Friday, December 7, 2018

UISLAMU SI MAHALI SALAMA PENYE UHURU NA USAWA

Image may contain: one or more people and textHata tukidhani kimakosa kuwa uislam ulianzia Afrika na kwamba Nabii wake alikuwa mweusi, hii pekee yake haitakuwa sababu nzuri kwa weusi kuasiri uislam.
Hata haitakuwa sababu nzuri kwa wazungu kuasiri uislamu kwasababu tu Muhammad alikuwa mweupe. Tunapaswa kuuangalia uislamu wenyewe.
Nisingependa niwe Muislam kwa sababu uislam hupingana na uhuru, kitu ambacho kipo karibu sana na mioyo na nia za Waamerika wenye asili ya Kiafrika, ukizingatia dhuluma waliyoipata hapo zamani.
Kitu kimoja ambacho uislam hauamini ni uhuru wa kidini. Ikiwa uislam utaichukua Amerika hapatakuwa na uhuru wa kidini. Koran inasema, "Ikiwa mtu yeyote ataka dini nyingine licha ya uislam, jambo hili halitakubaliwa kwake kamwe; na katika maisha yajayo mtu huyu atakuwa katika kundi la waliopotea (Sura 3:85).
Mafundisho mengi ya uislam hayaendani na na maendeleo na nyakati. Na pia hayaendani na haki za binadamu, haki za kiraia au haki za kikatiba.
Ifuatayo ni mifano michache ya uislam Wanaume ni bora kuliko wanawake (Sura 2:228) Wanawake wana haki nusu ya zile za wanaume:
haki za kutoa ushahidi mahakamani (Sura 2:282) haki za mirathi (Sura 4:11)
Mwanaume aweza kumpiga mkewe (Sura 4:34) Mwanaume aweza kuoa wake hadi wanne kwa wakati mmoja (Sura 4:3) Waislam lazima wapigane mpaka wapinzani wao wajisalimishe kwenye uislam (Sura 9:5) Muislam asiwe na rafiki Myahudi wala Mkristo (Sura 5:54) Mtu anayeasi uislamu lazima auawe (Sura 9:12) Wizi huadhibiwa kwa kukata mikono (Sura 5:41) Ugoni huadhibiwa kwa kupigwa mijeredi hadharani (Sura 24:2) Hakuna utengano kati ya kanisa [dini] na serikali. (Sura 2:193) Hakuna upinzani utakaoruhusiwa hata kidogo (Sura 4:59)
Mwamerika mwenzangu mwenye asili ya Kiafrika
Kwa kusema kuwa uislam ni dini ya mtu mweusi, wakereketwa wa uislam wanaonyesha tu chuki yao halisi na ubaguzi wa rangi. Usiliache hili likakurubuni.
Waislam hawajali rangi ya ngozi yako, wanatumia usemi huo tu ili wapate kukuteka. Maana kama Waislam wangelikuwa wanajali watu weusi, kwa nini Waislam weusi wanawateka ndugu zao Wakristo weusi huko Sudan siku hizi, wakiwachinja wanyonge na kuwauza wenye afya kama watumwa (angalia taarifa ya Idara ya Taifa [State Dept]: Habari za Mtandao wa Kimataifa; Mei 26, 1993).
Zingatia, upande mwingine, kuwa Yesu Kristo alikuja kutupa uzima wa milele, ambapo kila mmoja ni sawa mbele za Mungu.
"Hapana Myahudi wala Myunani. Hakuna mtumwa wala aliyehuru. Hakuna mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu" (Wagalatia 3:28).
Tofauti kati ya mafundisho ya kiislam na mafundisho ya Yesu Kristo ni kubwa. Uchaguzi uko wazi, na uchaguzi huu ni wako mwenyewe.
IJUE KWELI
IFUATE KWELI
ISAMBAZE KWELI

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW