Je, Yesu ni Mwana wa Mungu?
Je, Isa bin Mariam ni Mwana wa Mungu?
Biblia inasema kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu. Katika hii mada, tuanze kwa kuangali, Je, Biblia inasema nini kuhusu Yesu? Kumbuka kuwa, Biblia ndio ilikuja kwanza kabla ya Quran. Ushahid unonyesha kuwa Biblia ilikuwepo miaka 632 kabla ya Quran kuandikwa na marafiki zake Muhammad.
YESU NI MWANA WA MUNGU
Tunaona hapa Biblia inatuambia YESU KRISTO ni Mwana wa Mungu (YOHANA 20:30-31) hapa Yesu mwenyewe anasema yeye ni Mwana wa Mungu ( MATHAYO 26:59-64; 16:13-17 ) , Neno Mwana linamzungumzia Yesu Mwana siyo kuwa Mungu anazaa la hasha
Yesu anaitwa mwana wa Mungu kwa sababu alizaliwa kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Hata sisi tumezaliwa kwa mara ya pili kwa Roho tunapo mwamini Yesu Kristo hivyo tunahesabika kuwa ni wana wa Mungu.(WAFILIPI 2:14-15,YOHANA 1:12). Kwahiyo Yesu anapoitwa Mwana wa Mungu maana yake ni chapa ya Mungu (HUIOS) WAEBRANIA 1:1-3. Ndiyo maana hapa Yesu anawaambia wanafunzi wake, mumeniona mimi ; mumemuona Mungu, maana yake ndiyo hiyo (HUIOS) yaani chapa ya Mungu (YOHANA 14:7-9)
Tunaona hapa Yesu alisema Yeye ni Mwana wa Mungu (YOHANA 9:35-37)
Shetani naye anajua kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu (MARKO 3:11,LUKA 4:41).
Malaika nao wanasema kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu (LUKA 1:30-35)
Mungu mwenyewe anasema kuwa Yesu ni Mwanangu mpendwa (MATHAYO 3:17,MATHAYO 17:5 )
ISA WA QURAN SIO MWANA WA MUNGU
Kama kuna jambo ambalo Allah Mungu anayeabudiwa na waislamu analikataa sana kupitia Qurani basi jambo hilo si lingine bali ni uwana wa Mungu. Allah anasema hivi.
Quani 6:101 Suratul Al-An-am [Wanyama]
Yeye ndiye Mwumba wa mbingu na ardhi. inamkinikanaje awe na mwana, hali hana mke. Naye ndiye aliye umba kila kitu (sio baadhi yake kavizaa). Naye ni mjuzi wa kila kitu.
Qurani 9:30 Suratul At-Tawba [Kutubu]
Na mayahudi wanasema “uzeri ni mwana wa Mwenyezi Mungu;”na “Wakristo wanasema Masihi ni Mwana wa Mwenyezi Mungu” Haya ndiyo wasemayo kwa vinywa vyao (pasina na kuyapima). Wanayaiga maneno ya wale waliokufuru kabla yao, Mwenyenzi Mungu uwaangamize. Wanageuzwa namna gani hawa!
Allah anasema katika aya hizo hapo juu kuwa, yeye hana Mwana na kuwa Wakristo na Wayahudi wanamsingizia Allah kuwa na Mwana. Allah anasema kuwa, yeye hana Mwana kwasababu hana MKE. Ikiimanisha kuwa, Allah hana uwezo wa kuwa na Mwana bila ya kufanya tendo la ndo na Mwnamke. Huu ni ushahid tosha kuwa, Allah sio mjuzi wa yote, maana hawezi kuwa na mwana bila ya mke.
Hebu tuangalie aya zingine za Biblia zinasema nini kuhusu Yesu.
1. Mathayo 17:5 ….Huyu ni mwanangu mpendwa wangu…
2. Malaika wa Mungu alisema hivi.
Luka 1:30-31,35
Malaika akamwambia usiogope Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.Tazama utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu Mwana wa Mungu.
Hivyo Isa siyo Mwana Mungu lakini Yesu ni mwana wa Mungu. Kwa hivyo Yesu siyo Isa.
Leo tumejifuinza kwa mara nyingine tena kuwa Isa wa Quran sio Yesu wa Biblia kwa kuwa Isa wa Quran yeye sio Mwana wa Mungu.
Katika huduma yake,
Max Shimba
Max Shimba Ministries
Copyright © Max Shimba Ministries 2015
Saturday, January 23, 2016
Wednesday, January 20, 2016
YESU NI MUNGU KUTOKANA NA QURAN (SEHEMU YA KWANZA)

Waumini wa dini ya Kiislam katika Mihadhara mbalimbali ya kidini kupitia wahadhiri wao wa Dini wamekuwa wakipinga kuwa Yesu Kristo si Mungu kwa madai kuwa, Mungu hawezi kuzaliwa.
Ndugu msomaji, nakusihi ufuatilie somo hili kwa makini ili ujue ukweli kuhusu Umungu wa Yesu Kristo katika Koran:
Je Yesu anazo sifa za kipekee za Mungu kutokana na Quran?
Hebu tuanze utafiti wetu kwa kusoma Quran na tujionee wenyewe kama kweli Yesu ni Mungu au la.
MUNGU NI MFALME
Adhama ya Kwanza kutokana na Quran: Mungu ni Mfalme:
Koran inasema kuwa, sifa Moja ya Mungu ni “Mfalme”. Je, Yesu anayo hii sifa ya “Mfalme”? Haya tusome Quran kwanza.
Quran 59: 23
Adhama ya Kwanza kutokana na Quran: Mungu ni Mfalme:
Koran inasema kuwa, sifa Moja ya Mungu ni “Mfalme”. Je, Yesu anayo hii sifa ya “Mfalme”? Haya tusome Quran kwanza.
Quran 59: 23
Yeye ndiye Mwenyezi Mungu ambaye hapana Mungu isipo kuwa Yeye tu. Mfalme, Mtakatifu, Mwenye salama, Mtoaji wa amani, Mwenye kuyaendesha Mwenyewe mambo yake, Mwenye nguvu, Anaye fanya analo litaka, Mkubwa, Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo mshirikisha nayo.
Sasa tuangalie kama kweli Yesu anayo hii sifa ya Mfalme ambayo ni adhama ya Mungu pekee kutokana na Koran.
Biblia takatifi inasema yafuatayo kuhusu Yesu Kristo:
Ufunuo 17:14
Ufunuo 17:14
Hawa watafanya vita na Mwana Kondoo na Mwana Kondoo atawashinda, kwamaana yeye ni Bwana wa Bwana na Mfalme wa Wafalme.
Katika aya hii tunasoma kuwa Yesu anaitwa “Mfalme wa Wafalme” ambayo ni adhama ya Mwenyezi Mungu kama ilivyo shaidiwa na Koran Surah ya 59 na aya 23. Hivyo basi , Allah na Koran wamekiri kuwa Yesu ni Mungu kwasababu Biblia imetuthibitishia kuwa Yesu ni Mfalme wa Wafalme katika Ufunuo 17 na aya 14.
Tuendelee na ushaidi mwingine kutoka Koran ambao unatuhakikishia kuwa Yesu ni Mungu.
MUNGU NI MTAKATIFU
Adhama ya Pili kutokana na Quran: Mungu ni Mtakatifu:
Adhama ya Pili kutokana na Quran: Mungu ni Mtakatifu:
Je, Yesu anayo hii sifa ya “Mtakatifu”? Tusome Quran kwanza:
Quran 59: 23 Yeye ndiye Mwenyezi Mungu ambaye hapana Mungu isipo kuwa Yeye tu. Mfalme, Mtakatifu, Mwenye salama, Mtoaji wa amani, Mwenye kuyaendesha Mwenyewe mambo yake, Mwenye nguvu, Anaye fanya analo litaka, Mkubwa, Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo mshirikisha nayo.
Katika Quran tumesoma kuwa, moja ya sifa za Mungu ni “Mtakatifu”, Je sifa hii ya utakatifu Yesu anayo?
Nenda kwenye hihiyo Kuran 19:19 Malaika akasema hakika mimi ni mjumbe ili nikupe Mwana Mtakatifu -Isa Bin Maryam.
Koran hiyo hiyo inatuhakikishia na kutujibu kuwa Yesu ambaye anajulikana kwa jina la Isa Bin Maryam katika Quran ni Mwana Mtakatifu. Hivyobasi, hii adhama ya Utakatifu ambayo ni ya Mungu pekee, tunasoma katika Quran iliyoteremshwa an Allah kuwa Yesu ameinyakua. Yesu anaitwa Mwana Mtakatifu.
BWANA NI MWENYEZI MUNGU
Adhama ya Tatu kutokana na Quran: Bwana ni Mwenyezi Mungu
Hebu tufungue Quran na tusome kuhusu Bwana:
Adhama ya Tatu kutokana na Quran: Bwana ni Mwenyezi Mungu
Hebu tufungue Quran na tusome kuhusu Bwana:
Quran 3:39 Alipo kuwa kasimama chumbani akisali, Malaika kamnadia: Hakika Mwenyezi Mungu anakubashiria Yahya, ataye kuwa mwenye kusadikisha neno litokalo kwa Mwenyezi Mungu, na ni Bwana na mt'awa na Nabii kwa watu wema naye ni Nabii Isa.
Quran 39: 29
Mwenyezi Mungu amepiga mfano wa mtu mwenye mabwana washirika wanao gombana, na wa mtu mwengine aliye khusika na Bwana Mmoja tu. Je! Wako sawa katika hali zao?
Alhamdulillahi, Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu! Lakini wengi wao hawajui.
Quran 39:29 inasema kuwa Mwenyezi Mungu ni Bwana na hiyo ni sifa njema kwa Mwenyezi Mungu. Zaidi ya hapo, Koran hiyo hiyo (Quran 3:39) inasema kuwa Isa Bin Maryam ni Neno litokalo kwa Mwenyezi Mungu na ni Bwana. Koran imejibu kuwa, sifa ya Bwana ambayo ni ya Mungu pekee ni ya Yesu. Sasa tusome na Biblia kwa ushaidi zaidi kuhusu Yesu ni Bwana.
Ufunuo 17:14
Hawa watafanya vita na Mwana Kondoo na Mwana Kondoo atawashinda, kwamaana yeye ni Bwana wa MaBwana na Mfalme wa Wafalme.
Katika Ufunuo tunasoma kuwa Mwana Kondoo ambaye ni Yesu Kristo anaitwa Bwana wa Mabwana. Hivyobasi, hii adhama ya “Bwana” ambayo ni ya Mungu pekee tunasoma katika Quran iliyoteremshwa an Allah kuwa Yesu ni Bwana na ameinyakua, vilevile, katika Biblia Takatifu tumesoma kuwa Yesu anaitwa Bwana, ambayo ni Sifa ya Mungu Pekee kutokana na Quran.
Leo nimejibu hoja ya Waislam kuwa, Je, Yesu ni Mungu? Koran pamoja na Allah wanasema kuwa Yesu ni Mungu kwa kuwa Yesu anazo adhama zote na/au sifa zote za Mungu.
Katika huduma yake,
Max Shimba
Copyright © Max Shimba Ministries 2013
Saturday, January 16, 2016
ALLAH ATEREMSHA AYA NA KUKIRI KUWA YEYE SIO AKBAR

1. ALLAH AOMBA MSAADA KWA VIUMBE DHAIF
2. KUMBE ALLAH SIO AKBAR
2. KUMBE ALLAH SIO AKBAR
Sura Al-Ankabut 29:6
Quran inasema:
Quran inasema:
Allah does not need his creatures’ help.
Yaani,
Allah hahitaji kusaidiwa na viumbe wake. (bila shaka ni katika kutekeleza makusudi na mipango yake).
LAKINI QURAN HIYO HIYO INAWAAMBIA WAISLAMU:
Sura Muhammad 47:7
If you help Allah, He will help you and make you strong.
Yaani,
Kama mkimsaidia Allah, yeye naye atawasaidia na kuwafanya kuwa imara.
Maswali:
1. Umesema huhitaji msaada, kisha unasema tena unahitaji msaada! Je, Mungu anaweza kufanya jambo kama hilo?
2. Aya hizi zinafanana au zinapingana?
3. Je, hii si ishara kuwa aya hizi zilisemwa tu ili kukidhi mahitaji ya wakati fulani, lakini msemaji alipoona anahitaji kuwafanya watu watende kinyume chake, akajikuta amesema tofauti na alivyosema siku za nyuma?
2. Aya hizi zinafanana au zinapingana?
3. Je, hii si ishara kuwa aya hizi zilisemwa tu ili kukidhi mahitaji ya wakati fulani, lakini msemaji alipoona anahitaji kuwafanya watu watende kinyume chake, akajikuta amesema tofauti na alivyosema siku za nyuma?
Na tena quran inasema katika sura Al-Baqara 2:244
Fight for the cause of Allah and bear in mind that He hears all and knows all.
Yaani:
Fanyeni vita kwa ajili ya Allah na mkumbuke kwamba anaona yote na anajua yote.
Maswali:
1. Kama kweli Allah hahitaji msaada wa viumbe wake; na kama kweli aliumba ulimwengu wote kwa NENO TU, iweje NENO hilo hilo lisiweze kuwabadilisha wanadamu hadi alazimike kuliingiza ndani yao kwa nguvu, kwa vitisho na kwa ukali namna hiyo?
(Ukristo unashinda na kufanikiwa kwa NENO tu. Maana sisi tumeumbwa kwa mfano wa Mungu wetu. Yeye aliumba kwa Neno; na sisi watoto wake, tunaumba kwa Neno hilo hilo. Tunahubiri tu na watu wanaokolewa, wanaponywa, wanalindwa na kusimama na Mungu wa kweli. Huoni kwamba hii hasa ndiyo maana ya nguvu ya Mungu? Hatuhitaji kuchinja au kupiga watu ili wampende Mungu!! Unawezaje, hata tu wewe mwenyewe, kumfanya mwanao au mkeo akupende kwa njia ya vipigo na kulazimisha? yaani, ukitaka mwanao au mkeo akupende utamshikia rungu au panga au bunduki? Je, hiyo si ishara kwamba wewe huna nguvu ndiyo maana unalazimisha? je, huko si kujikanganya maana umetuambia kuwa wewe ni Mungu unayeweza yote?)
2. Je, Allah anapotaka wanadamu wanaomwamini wafanye vita ili kuwalazimisha wasioamini wamwamini, huko si kutaka msaada kwa viumbe wake?
ALLAH ATEREMSHA AYA NA KUSEMA KUWA AKHERA ITAJAA WATU WENYE CHUKI

Sura Al-Nahl 16:28
The angels will say to those whom they cause to die in purity, ‘Peace be on you.’ Come into paradise for what you did.
Yaani:
[Kuhusu wale wanaoingia mbinguni] – Malaika watasema kwa wale ambao watawafanya wafe katika usafi (utakatifu), ‘Amani na iwe juu yenu. Ingieni paradiso kutokana na matendo yenu.’
LAKINI, QURAN HIYO HIYO INASEMA:
Sura Al-Hijr 15:45-47
Indeed, the righteous will be within gardens and springs, [Having been told], "Enter it in peace, safe [and secure]." And We will remove whatever is in their breasts of resentment, [so they will be] brothers, on thrones facing each other.
Yaani:
Surat Al Hijir
45. Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem. 46. (Wataambiwa:) Ingieni kwa salama na amani. 47. Na tutaondoa chuki iliyo kuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya enzi wameelekeana.
45. Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem. 46. (Wataambiwa:) Ingieni kwa salama na amani. 47. Na tutaondoa chuki iliyo kuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya enzi wameelekeana.
Maswali:
1. Katika 16:28, inaonekana kwamba watakaiongia peponi ni watu walio safi kwa sababu malaika wamesababisha watu hao wafe wakiwa safi. Lakini 15:45-47 inaonyesha kuwa wataingia peponi wakiwa na chuki mioyoni mwao. Je, chuki ni sehemu ya usafi?
2. Je, aya hizi zimetoka kwa mtoaji yule yule?
3. Kama chuki ni mbaya kiasi cha kuhitajika kuondolewa mioyoni mwa Waislamu wanaoingia peponi, iweje wakiwa duniani wanaagizwa kuwachukia wale wasio Waislamu (kama tulivyoona kwenye 4:101)?
2. Je, aya hizi zimetoka kwa mtoaji yule yule?
3. Kama chuki ni mbaya kiasi cha kuhitajika kuondolewa mioyoni mwa Waislamu wanaoingia peponi, iweje wakiwa duniani wanaagizwa kuwachukia wale wasio Waislamu (kama tulivyoona kwenye 4:101)?
ALLAH ATEREMSHA AYA KWA MUHAMMAD NA KUSEMA UISLAM NI DINI YA VITA

1. KUMBE ALLAH NI KIGEUGEU
2. KUMBE MUHAMMAD NI KIGEUGEU
2. KUMBE MUHAMMAD NI KIGEUGEU
Sura Al-Kafirun 109:1-6
Say, "O unbelievers, I do not worship what you worship, nor do you worship what I worship. I shall never worship what you worship, nor will you worship what I worship. You have your own religion and I have mine."
Yaani,
Enyi msioamini, mimi siabudu mnachoabudu, wala ninyi hamuabudu ninachoabudu. Mimi kamwe sitaabudu kile mnachokiabudu, wala ninyi kuabudu kile ninachokiabudu. Ninyi mnayo dini yenu, nami nina yangu.
Pia, quran inasema katika sura Al-Baqara 2:256
There shall be no compulsion in religion.
Yaani:
Hakutakuwapo na kulazimishana katika dini.
LAKINI ALLAH HUYO HUYO ANASEMA:
Sura Al-Anfal 8:39
Make war on them until persecution is no more and Allah’s religion reigns supreme.
Yaani:
Fanyeni vita juu yao hadi kusiwepo na mateso tena na hadi pale dini ya Allah itakapokuwa imetawala.
Maswali:
1. Aliyemwambia Muhammad asiwalazimishe wasioamini kuamini Uislamu ndiye huyo huyo aliyemwambia afanye vita?
2. Aliyesema kuwa “ninyi msioamini hamtaabudu ninachoabudu” ndiye huyo huyo anayesema ni vita tu hadi dini ya Allah itawale?
3. Na je, aliyesema kuwa hakuna kulazimishana katika masuala ya dini ndiye huyo huyo anayesema watu wake wapigane vita?
4. Huku si kujipinga mwenyewe?
2. Aliyesema kuwa “ninyi msioamini hamtaabudu ninachoabudu” ndiye huyo huyo anayesema ni vita tu hadi dini ya Allah itawale?
3. Na je, aliyesema kuwa hakuna kulazimishana katika masuala ya dini ndiye huyo huyo anayesema watu wake wapigane vita?
4. Huku si kujipinga mwenyewe?
ALLAH, MUHAMMAD NA UISLAM WASEMA NI MARUFUKU KWA MUISLAM KUWA RAFIKI NA MKRISTO
Ndugu msomaji,
Leo ningependa tujifunze kuhusu chuki iliyo ndani ya Allah na dini yake ya Uislam. Wengi wenu huwa mnadai na au fikiria kuwa Mungu wa Biblia aliye jaa upendo ni huyo huyo wa kwenye Quran ya Jibril. La hasha.
Allah ambaye ndie munguwa Waislam yeye amejaa chuki na anawataka na kuwaamrisha Waislam wote kufanye chuki iliyo ndani ya Quran.
Hebu anza moja kwa moja kusoma chuki za Allah:
ALLAH ANAWAAMBIA WAISLAM WOTE KUWA: NI MARUFUKU KUWA MARAFIKI NA WAKRISTO:
Surat Al Maida 51. Enyi mlio amini! Msiwafanye Mayahudi na Wakristo kuwa ni marafiki. Wao ni marafiki wao kwa wao. Na miongoni mwenu mwenye kufanya urafiki nao, basi huyo ni katika wao. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu wenye kudhulumu. http://www.quranitukufu.net/005.html
SASA, kama Allah ni Yehovah wa Biblia, mbona hatusomi Mungu wa Biblia akisema muwachukie watu ambao sio wa imani yenu?
SOMA Luka 6:35 Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
35 Bali, wapendeni adui zenu, watendeeni mema. Wakopesheni bila kutegemea kurudishiwa mlichokopesha. Ndipo mtapata zawadi kubwa nanyi mtakuwa wana wa Mungu Aliye Juu. Yeye ni mwema kwa watu wasio na shukrani na watu waovu.
MUNGU WA BIBLIA ANSEMA Wapendini adui zenu, ni tofauti kabisa na Allah anaye sema WACHUKIENI WAKRISTO NA WAYAHUDI. Allah wa Quran sio Mungu wa Biblia.
ALLAH ANASEMA KUWA, WAISLAM HAWARUHUSIWI KUWAPENDA WAKRISTO HATA KAMA NI BABA ZAO AU MAMA ZAO AU NDUGU ZAO:
Suratul Al Mujaadalah 22. Huwakuti watu wanao muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho kuwa wanawapenda wanao mpinga Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hata wakiwa ni baba zao, au watoto wao, au ndugu zao, au jamaa zao. Hao ameandika katika nyoyo zao Imani, na amewapa nguvu kwa Roho itokayo kwake. Na atawaingiza katika Mabustani yapitayo mito kati yake. Humo watakaa daima. Mwenyezi Mungu awe radhi nao, na wao wawe radhi naye. Hao ndio Hizbullahi, Kundi la Mwenyezi Mungu. Hakika Kundi la Mwenyezi Mungu ndilo lenye kufanikiwa. http://www.quranitukufu.net/058.html
HIVI, kweli bado unaamini kuwa Allah ni? Mbona sifa zake zote ni za SHETANI wa aliye semwa kwenye Biblia?
ALLAH ATEREMSHA AYA NA KUSEMA WAISLAM WASIWAFANYE WAKRISTO NA WAYAHUDI KUWA MARAFIKI ZAO.
Surat An Nisaai 144. Enyi mlio amini! Msiwafanye Wakristo na Mayahudi kuwa ndio marafiki badala ya Waumini. Je, mnataka Mwenyezi Mungu awe na hoja iliyo wazi juu yenu? http://www.quranitukufu.net/004.html
Allah anaendelea kuonyesha sifa za Shetani. Leo anasema na kuwaamrisha Waislam kuwa, WASIWE NA URAFIKI NA WAKRISTO. Hivi Mungu gani huyu anaye penda kuchonganisha watu? Hii tabia ya chuki ni ya nani kama si SHETANI?
Hebu tumsome YESU WA KWENYE BIBLIA ANASEMA NINI?
‘Basi Yesu aliwaambia tena, Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi mlango wa kondoo. Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho. MWIVI HAJI ILA AIBE NA KUCHINJA NA KUHARIBU; MIMI NALIKUJA ILI WAWE NA UZIMA, KISHA WAWE NAO TELE. Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo. Mtu wa mshahara, wala si mchungaji, ambaye kondoo si mali yake, humwona mbwa-mwitu anakuja, akawaacha kondoo na kukimbia; na mbwa-mwitu huwakamata na kuwatawanya. Yule hukimbia kwa kuwa ni mtu wa mshahara; wala mambo ya kondoo si kitu kwake. Mimi ndimi mchungaji mwema; nao walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi; kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo. #YOHANA 10:7-15
ALLAH ATEREMSHA AYA NA KUSEMA WAISLAM NI MARUFUKU KUWA NA UMOJA NA WASIO WAISLAM
Surat Al Imran 118. Enyi mlio amini! Msiwafanye wasiri wenu watu wasio kuwa katika nyinyi. Hawataacha kukufanyieni ubaya. Wanayapenda yanayo kudhuruni. Imekwisha fichuka chuki yao katika midomo yao. Na yanayo ficha vifua vyao ni makubwa zaidi. Tumekwisha kubainishieni Ishara ikiwa nyinyi mtayatia akilini.
Allah anaendelea kupanda chuki kubwa kubwa kwa Waislam, sasa anasema kuwa Waislam wasiwe na wasiri na watu ambao sio Waislam, hata kama huyo mtu ni Baba yao, mama yao nk. Hii chuki inapatika kwa SHETANI na sio Mungu wa kwenye Biblia.
ALLAH ATEREMSHA YA NA KUSEMA KUWA WAKRISTO NI MAADUI ZA WAISLAM.
Surat An Nisaai 101. Na mnapo safiri katika nchi si vibaya kwenu kama mkifupisha Sala, iwapo mnachelea wasije wale walio kufuru wakakuleteeni maudhi. Hakika makafiri ni maadui zenu walio wazi wazi.
ALLAH AWAAMRISHA WAISLAM KUWAKATAA WAKRISTO
Surat Al Mumtahinah 4 ...............Tunakukataeni; na umekwisha dhihiri uadui na chuki baina yetu na nyinyi mpaka mtakapo muamini Mwenyezi Mungu peke yake.
ALLAH AWAAMRISHA WAISLAM KUPIGANA NA KUWAUWA WAKRISTO.
Surat Tawba 123. Enyi mlio amini! Piganeni na wale makafiri walio karibu yenu, na wakute ugumu kwenu. Na jueni ya kwamba Mwenyezi Mungu yu pamoja na wacha- Mngu
Mwana wa Mungu siku zote Shetani kazi yake ni kuiba, kuua na kuharibu. Ndiyo kazi yake. Hajawahi kubadilika. Toka afukuzwe mbinguni hiyo ndo imekuwa kazi yake hapa duniani. Na Bwana Yesu amelisema hilo bila kumung’unya maneno. Bwana Yesu dhamira yake ni kutupa uzima tele.
Adui siku zote amekuwa ni muuaji tu. Kila sehemu anakopita yeye ni mharibifu. Huwa inafika mahala najiitisha kikao na kujiuliza sisi wanadamu tuna matatizo gani. Kwa nini kufanya urafiki na Shetani na kukubali kuwa mtumwa wake? Unapokubali kuwa mtenda dhambi maanake umekubali kufanya urafiki na Shetani maishani mwako.
Mwana wa Mungu Bwana Yesu anasema yeye amekuja ili wanadamu WAWE NA UZIMA, KISHA WAWE NAO TELE.
Ikiwa adui amepora chochote ndani yako, ameua chochote ndani yako, amefanya uharibifu wowote ndani yako, ndani ya ndoa yako, au ndani ya familia yako, ndani ya kazi yako, ndani ya biashara yako, katika ukoo wako, kwa watoto wako, kwa wazazi wako, basi nakutangazia BWANA YESU ALIKUJA ILI UWE NA UZIMA, KISHA UWE NAO TELE. Ni ombi langu Bwana akupe uzima tele katika kila eneo adui alifanya uharibifu. Kama ilikuwa kwenye ndoa, kwenye biashara, kwenye kazi, kwenye kuutafuta uso wa Mungu. katika kupata watoto, kupata mume, kupata mke n.k Bwana akupe hitaji lako.
Shetani yuko chini ya miguu yako mpendwa, simama kurudisha chochote adui alikuwa amefanya uharibifu dhidi yako na usikubali kushindwa na Shetani. Yesu aliyemo ndani yako ni mkuu kuliko Shetani. Anataka akupe uzima tena uzima tele.
Barikiwa sana.
Yamkini unataka kuokoka? Basi wasiliana nasi tukusaidie
kuchukua uamuzi mwema wenye busara maishani mwako.
Yesu anakupenda.
Max Shimba Ministries
Thursday, January 14, 2016
MAJINI NI MAISLAM

MAJINI KATIKA DINI YA KIISLAM ( Q 72:1-14 )
1. QURAN INASEMA KUWA MAJINI YANAZALIANA NA KUFA KAMA BINADAMU
2. ALLAH AYARUHUSU MAJINI KUZAA NA BINADAMU
3. QURAN INAKIRI KUWA MAJINI NI MAISLAM NA YALISILIMU PALE QURAN ILIPO TEREMSHWA KWA MUHAMMAD.
4. MAJINI YANAMWABUDU ALLAH
5. KILA MUISLAM AMEPAGAWA NA MAJINI KATIKA MWILI WAKE
Leo ningependa tujifunze kidogo kuhusu Majini au Mashetani katika Uislam.
JINI NI NINI?
Katika lugha ya kiarabu, neno Jini linamaanisha kitu kilichofichwa au kisichoonekana QURAN 1:71 Neno hili hutumiwa na Waarabu kwa ajili ya kutaja jina fulani. Kwa Waarabu, Jini anayevaa sura ya kike humwita Jinivya, hivyo majini Ghul/Ghilan, nao hujifunua kwa sura ya kike.
Katika imani ya Kiislamu, wao huamni kwamba Majini hutofautiana na Mashetani. Majini waliosilimu wao huitwa majini mazuri na hawa wakiwa katika hali kujionyesha kwa wanadamu, hao huitwa AJINU na wale walioacha kusilimu mwaka 610 AD (Baada ya Kristo) katika safari ya mtume Muhamad alipotoka Taif , wao wanaitwa Mashetani . Hivyo, wao wanapokuwa katika hali ya kutoonekana huitwa ALBAHATWA lakini pia Majini wote wanapokuwa katika hali ya kutoonekana waweza kuitwa ALBAHATWA, yaani PEPO.
QURAN INASEMA KUWA MAJINI YANAZALIANA NA KUFA KAMA BINADAMU
Muislamu huamini kwamba kuna majini ya kike na kiume. Lakini pia , huamini kuwa Majini huoana na kuzaliana QURAN 55:56 na kuwa Majini huzaa sana kuliko binadamu na kwamba, Jini mmoja anaweza kuzaa watoto 300, na kuwa Jini huzaa watoto 3 hadi 4 kwa mkupuo. Somo QURAN 55:26-28 na kuwa Majini wanaweza kuishi miaka 400-1,000 kisha wanaweza kufa. Tofauti yao na binadamu ni kwamba wao wanaishi miaka mingi kuliko binadamu. Lakini pia, huamini kuwa wapo Majini wanaokula, wanaomeza, wanaokunywa, ila tofauti yao na wanadamu ni kwamba wao hula kwa kutumia mkono wa kushoto.
ALLAH AYARUHUSU MAJINI YANAZAA NA BINADAMU
Pia hiamini kuwa Majini wana uwezo wa kuzaa na Wanadamu. Soma QURAN 17:64. Waislamu huamini kwamba mtu anauwezo wa kuoa au kuolewa na Jini bila kujua, na mwanadamu anauwezo wa kumuua Jini. Soma QURAN 57:14-15
SURATULJINN
Ndani ya QURAN pia imo sura inayoitwa Suratuljinn (QURAN 72). Sura hiyo huitwa hivyo kwa sababu ni sura ya Majini (Mapepo).
Kwa nini wanatajwa Majini katika imani ya Kiislamu?
QURAN INAKIRI KUWA MAJINI NI MAISLAM NA YALISILIMU PALE QURAN ILIPO TEREMSHWA KWA MUHAMMAD.
Majini wanatajwa sana katika dini ya Kiislamu kwa kuwa ni waislam kwa kusilimu, kwa kuiamini Quran tukufu aliyopewa mtume Muhamad.
Majini walisilimu na kuwa Waislamu mwaka 610 AD(Baada ya Yesu) SOMA 72:1-14 QURAN. Hivyo basi, unapotumia neon jinni maana yake unatumia lugha ya Kiarabu ukimaanisha Pepo mchafu. Ni kama Spoon/kijiko, vyote ni kitu kimoja. Ndani ya Quran, neon “PEPO” limetumika kama Paradiso, mbinguni. Lakini pia, tunapata neon jingine liitwalo AKHERA ila neno hilo halimaanishi PARADISO, bali kwa lugha ya Kiarabu neno hili “AKHERA” lina maana ya KUZIMU.
Lakini pia ukiangalia ndani ya SURALJINN ( QURAN 72:1-2, 8-9, 12 ) Mapepo hawa wanajieleza waziwazi kabisa kuwa mwanzo waliishi Mbinguni, walipogeuka kwa kuasi, walitegwa na Mungu. Linganisha na maandiko haya katika Biblia ( UFUNUO WA YOHANA 12:7-9; YUDA 1:6-8; UFUNUO 20:10; UFUNUO 21:8 ). Kwa mujibu wa dini ya Kiislamu, hawa majini ( Mapepo ) waliotegwa na Mungu Mbinguni wakiwa Malaika huko na kutupwa Duniani baada ya kuasi huko, sasa, wakati wa mtume Muhamad katika safari yake ya kurudi Taif mwaka 620 AD (baada ya Yesu) wapo walioamini na kuona kuwa Quran ni ya ajabu ya kuwatangazia neema ya kuabudu. Katika vol 8-9, husema , wanapojaribu kwenda Mbinguni ( walikotoka zamani ), hukuta ile Mbingu imezungushiwa vimondo vya moto. Hivyo, hudai kuwa mbingu yao iko Akhera, yaani Kuzimu, maana Mbingu ya juu ina moto na hawana uwezo wa kwenda huko. SOMA (QURAN 72:9), Mbingu ina utisho wa moto ila Akhera ( kuzimu ) hakuna shida kwao.
MAJINI YANAMWABUDU ALLAH
Hivyo basi, kulingana na jinsi Allah asemavyo ndani ya Quran kuwa nimeumba binadamu na majini ili muniabudu ( QURAN 57:58 ; 51:56) na kuwa , mbinguni mwao Majini wanaabudu (Majini waliosilimu mwaka 620 AD) ,SOMA QURAN 72:14, ambao ni wema wanaosafiri na kurithi uzima wa milele upatikanao Akhera ( Kuzimu ). Lengo kubwa la Shetani na Majini ni kufanya urafiki na wanadamu wengi ili kwa wingi huo apate watu wengi wa kwenda nao JEHANAMU ( QURAN 6:128 ). Jambo la muhimu kujua hapa ni kwamba moto wa milele hakuwekewa Mwanadamu bali ni Shetani na malaika zake wote ( Majini au mapepo ). Hawa, hawana nafasi tena ya kuungama au kutubu.
Yesu Kristo anayetambuliwa na Waislam kama Mtume tu, hakuwa na urafiki wowote na Shetani wala Mapepo ( Majini ). Aliyaamuru Majini kutoka ndani ya watu waliokuwa wakiteswa nayo ( MATHAYO 8:29: MARKO 5 N,K )
Wakati Yesu anaondoka hapa duniani, alichukuliwa na wingu na kupaa kuelekea juu. Mbinguni ni juu kama Quran inavyothibitisha. Yesu aliweza kupaa na kuingia Mbinguni lakini Majini ( Mapepo ) walioslimu wakijaribu tu, wanakutana na moto mkali. Tumeona kuwa Majini ambao ni Waislamu kwa kusilimu, wanaishi AKHERA yaani Kuzimu. Je, Waislamu wengine unadhani wataishia wapi milele? Katika imani ya Kiislam huamini kuwa, Muislam akifa anakuwa na Majini wawili wa Kumlinda humo Kaburini.
KILA MUISLAM ANA JINI KATIKA MWILI WAKE
Majini wamepewa ruhusa ya kukaa katika mwili wa Muislam yeyote, hivyo kila Muislam ana Jini kuanzia moja na kuendelea. Vile vile Majini wameruhusiwa kukaa katika nyumba za Waislam. Katika nyumba yoyote ya Muumini wa dini hiyo, kuna Jini au Majini wanaokaa humo. Ni ukweli usiopingika kuwa bila Majini hakuna Uislamu kama vile pasipo Roho Mtakatifu hakuna Ukristo. Majini ndiyo yaliyomchukua mtume Muhamad kwa muda wa siku 40 akiwa Mabondeni walikompeleka na kuanza kumuagiza kuhusiana na kuanzisha imani hiyo ya Kiislamu.
USHAURI WANGU KWA WA WAKRISTO:
Ushauri wangu wa bure kwa Mkristo ni huu, USIMUACHE KAMWE KRISTO NA KUINGIA KATIKA IMANI ZA MASHETANI (1TIMOTHEO 4:1-2 ).
Majini au Mashetani ni kitui kimoja na wala hakuna tofauti yao. Wote hao Mashetani/Majini yalimpinga Mungu na kutupwa duniani. Biblia inasema kuwa Hakuna Msamaha kwa Majini maana wao walisha hukumiwa na wanacho subiri ni kutupwa Jehannam.
Shetani bado ni “mfalme wa nguvu za anga” (Waefeso 2:2). Hii inamaanisha kwamba Shetani na Malaika wengine walioasi wanaweza kushawishi mia zetu na mawazo yetu kupitia miziki, runinga, mijadala, nk. Tumeambiwa kujihadhari katika mawazo na nia zetu (2Wakorintho 10:3-5). 2Wakorintho 4:4 inatuambia kuwa mungu wa dunia hii amepofusha mawazo ya watu ili wasiamini.
Shetani ndiye yuko nyuma ya dini zote za uongo na dini za dunia. Shetani atafanya na kila kitu katika uwezo wake ili ampinge Mungu na wale wote wanaomfuata. Ingawa hatima ya Shetani imewekwa muhuri kuwa tanuru la moto milele (Ufunuo Wa Yohana 20:10).
Mungu awabariki sana,
Katika Huduma Yake,
Max Shimba Ministries Org.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2015. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
Wednesday, January 13, 2016
WAISLAM WANAULIZA: JE, ALIYE TAJWA KWENYE KUMBUKUMBU YA TORATI NI MUHAMMAD AU YESU?
Swali: Katika Kumbukumbu 18:17-18; 33:1-2, na 34:10-11, ni Muhammad aliyetabiriwa hapa, kama baadhi ya Waislam wanavyodai?Jibu: Kumbukumbu 18:15-18 inasema Mungu atamwinua nabii, kuwa watamsikia, kama Musa kutoka miongoni mwao, miongoni mwa ndugu zao.
Je Yesu alikuwa nabii?
Je Wayahudi walio wengi walimsikia Yesu?
Je Yesu alikuwa mmoja wa Wayahudi?
Je Yesu alikuwa Myahudi?
Je Wayahudi walio wengi walimsikia Yesu?
Je Yesu alikuwa mmoja wa Wayahudi?
Je Yesu alikuwa Myahudi?
Waislam wanapaswa kutokuwa na shida kuafiki kuwa mistari hii inamfaa Yesu kuliko Muhammad. Kama angalizo la kihistoria, kabla ya Nicea Archelaus (262-278 B.K.) pia alizungumzia jinsi ambavyo Kumbukumbu 18:15 isivyoweza kuwa inamwongelea mtu mwingine yoyote yule isipokuwa Yesu Kristo kwenye Disputation with Manes sura ya 43 uk.219.Yafuatayo ni maoni zaidi.
a. Kumbukumbu 33:1-2 inasema "Bwana", na Waislam hawamwiti Muhammad Bwana wao. (Waislam wa ‘Alawite na makundi mengine ya Ghulat wanamchukulia Muhammad kuwa Mungu, lakini maoni hayo siyo kawaida kwa Waislam.)
b. Kumbukumbu 34:10 kwamba "Wala hakuinuka tena katika Israeli nabii kama Musa." Wasifu huu uliandikwa, huenda na Yoshua, muda mrefu kabla Yesu hajaja.
c. Kumbukumbu 34:10 inasema "uso kwa uso", na Muhammad hajawahi kusema kuwa alipata maneno yake moja mwa moja kutoka kwa Mungu, bali kupitia malaika (Sura 2:97). Yesu aliwasiliana moja kwa moja na Mungu Baba kwa mujibu wa Yohana 1:18 na vifungu vingine.
d. Mstari unaofuatia, 34:11, unasema kuwa hakuna nabii mwingine yoyote aliyefanya miujiza hiyo mikubwa kama Musa.
Muhammad, kama ilivyoandikwa kwenye Kurani (Sura 17:90-93) hakuwahi kufanya miujiza kama hii, isipokuwa kusema Kurani. (Kurani inapingana na jinsi mapokeo ya baadaye ya Hadithi yanavyosema.)
e. Kwenye Kurani yenyewe, Sura 29:27 inasema unabii umekuja kupitia Isaka na Yakobo. Kwenye tafsiri ya Yusuf Ali ya Kurani, anasema, "Na tumewapa (Abraham) Isaka na Yakobo, na tumeagiza miongoni mwa wazao wake unabii na ufunuo . . ."
Wakati ambapo mabano kwenye jina la Abraham yapo kwenye tafsiri ya Yusuf Ali, neno lote "Abraham" halimo kwenye Kurani ya Kiarabu, na Yusuf Ali aliona haja ya kuongeza neno "Abraham" kwenye maandiko ambayo Waislam wanayaona kuwa ni neno la Mungu.
f. Mwisho, Petro, mtume wa Yesu, alisema andiko hili lilitimia kwa Yesu kwenye Matendo 3:22-26. Mtume Petro alikuwa na nafasi kubwa sana ya kuweza kujua jambo hili.
1. Ama, Yesu alifanya makosa ya kumruhusu mtu mwongo kama Petro kuwapotosha watu, kwa kwa karibu miaka 2,000, ambao wamekuwa wakijaribu kumfuata Mungu, na Mungu hakuinua kidole kuwaambia watu ukweli.
2. Au, Yesu alijua alichokuwa anafanya wakati alipomchagua Petro, na Mungu hakusahihisha kitu ambacho hakikihitaji masahihisho yoyote yale.
3. Vinginevyo, Petro hakusema hivyo, na kitabu cha Matendo ya Mitume kilipotoshwa kabla ya maelezo ya maneno hayo ya kwanza tuliyo nayo toka nje ya Biblia yanayoturejesha kwa Yesu, karibu mwaka 138 B.K.
Viongozi wa awali wa kanisa walisema kuwa mstari huu ulimwongelea Yesu. Baadhi yao ni
Justin Martyr 138-165 B.K.
Irenaeus 182-188 B.K.
Tertullian 220-220 B.K.
Origen 225-254 B.K.
Chrysostom 407 B.K.
Justin Martyr 138-165 B.K.
Irenaeus 182-188 B.K.
Tertullian 220-220 B.K.
Origen 225-254 B.K.
Chrysostom 407 B.K.
Justin Martyr alizaliwa karibu mwaka 114 B.K., ingawa watu wengine hudhani mwaka 110 B.K. Apology yake ya kwanza iliandikwa kati ya mwaka 138 B.K. na mwaka 165 B.K. wakati wa kifo chake. Ni dhahiri kuwa alitakiwa kusoma unabii huu unaomwongelea Yesu kabla ya kuandika.
Muislam anaweza kusema kuwa Justin hakukosea tu bali pia manuscripts zote za Agano Jipya ziliunukuu usemi wa Petro kimakosa.
Pia, tafsiri kwenye lugha nyingine zilifanywa mapema sana; tarehe za hapo juu si za tafsiri za kwanza, bali ni tarehe za manuscripts za zamani zaidi ambazo zipo leo hii.
Hizi zinaaminika kwa sababu zimepita kwenye mtiririko huru ambao watu wanaweza kuutumia kuthibitisha manuscripts za Kiyunani.
Mtiririko wote wa manuscripts hizi, kutoka Afrika kwenda Asia, unaafiki kuwa Petro alisema hivi akimwongelea Yesu.
Tazama When Cultists Ask uk.43-44,45-46 na When Critics Ask uk.125-126, uk.131-132, na uk.133 kwa habari zaidi.Mungu awabariki sana
Max Shimba Ministries Org
KATIKA TAURAT, ZABURI, INJILI HAKUNA NENO ISLAM AU WAISLAM

KATIKA TAURAT YA MUSA, HAKUNA NENO ISLAM AU WAISLAM
KATIKA INJIL YA YESU, HAKUNA NENO ISLAM AU WAISLAM
KATIKA ZABURI YA DAUDI, HAKUNA NENO ISLAM AU WAISLAM.
A. Kwanini Waislam wanadai eti Musa alikuwa Muislam, wakati Taurat iliyo kuwepo Kabla ya Quran haisemi na wala haina neno "ISLAM" au WAISLAM"?
B. Kwanini Waislam wanadai eti Yesu alikuwa Muislam, wakati Injili iliyo kuwepo Kabla ya Quran haisemi na wala haina neno "ISLAM" au WAISLAM"?
C. Kwanini Waislam wanadai eti Daudi alikuwa Muislam, wakati Zaburi iliyo kuwepo Kabla ya Quran haisemi na wala haina neno "ISLAM" au WAISLAM"?
Kama Waislam wanabisha, nionyesheni ipo wapi Taurat aliyo iteremsha Allah kwa Musa tuione? Na iwe na aya inayosema kuwa Musa alikuwa Muislam.
Quran inasema kuwa Allah ameitunza Taurat na Injil katika Surah 15 aya 9. Vile vile tunasoma kuwa Taurat na Injil vinasemwa kama kumbukumbu katika Surah 16:43, 21:7, 21:48, 21:105 na 40:53-54.
Kwahiyo, Surah 15:9 inakubali kuwa Taurat na Injil zimetunzwa na Allah. Kama ni kweli haya madai ya Quran:http://www.quranitukufu.net/005.html
1. Ipo wapi nakala ya Taurat ambayo Allah ameitunza na aliiteremsha kabla ya Quran?
2. Ipo wapi nakala ya Injil ambayo Allah ameitunza na aliiteremsha kabla ya Quran?
3. Ipo wapi nakala ya Zaburi ambayo Allah ameitunza na aliiteremsha kabla ya Quran?
2. Ipo wapi nakala ya Injil ambayo Allah ameitunza na aliiteremsha kabla ya Quran?
3. Ipo wapi nakala ya Zaburi ambayo Allah ameitunza na aliiteremsha kabla ya Quran?
Kama Waislam wanabisha, tuleteeni nakala ya Taurat iliyo teremshwa na Allah kabla ya Quran, na iwe na aya Adam anasema kuwa yeye ni Muislam.
Kama Waislam wanabisha, tuleteeni nakala ya Taurat iliyoteremshwa kabla ya Quran, na iwe na aya ambayo Ibrahim anasema kuwa yeye ni Muislam.
Waislam, ipo wapi Taurat ambayo mnadai kuwa Allah aliiteremsha kwa Musa? Mbona kila siku mnatuletea aya za Quran ambazo sio Taurat?
Kama kweli Allah aliteremsha Taurat kwa Musa, basi tuonyesheni wapi ilipo hiyo Taurat na sio aya dhaif za Quran. Hivi Quran sasa imekuwa Biblia - Mkusanyiko wa Vitabu?
Allah anadai kuwa aliteremsha Injil: Surat Al Maida 46. Na tukawafuatishia hao Isa bin Maryamu kuyahakikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Taurati, na tukampa Injili iliyomo ndani yake uwongofu, na nuru na inayo sadikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Taurati, na uwongofu na mawaidha kwa wachamngu. http://www.quranitukufu.net/005.html
Waislam, tuonyesheni wapi ilipo nakala ya Injil ambayo Allah anadai kuitunza katika Surat Al Hjr aya ya 9?
Hakika Allah hakuteremsha kitabu chochote kile zaidi ya maneno matupu yaliyo ndani ya Quran ya Jibril.
Allah sio Mungu. Musa hakuwa Muislam, Daudi Hakuwa Muislam, Ibrahim Hakuwa Muislam. Yesu hakuwa Muislam.
Kama kuna Muislam anao ushahid kuwa Musa, Daudi, Ibrahim, Yesu walikuwa Waislam, basi watuonyeshe wapi vilipo vitabu vyao ambavyo Allah anadai kuviteremsha. Waislam, sina muda na aya za Quran zilizo kuja miaka maelfu baadae.
Max Shimba Ministries.
Subscribe to:
Comments (Atom)
Ancient Jewish Wedding Ceremony: “No man knows the day or hour, only the Father”
The Ancient Jewish Marriage Rite: A Detailed Exposition of Betrothal, Preparation, and Consummation Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological ...
TRENDING NOW
-
Baba umenipa funguo muhimu katika Mathayo 16:19 za kufunga na kufungua. Ninatumia funguo hizo kufunga na kufungua, kuvunja na kubamiza kil...
-
Kuna watu wanapitia mateso mengi sana, wengine wamefungwa katika vifungo bila wao kujijuwa basi chukua muongozo huu utakusaidia au itasaid...
-
Adui anakuja kuiba, kuua na kuharibu kila kitu chetu, ni lazima kuwa tayari kupambana na maadui, tujue silaha zetu, na kutumia neno la Mun...
-
Twakusalimu kwa mara ingine katika jina tukufu na takatifu la Yesu Kristo Bwana wetu. Twazidi pia kukushukuru kwa ajili ...