Friday, March 17, 2017

KILA MUISLAM ANA JINI KATIKA MWILI WAKE

Image may contain: 1 person, beard and text
HILI NI JAMBO LA AJABU SANA, MAANA YESU YEYE ALIYATOA MAJINI NDANI YA WATU.
Majini wamepewa ruhusa ya kukaa katika mwili wa Muislam yeyote, hivyo kila Muislam ana Jini kuanzia moja na kuendelea.
Vile vile Majini wameruhusiwa kukaa katika nyumba za Waislam. Katika nyumba yoyote ya Muumini wa dini hiyo, kuna Jini au Majini wanaokaa humo. Ni ukweli usiopingika kuwa bila Majini hakuna Uislamu kama vile pasipo Roho Mtakatifu hakuna Ukristo. Majini ndiyo yaliyomchukua mtume Muham-mad kwa muda wa siku 40 akiwa Mabondeni walikompeleka na kuanza kumuagiza kuhusiana na kuanzisha imani hiyo ya Kiislamu.
Sasa inakuwaje Yesu atoe Majini ndani ya watu kama ilivyo sema kwenye Luke 11:14, Matthew 8:16, Mark 1:34, Luke 4:41, Matthew 8:32, Mark 5:8, nk huku Allah yeye akiwajaza Waislam Majini?
Katika Walawi 19: 31, Mungu ametuonya kutokuwa na uhusiano wowote ule na Majini, LAKINI Allah anasema katika Quran kuwa, ameteua Mtume kwa kila kiumbe mpaka Majini machafu. Hebu soma aya hapa chini
ALLAH ANASEMA KUWA MAJINI YANA MTUME WAO
Quran 6: 130. Enyi makundi ya majini na watu! Je, hawakukujieni Mitume kutokana na nyinyi wenyewe wakikubainishieni Aya zangu, na wakikuonyeni mkutano wa Siku yenu hii. Nao watasema: Tumeshuhudia juu ya nafsi zetu. Na yaliwadanganya maisha ya dunia. Nao watajishuhudia wenyewe ya kwamba walikuwa makafiri.
Ndugu msomaji, natagemea baada ya kusoma hiki kijarida kifupi kuwa umeelewa na kufahamu Allah wa Quran sio Mungu wa Biblia anaye kataza uhusiano na Majini.
Mawali la kujiuliza:
1. Kwanini Mungu wa kwenye Biblia anakataza uhusiano na Majini LAKINI Allah wa Quran anaruhusu uhusiano na Majini?
2. Kwanini Mungu wa Biblia anatoa Majini ndani ya Watu, LAKINI Allah wa Quran anawajaza watu Majini?
3. Kwanini Mungu wa Biblia nasema kuwa Majini yote yataingia Jehannam LAKINI Allah wa Quran anasema kuwa Majini yalisilimu na ni Maislam?
Ndugu msomaji, ushahid wa aya umesha usoma mwenye. Nakushauri umchague Mungu wa Biblia anye kupenda na kulinda kutoka hizo nguvu chafu za Majini.
Karibuni kwa Yesu ambaye ndie Njia Pekee ya Kwenda Mbinguni.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,

1 comment:

Unknown said...

Allah aliyempa kitabu Issa A.S ndiye yeye Allah aliempa kitabu Mtume Muhammad s.a.w. sisi waislam tumeifaham Quran kwa kuisoma kwa madrasa na sio kwenye mitandao huwezi kuifaham Quran kwa kusoma tu kama gazeti katika kila aya kuna matawi yake ambayo inatakiwa itafsiriwe vilivyo sio kama gazeti . Nakushauri tafuta masheikh waliobobea kwenye Quran wakufahamishe.. hakuna jini alieruhusiwa kuingia kwenye mwili wa binaadam sio muislam tu ni binaadam yyt. Unapoona jini ameingia kwemye mwili wa binaadam amekhalifu amri ya Allah s.w (ameasi)..na anaitwa sheitwani. usiwapoteze watu kwa kuisoma quran kama gazeti.. kwa

kuengezea tu, Issa ambae mnamwita yesu ni mtume kama mitume iliyopita na amepewa kitabu kama waliyopewa waliopita na amepewa miujiza na kila mtume anamiujiza yake.. Allah ndie mwenye kujua zaidi

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW