosa kumuelezea bwana yake kuhusu ombi na naziri aliyofanya, kwa kuwa Sheria ya Musa inasema kwamba bwana ana haki ya kuvunja naziri ambayo bibi yake alifanya bila kumuuliza bwana yake maoni yake. (Hes. 30:10-15) Lakini, mwanaume huyo mwaminifu havunje naziri hiyo. Kuliko kufanya hivyo, yeye na Hana wanamuabudu Yehova pamoja kwenye hema mbele ya kushika njia yao na kurudi nyumbani.
Ni wakati gani kabisa Penina alitambua kuwa uchokozi wake haumuhuzunishe tena Hana? Biblia haizungumuzie jambo hilo, lakini maneno ‘uso wake haukuwa tena na huzuni,’ yanaonyesha kama kuanzia wakati huo Hana alirudiliwa na furaha yake. Kwa vyovyote, Penina aliona kama mazarau yake hayakuwa na matokeo juu ya Hana. Na Biblia haitaje tena jina la Penina.
Ni baraka gani ambayo Hana anapata, na namna gani anaonyesha kama alijua yule aliyemupatia baraka hiyo?
Miezi inapita, amani ya Hana inaongezeka na anakuwa mwenye furaha sana. Ni mwenye kuwa na mimba! Hana anafurahi sana, lakini hasahau hata kidogo ni nani amemubariki hivyo. Mtoto anapozaliwa, anampatia jina la Samweli, linalomaanisha “Jina la Mungu,” na kwa kweli jina hilo linaonyesha tendo la kuitia jina la Mungu kama Hana alivyofanya. Mwaka huo Hana haende Shilo pamoja na Elkana na jamaa yote. Anabaki nyumbani pamoja na mtoto kwa miaka mitatu mpaka wakati mtoto anaachishwa kunyonya. Sasa anajitayarisha kwa ajili ya siku ambayo ataachana na mwana wake mupendwa.
Namna gani Hana na Elkana wanatimiza mambo waliyomuahidia Mungu?
Si jambo rahisi kwa Hana kuachana na mtoto wake. Bila shaka, Hana anajua kama Samweli atatunzwa vizuri huko Shilo; inaonekana ni wanawake fulani wanaotumika katika hema ya ibada ndio watamtunza. Hata hivyo, kijana Samweli angali bado mutoto sana na tunajua kwamba si vyepesi kwa mama kuachana na mtoto ambaye angali mchanga. Lakini, Hana na Elkana wanampeleka mtoto huko kwenye nyumba ya Mungu, hawafanye hivyo wakiwa na kinyongo, lakini wanafanya hivyo kwa furaha. Wanatoa zabihu na kisha wanamuacha Samweli katika mikono ya Eli, wanamkumbusha Eli naziri ambayo Hana alifanya hapo miaka fulani iliyopita.
Hana alikuwa baraka kabisa kwa Samweli
Namna gani sala ya Hana inaonyesha kwamba alikuwa na imani yenye nguvu?
Kisha Hana anatoa sala ambayo Mungu aliona kama inastahili kutiwa katika Neno lake lililoongozwa na roho. Unaposoma maneno ya Hana katika 1 Samweli 2:1-10, utaona kama kila mustari unaonyesha imani yenye nguvu ya mwanamuke huyo. Anamusifu Mungu namna anavyotumia kwa ajabu nguvu zake na uwezo wake usiolinganishwa ili kuwashusha wenye kujivuna, kuwabariki wanaoonewa, na namna alivyo na uwezo wa kuua na hata wa kuokoa kutoka katika kifo. Anamsifu Baba yake wa mbinguni kwa kuwa ni mtakatifu zaidi, ni mwenye haki, na ni mwaminifu. Hana ana haki ya kusema hivi: “Hakuna mwamba ulio kama Mungu wetu.” Mungu anastahili kabisa kutumainiwa, yeye habadilike, ni kimbilio kabisa kwa wote wanaoonewa na kugandamizwa na ambao wanamuomba musaada.
(a) Sababu gani tuko hakika kwamba Samweli anaendelea kukomaa akiwa mwenye kujua kwamba wazazi wake wanampenda?
Namna gani Mungu anaendelea kumbariki Hana?
Bila shaka, kijana Samweli ana pendeleo kabisa la kuwa na mama aliye na imani kama hiyo kwa Mungu. Hata ikiwa anakomalia mbali naye, hajisikie hata kidogo kuwa anasahauliwa. Kila mwaka, Hana anakuja Shilo; anamletea koti lisilo na mikono ambalo Samweli atavaa anapomutumikia Mungu katika hema. Kumshonea yeye mwenyewe koti hilo kunaonyesha kama anamupenda na kumhangaikia mwana wake. (Soma 1 Samweli 2:19.) Funga macho kidogo: unamuona Hana akimuvalisha kijana wake koti hilo, akilinyoosha, na kumtazama kwa upendo anapomutia moyo na kuzungumza naye kwa fazili? Samweli ni mwenye kubarikiwa kabisa kuwa na mama kama huyo, naye anapoendelea kukomaa, anakuwa baraka kubwa kwa wazazi wake na kwa Waisraeli wote.
Mungu pia hamsahau Hana. Anafungua tumbo lake la uzazi kabisa, na anamuzalia Elkana watoto wengine watano. (1 Samueli 2:21) Hata hivyo, labda baraka kubwa ambayo Hana anapata ni uhusiano wa karibu sana alio nao na Mungu, ambao unaendelea kuwa nguvu kadiri miaka inavyopita. Acha iwe hivyo pia kwako, wakati unapoendelea kuiga imani ya Hana.
USIKOSE SOMO KUHUSU "SAMWELI MTUME BAADA YA MUSA....
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW