Friday, June 9, 2017

MPIGENI IBILISI NAE ATAWAKIMBIA

Image may contain: one or more people, people sitting and text
Ufunuo wa Yohana 20:1-3
“1 kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake. 2 Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na shetani, akamfunga miaka elfu. 3 Akamtupa katika kuzimu, akamfunga, akatia muhuri juu yake, asipate kuwadanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe muda mchache.”
“Yule nyoka wa zamani, yeye anayeitwa Ibilisi na Shetani, anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa.”—Ufunuo 12:9.
Shetani ni kiumbe halisi. Yeye ni malaika mwasi, kiumbe wa roho anayempinga Mungu. Biblia inamwita Shetani “mtawala wa ulimwengu huu.” (Yohana 12:31) Yeye hutumia “ishara za uwongo” na “udanganyifu” kutimiza makusudi yake.—2 Wathesalonike 2:9, 10.
Shetani anaishi wapi?
“Ole wa dunia . . . kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu.”—Ufunuo 12:12.
Je, hilo linamaanisha kwamba Shetani anakaa mahali fulani hususa duniani?
Kwa mfano, huenda umesoma kuhusu jiji la kale la Pergamamu ambalo lilisemekana kuwa mahali “anapokaa Shetani.” (Ufunuo 2:13) Kwa kweli, maneno hayo yalimaanisha kwamba ibada ya kishetani ilikuwa imekita mizizi mahali hapo. Shetani haishi mahali fulani hususa duniani, labda Makka. Kinyume cha hilo, Biblia inasema kwamba “falme zote za dunia inayokaliwa” ni mali yake.—Luka 4:5, 6.
BIBLIA INASEMA NINI?
Wanadamu wengi wamejiacha washindwe na uvutano wenye kupotosha wa Shetani na kwa hiyo wako chini ya nguvu zake. (2 Wakorintho 11:14) Jambo hilo linatusaidia kuelewa ni kwa nini wanadamu wameshindwa kuboresha hali ulimwenguni.
Biblia pia inataja visa ambapo Shetani na malaika wengine waasi wamewafanya watu kuwa chini ya uvutano wao na kuwadhuru kimwili.—Mathayo 12:22; 17:15-18; Marko 5:2-5.
UNAWEZA KUFANYA NINI?
Hupaswi kuogopa nguvu za Shetani. Ili uepuke kushindwa na uvutano wake, unahitaji kujua jinsi anavyowadanganya watu, ili ‘usikose kuzijua mbinu zake.’ (2 Wakorintho 2:11) Kwa kusoma Biblia, unaweza kupata ujuzi muhimu kuhusu mbinu za Shetani na hivyo uepuke kunaswa naye.
Tupilia mbali vitu vyovyote vinavyohusiana na utendaji wa roho waovu. (Matendo 19:19) Vitu hivyo vinatia ndani hirizi, vitabu, video, muziki, na programu za kompyuta ambazo zinaendeleza zoea la kuwasiliana na pepo au uaguzi.
“Mpingeni Ibilisi,” Biblia inasema, “naye atawakimbia ninyi.” (Yakobo 4:7) Ukitii shauri lenye hekima la Biblia, unaweza kujilinda dhidi ya hila za Shetani.—Waefeso 6:11-18.
MPIGENI IBILI KWA JINA LA YESU, NAE ATAWAKIMBIA.
Unao ushindi katika Yesu Kristo,Bwana wetu na Mungu wetu Mkuu.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW