Wednesday, March 21, 2018

CHANZO CHA UHAI WAKO NI NINI AU NANI?

Image result for beginning of life
Mwili wako ni kati ya vitu tata sana ulimwenguni. Umefanyizwa kwa chembe ndogo zipatazo trilioni 100—chembe za mifupa, chembe za damu, chembe za ubongo, na kadhalika. Kuna aina tofauti-tofauti zaidi ya 200 ya chembe katika mwili wako.

Licha ya kutofautiana katika umbo na jinsi zinavyotenda kazi, chembe zako zinafanyiza mtandao tata uliounganishwa kwa njia ya ajabu. Intaneti, pamoja na mamilioni ya kompyuta na nyaya zake zinazoweza kutuma data kwa kasi, ni duni sana ikilinganishwa na mtandao huo. Hakuna uvumbuzi wowote wa mwanadamu unaoweza kulinganishwa na ustadi wa hali ya juu unaoonekana katika hata zile chembe za msingi zaidi. Chembe zinazofanyiza mwili wa mwanadamu zilitoka wapi?

Wanasayansi wengi husema nini?

Chembe zote zilizo hai ziko katika vikundi viwili—zenye kiini na zisizo na kiini. Chembe za wanadamu, wanyama, na mimea zina kiini. Chembe za bakteria hazina kiini. Chembe zenye kiini huitwa eukaryotic. Chembe zisizo na kiini huitwa prokaryotic. Kwa kuwa chembe zisizo na kiini si tata sana kama zile zenye kiini, watu wengi huamini kwamba chembe za wanyama na mimea zilitokana na chembe za bakteria.


Inawezekana kweli kwamba aina tofautitofauti zaidi ya 200 za chembe zinazofanyiza mwili wako zilijitokeza kiholela?

Je, kweli hata chembe “sahili” ingeweza kutokana na kemikali zisizo hai?

Wengi hufundisha kwamba kwa mamilioni ya miaka, baadhi ya chembe “sahili” zisizo na kiini zilimeza chembe nyingine lakini hazikuzimeng’enya. Badala yake, kulingana na nadharia hiyo, tukio fulani la “asili” lisilotegemea akili, lilifanyiza mabadiliko muhimu kuhusiana na utendaji-kazi wa chembe zilizomezwa na pia kuendelea kuzihifadhi chembe hizo ndani ya chembe “kimelewa” (iliyozimeza) ilipokuwa ikijigawanya.

Biblia inasema nini?

Biblia inasema kwamba uhai ulio duniani ulitokana na Muumba mwenye akili. Fikiria maneno haya ya Biblia: “Bila shaka, kila nyumba hujengwa na mtu fulani, lakini yeye aliyevijenga vitu vyote ni Mungu.” (Waebrania 3:4) Kifungu kingine cha Biblia kinasema: “Jinsi kazi zako zilivyo nyingi, Ee Yehova! Zote umezifanya kwa hekima. Dunia imejaa vitu ulivyotokeza.

. . . Humo mna vitu vyenye kutambaa visivyo na hesabu, viumbe hai, vidogo kwa vikubwa.”—Zaburi 104:24, 25.

Uthibitisho unafunua nini?
Maendeleo katika elimu ya mikrobiolojia yamewawezesha wanasayansi kuchunguza sehemu yenye kustaajabisha ya ndani ya chembe hai sahili za prokaryotic zinazojulikana. Wanasayansi wanaounga mkono mageuzi wanakisia kwamba chembe za kwanza zilizo hai zilifanana na chembe hizo.

Ikiwa nadharia ya mageuzi ni ya kweli, basi inapaswa kueleza kinagaubaga jinsi chembe “sahili” ya kwanza ilivyojitokeza yenyewe. Kwa upande mwingine, ikiwa uhai ulitokana na Muumba, kunapaswa kuwa na uthibitisho wa ubunifu wa hali ya juu hata katika viumbe vidogo sana. Kwa nini usitembelee
chembe ya prokaryotic? Unapoichu Hakuna majaribio yoyote yaliyofanywa kuthibitisha kwamba tukio hilo linawezekana. nguza, jiulize ikiwa chembe hiyo inaweza kujitokeza yenyewe.

UKUTA UNAOILINDA CHEMBE

Ili uingie ndani na kuchunguza chembe ya prokaryotic, utahitaji kusinyaa na kuwa mdogo zaidi ya nukta iliyo mwishoni mwa sentensi hii. Chembe hiyo inalindwa na utando wenye kunyumbulika unaotenda kama ukuta wa matofali Unaokizunguka kiwanda. Utando huo ni Mwembamba sana hivi kwamba matabaka 10,000 ya utando huo yanalingana na unene wa karatasi moja. Hata hivyo, utando wa chembe ni tata sana kuliko ukuta wa matofali.

Jinsi gani?

Kama ukuta unaolinda kiwanda, utando wa chembe hulinda vitu vilivyo ndani dhidi ya hatari inayoweza kutokea. Hata hivyo, utando huo si mgumu; unaruhusu chembe “kupumua” na hivyo kuwezesha molekuli ndogo, kama oksijeni, kuingia au kutoka. Lakini utando huo huzuia molekuli zilizo tata zaidi zinazoweza kusababisha madhara zisiingie bila chembe kuziruhusu. Utando huo pia huzuia molekuli zenye manufaa zisitoke nje ya chembe. Utando huo hufanya hivyo jinsi gani?

Kifikirie tena kiwanda. Huenda kina walinzi wanaochunguza bidhaa zinazoingia na kutoka kiwandani kupitia milango iliyo kwenye ukuta. Vivyo hivyo, utando wa chembe una protini za molekuli maalum zinazotenda kama milango na walinzi.

Shalom

Max SHimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu. Titop 2:13

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW