Monday, March 19, 2018

KUTO KUWEPO "NOTHING" HAKUWEZI KUUMBA KITU

Image result for creation ex nihilo
Kwanza, ifuatayo ni njia rahisi na yenye mantiki rahisi yenye kuelezea.
Haya, tuanze kufikicha akilia na Max Shimba.

Huwezi kupata kitu bila kuwa na kitu (kingine). Kila kitu kilichoumbwa kilihitajika kuumbwa. Hata vitu vya kwanza kuumbwa vilihitajikwa kuumbwa na kitu/mtu mwingine ambaye aliisha kuwepo. Kwa hiyo, panatakiwa kuwa na kitu au mtu ambaye hajaumbwa na anaishi milele.
Yafuatayo ni maelezo makali; maana ni zangu mwenyewe.
Tunadhani kuwa kila mtu anaufahamu wa kutosha kuweza kuwa na maana inayofaa ya mantiki, kupingana na kutopingana, tukio, mchakato, "ndani ya", kitu, mkusanyiko, muda, mada, nishati, roho, chanzo, kilichosababishwa na, na matokeo.

Uwepo halisi kunafafanuliwa, katika makala hii, kuwa ni kuwepo kwenye ulimwengu huu, kuwa na uwezo wa kuathiriwa na kitu mojawapo hapa ulimwenguni, au kuwa na uwezo wa kuathiri kitu kimojawapo hapa ulimwenguni. Huu ni ufafanuzi mfinyu sana wa kuwepo/kuishi, kwani unashindwa kuhusisha mawazo, mienendo, na mambo mengine. Kwa hiyo, hebu na tuuite uwepo "halisi" na tufanye majadiliano yetu hapa yakomee kwenye uwepo halisi.

Kitu halisi kinafafanuliwa hapa kuwa ni kitu au mkusanyiko au mada, nishati, roho, au mchanganyiko wenye kuwa na uwepo halisi. Ukweli wa kimantiki, ukinzani wa kimantiki, na ushahidi wa kihesabu havichukuliwa kuwa vitu hapa.

Uwepo wa kimelea, kama kitu cha ndani, unfafanuliwa kuwa ni uwepo halisi wa vitu ambavyo si vitu halisi. Mashimo, giza, upungufu, kutokuwa sahihi, na maovu si mada, nishati, au roho, lakini kama ambavyo kivuli kinaweza kuua mimea ambayo inahitaji jua, au upungufu ea chakula unavyoweza kuua mtu, vivuli na upungufu wa chakula vina uwepo halisi licha ya kutokuwa vitu halisi.

Ulimwengu unafafanuliwa hapa kuwa ni mkusanyiko wa vitu halisi ambavyo vipo kiuhalisi. Tazama kuwa katika ufafanuzi huu, ulimwengu unajitisheleza, na Mungu (tuchulie kuwa Mungu yupo, ni roho na anaweza akaathiri vitu) yupo ulimwenguni.

Kutokwepo (nothing) kunafafanuliwa kuwa ni kitu ambacho hakijawahi kabisa kuwepo, au ambacho hakijawahi kuwa na uwepo wa kweli/kihalisi wakati wowote ule. Kwa maneno mengine, kabla hakijaumbwa [au baaday ya kuharibiwa], kitu halisi hakipo ulimwenguni, hakiuathiri ulimwengu, na hakiathiriki na ulimwengu.

Uumbaji unafafanuliwa hapa kuwa ni tukio au mchakato wa kufanya kitu halisi kipya. Kuumba kunatofautishwa na "kubadilisha", ambako hakuhitaji chanzo chochote mbali ya kitu chenyewe. Kuumba kitu halisi kipya kunaweza kuhusisha kubadilisha au kuharibu kitu halisi kilichowahi kuwepo, lakini hakulazimiki kufanya hivyo. Hata hivyo, angalia sehemu inayofuata.

Hakuna kitu kinachoweza kuwepo kutokana na kitu kisichokwepo. Kitu chochote halisi kilichoumbwa kinahitaji chanzo cha kuumbwa kwake. Kwa maneno mengine, hakuna kitu kinachoweza kuumbwa isipokuwa kitu/vitu vinginie vimekiumba.

Hakuna kitu kinachoweza kujiumba chenyewe. Hakuna kitu kinachoweza kujiumba chenyewe. Ingawa vitu halisi vinaweza kujibadilisha wakati mwingine, au kujiharibu vyenyewe, hakuna kitu kinachoweza kuwa chanzo cha kuumbwa kwake.

Chanzo cha kwanza. Ingawa vitu halisi vilivyoumbwa vinaweza kuumba vitu vingine halisi vilivyombwa, mwisho wa siku patahitajika kuwa na chanzo cha kwanza. Kwa maneno mengine, kwenye mlolongo wa vyanzo, chanzo walau kimoja kinatakiwa kuvitangulia vyanzo vingine vyote.

Kisichoumbwa. Kwa vile chanzo walau kimoja hakitakiwa kuwa na chanzo kilichokitangulia, na kila kiumbe kinahitaji chanzo, kuna kitu halisi walau kimoja ambacho hakijaumbwa na kimekuwepo toka milele iliyopita, kwa sababu kuna kitu halisi walau kimoja ambacho hakijaumbwa.

Mhutasari: Kila kitu halisi ambacho kinaishi ama kina wakati au kipindi fulana=i ambacho kiliwahikuishi, vinginevyo hakijawahi kuishi. Kama kimewahi kuishi, basi kuna kitu halisi ambacho ni chanzo cha kuwepo kwake.

Mipaka: Hoja hii haithibitishi kwamba chanzo cha kwanza ni kitu chenye uhai, au kwamba kuna chanzo kimoja tu ambacho hakijaumbwa, au kwamba vyanzo vyovyote ambavyo havijaumbwa bado vinaishi. Kitu ambacho hoja hii inasema ni kwamba kuna walau kitu kimoja halisi (nafsi iliyo hai au kitu kisichokuwa nafsi) ambacho kimekuwepo milele bila kuumbwa.
Moja ya waandishi wa kwanza aliyeiona hoja ya muundo na umbo la ulimwengu na kusema kuwa Mungu ni chanzo cha kwanza alikuwa Philo, Myahudi aliyeishi Alexandria, Misri, toka mwaka 15/20 KK hadi mwaka 50BK. R. C. Sproul na Norm Geisler wameandika kazi nyingi na nzuri kuhusiana na hoja ya muundo na umbo la ulimwengu.

Je, kuto kuwepo kunaweza kutengeneza au umba uwepo?
If nothing ever existed, nothing would exist now. Nothingness has no capacities or being.

Shalom,

Max Shimba Mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu. Tito 2:13.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW