Tuesday, March 14, 2017

MAMILIONI YA WAISLAMU DUNIANI WAMELISHWA KURAN FEKI!

No automatic alt text available.
Mwandishi maarufu wa Kiislamu-Caliph Uthman aliandika Quran na kuchoma aya ambazo hakupendezwa nazo! (Sahih Bukhari 6:61:510)
Hakuchoma tu aya za kuran bali Sura nzima ya kuran ilipotea na kusahaulika. (Sahih Muslim 5:2286)
Vile vile, aya zingine zilifutwa kwa maksudi. (Bukhari 6:61:527).
Mohammad aliwaagiza waislamu kujifunza uislamu kutoka kwa kuran ya Ubai na wala sio ambayo Zayd Ibn Thabit aliandika (ambayo ni ya kisasa) tazama (Bukhari 6:61:521).
Ibn Sad (Kitab al-Tabaqat al-Kabir vol.2 p.444 ) inasema kuwa maandiko ya kuran ya Zayd Ibn Thabit ni tofauti na ya Muhammad. Kwa hivyo waumini wamepotoshwa kwa kukariri kuran hiyo ya kisasa.
Jami At-Tirmidhi 3104 vile vile anasema kuran iliyopo sasa ni feki-ya Zayd Ibn Thabit.
Katika kufanya marekebisho mengi kwenye kuran watu walikuja na nakala tofautitofauti za kuran (Jami at-Tirmidhi 3104) hivyo kulikuwa na mtafaruku miongoni mwa wafuasi wa mohammad kwa sababu zilikuwa tofauti.
Kuran ya Ibn Masood ilikuwa na sura 111, ya Ubay ilikuwa na sura 116 na kuran ya Zayd (ambayo ndio inatumika sasa hivi) ina sura 114. Tazama (Ibn Daud , Kitab al-Masahif).
Hata zile zilizotajwa kuwa feki hazikuhifadhiwa kwa sababu mbuzi alikula sehemu ya aya zake (Sunan Ibn Majah 1934/1944).
Hivyo hamna aliyeandika kuran hadi baadhi ya waliokuwa wanakariri mafunzo ya mohammad kufa na kulikuwa na hofu kuwa aya zilizosalia zingepotea kabisa (Bukhari z6:61:509).
Hivi ndivyo Zayd Ibn Thabit alipata kuandika kuran ambayo tunayo leo hii kutoka kwa shuhuda za wakariri waliobaki (kurasa chache tu kutokana na miaka 23 ya ufunuo).
MASWALI NYETI YAIBUKA HAPA;
1. Je, kwanini historia ya mohammad haikuandikwa kwenye kuran?
2. Je, utajuaje uislamu pasipo kumjua vyema allah na mohammad?
3. Kwanini waislamu wanaficha ukweli kuhusu dini yao?
4. Je, ni kweli kuwa mohammad aliteremshiwa kuran na allah?
5. Je, ni kweli kuwa allah alimtuma mohammad duniani kuwasilimisha watu?
TAFAKARI HAYO NA UCHUKUWE HATUA!
Max Shimba Ministries Org

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW