Friday, December 7, 2018

WAPI YESU KASEMA WATU WAWE WAKRISTO?




WAPI YESU KASEMA WATU WAWE WAKRISTO?
Hili ndilo swali dhaifu linalo ulizwa na ndugu zetu kila kukicha. Leo nawajibu kwa aya ili wanyamaze milele yote.
Marko 9: 39 Yesu akasema, Msimkataze, kwa kuwa hakuna mtu atakayefanya mwujiza kwa jina langu akaweza mara kuninenea mabaya;
40 kwa sababu asiye kinyume chetu, yu upande wetu.
41 Kwa kuwa ye yote atakayewanywesha ninyi kikombe cha maji, kwa kuwa ninyi ni watu wa Kristo, amin, nawaambia, hatakosa thawabu yake.
Katika aya ya 41, Yesu anasema sisi ni watu wa Kristo. Je, mtu wa Kristo ni nani kama sio Mkristo?
Je, hawa watu waliomfuata Yesu waliitwa Wakristo?
Matendo 11: 26 hata alipokwisha kumwona akamleta Antiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. Na wanafunzi waliitwa Wakristo kwanza hapo Antiokia.
Neno la Mungu linakujibu kuwa, wanafunzi wa Yesu ambao ni sisi tunaitwa Wakristo.
Je, dai la Ukristo ni dini linathibitishika kama wanavyo lazimisha Waislam?
3.Suurat Al 'Imran 99. Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Kwa nini mnamzuilia aliye amini NJIA ya Mwenyezi Mungu mkiitafutia kosa, na hali nyinyi mnashuhudia? Na Mwenyezi Mungu si mwenye kughafilika na mnayo yatenda.
Waislam wanakiri kuwa NJIA YA MWENYEZI MUNGU NI DINI. YAANI DINI NI NJIA. JE, NJIA HII YA MWENYEZI MUNGU NI IPI?
Soma: "Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi." Yohana 14:6
YESU ANASEMA YEYE NI NJIA. WAISLAM WANASEMA DINI NI NJIA, KUMBE BASI UKRISTO KWA TAFSIRI YA WAISLAM NI DINI.
1 Petro 4:16 Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina hilo.
KUMBE JINA LA UKRISTO NI LA KUMTUKUZA MUNGU KAMA ILIVYO THIBITISHWA KWENYE PETRO HAPO JUU.
Sasa tusome Tafsir ya Bharwani hapa chini: 1.Suurat An Nahl 125
Maelezo: Suuratun Nah'l * 125. Ewe Nabii! Lingania, uwite watu kwenye Njia ya Haki ambayo Mola wako Mlezi amewataka watu wako waifuate. Na katika huo Wito wako pita njia ambayo inamnasibu kila mmoja wao. Waite wenye vyeo vya juu katika wao kwa maneno ya hikima kwa mujibu wa akili zao. Na watu wa kawaida walio baki kati yao walinganie kwa kuwapa mawaidha yanao waelekea, na kuwapigia mifano ya mambo wanayo pambana nayo ya kuwapeleka kwenye Haki, na uwaongoze kwenye njia fupi inayo wanasibu. Na jadiliana na watu wa dini zilizo tangulia katika watu wa Biblia, yaani Mayahudi na Wakristo, kwa kutumia hoja za kiakili, Mant'iqi, na maneno laini, na majadiliano mazuri, si maneno ya ukali na matusi, ili uwakinaishe na uwavutie. Hii ndiyo njia ya Daa'wa (Wito), kuwaita watu kumwendea Mwenyezi Mungu -watu wa mila zote. Basi ifuate njia hii unapo waita, na baada ya hayo yaliyo baki mwachilie Mola wako Mlezi, ambaye anamjua aliye zama katika upotovu kati yao na akawa mbali na njia ya uwokovu, na nani ambaye aliye salimika, akaongoka, na akayaamini hayo uliyo waletea.
ALLAH ANASEMA UKRISTO NI DINI ILIYO TANGULIA. KUMBE UISLAM HAUKUWEPO KABLA YA UKRISTO. http://www.iium.edu.my/deed/quran/swahili/without/c16.htm…
JE , NIKWELI UKRISTO NA KANISA VILIKUWEPO KABLA YA UISLAM.
Tumsome Musa, Je aliingia KANISANI?
Matendo ya Mitume 7: 37 Musa huyo ndiye aliyewaambia Waisraeli, Bwana Mungu wenu atawainulieni nabii, katika ndugu zenu, kama mimi; msikieni yeye.
38 Yeye ndiye aliyekuwa katika kanisa jangwani pamoja na yule malaika aliyesema naye katika mlima wa Sinai, tena pamoja na baba zetu; ndiye aliyepokea maneno ya uzima atupe sisi.
Musa anawajibu waislam kuwa yeye aliingia Kanisa alipo kuwa Jangwani. Kumbe Musa hakuwa Muislam wala hakuwai ingia Msikitini.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW