Tuesday, May 22, 2018

ISHARA YA SIKU ZA MWISHO


YESU ANASEMA: Nanyi mtasikia habari za vita na matetesi ya vita; angalieni, msitishwe; maana hayo hayana budi kutukia; lakini ule mwisho bado.
Umeshawai kusikiliza taarifa ya habari na ukajiuliza hivi, ‘Kwa nini mambo yanazidi kuwa mabaya?’ Dunia imejaa majanga na ukatili unaofanya baadhi ya watu waamini kwamba lazima mwisho wa dunia uwe karibu sana. Je, kweli mwisho uko karibu? Je, kuna njia yoyote ya kujua jambo hilo? Bila shaka. Wanadamu hawawezi kutabiri mambo ya wakati ujao. Ni Mungu pekee anayeweza kutabiri. Katika Biblia, anatueleza kuhusu wakati ujao wa dunia na wanadamu.—Isaya 46:10; Yakobo 4:14.
Nabii Daniel alizungumza juu ya “Wakati wa Mwisho.” Mtume Petro alisema, “katika siku za mwisho watakuja na dhihaka zao watu wenye kudhihaki.” Paulo alisema, “Siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.” Wanafunzi wa Kristo walimwuliza juu ya “Mwisho wa ulimwengu” Je, wakati huo umefika? Unaweza kuwa na uhakika?
Orodha ifuatayo inaonyesha baadhi ya mambo makuu yaliyotabiriwa kutokea katika siku za mwisho, au wakati wa mwisho:
Vita kwa kadiri kubwa.—Mathayo 24:7; Ufunuo 6:4. Yesu alisema: “Taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme.” (Mathayo 24:7) Katika siku zetu watu wengi wamekufa vitani kuliko wakati mwingine wowote katika historia. Ripoti moja ya shirika la Worldwatch inasema kwamba watu zaidi ya milioni mia moja wameuawa vitani tangu mwaka wa 1914. Idadi ya watu waliouawa vitani kwa miaka mia moja tangu mwaka wa 1900 hadi 2000 ni mara tatu zaidi ya idadi ya watu waliouawa kabla ya mwaka wa 1900. Hebu wazia uchungu na mateso ambayo watu wengi wamepata kutokana na vita!
Njaa kali.—Mathayo 24:7; Ufunuo 6:5, 6. Yesu alisema: “Kutakuwa na upungufu wa chakula.” (Mathayo 24:7) Ingawa mazao ya chakula yanakuzwa kwa wingi kuliko zamani, watu wengi hawapati chakula cha kutosha. Kwa nini?
Matetemeko makubwa ya nchi.—Luka 21:11. Yesu alitabiri hivi: “kutakuwa na matetemeko makubwa ya nchi.” (Luka 21:11) Matetemeko makubwa ya ardhi hutokea kila mwaka.
Tauni, au magonjwa mabaya yanayoenea sana.—Luka 21:11. Yesu alitabiri kwamba kungekuwa na “tauni.” Magonjwa hatari yanaenea kwa haraka na kuua watu wengi. (Luka 21:11) Ingawa madaktari wamejifunza kutibu magonjwa mengi, bado kuna baadhi ya magonjwa ambayo hayatibiki.
Kuongezeka kwa uhalifu.—Mathayo 24:12.
Wanadamu kuiharibu dunia.—Ufunuo 11:18.
Kuzorota kwa mtazamo wa watu, na hivyo watu wengi watakuwa “wasio na shukrani, wasio washikamanifu, wasio na upendo wa asili, wasiotaka makubaliano yoyote, wachongezi, wasiojizuia, wakali, wasiopenda wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi.”—2 Timotheo 3:1-4.
Kuvunjika kwa familia, kwa kuwa watu hawana “upendo wa asili” na watoto ‘hawatii wazazi.’—2 Timotheo 3:2, 3.
Upendo wa watu wengi kumwelekea Mungu ungepoa.—Mathayo 24:12.
Unafiki wa kidini unaoonekana waziwazi.—2 Timotheo 3:5.
Kuongezeka kwa uelewaji wa unabii wa Biblia, kutia ndani unabii unaohusiana na siku za mwisho.—Danieli 12:4.
Kuhubiriwa kwa habari njema ya Ufalme ulimwenguni pote.—Mathayo 24:14. Alipokuwa akizungumzia siku za mwisho, Yesu alisema hivi: “Habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote.” (Mathayo 24:3, 14) Habari njema ya Ufalme inahubiriwa katika lugha zaidi ya 700 katika nchi zaidi ya 230.
Watu wengi hawapendezwi na hata wanadhihaki kama kweli mwisho unakaribia.—Mathayo 24:37-39; 2 Petro 3:3, 4.
Unabii wote huu unatimia kwa wakati uleule, si mambo machache tu au sehemu kubwa ya unabii.—Mathayo 24:33.
Je, tunaishi katika “siku za mwisho” au bado ishara hazija timia?
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu. Tito 2:13

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW