Friday, June 8, 2018

KWANINI SHETANI ALIMKABIDHI UFUNGUO WA ULIMWENGU MUHAMMAD S.A.W?

Image result for islam will dominate the world
Katika Sahihi Bukhary Hadithi No 731 uk 219 na Mishkat al- Maswabih Vol ya I Hadithi no 2 uk 3. Aisha mke wa nabii wa
Allah, alimsikia Muhammad anasema nimetokewa na kiumbe mfano wa mwanadamu, mavazi yake yalikuwa meupe sana umezidi weupe wa kawaida. Na nywele zake zilikuwa nyeusi zimezidi weusi wa kaiwada akanionesha funguo za dunia hii akaniambia niakupa funguo hizi ukianguka na kunisujudia. Nami nikiwa katika maono nikaanguka nikamsujudia.
 
Mtume wa Allah anakiri katika hadithi hii kwamba alikusudia kiumbe ambacho ni mfano wa mwanadamu. Lakini kwa bahati mbaya hata kukifahamu kwa jina hakukifahamu ila alikisujudia kwa sababu aliambiwa angepewa funguo za duniani.
 
JE, UNAMFAHAMU NANI NI MUNGU WA HII DUNIA?
 
Katika 2 Wakorintho 4: 4, asiyeamini anafuata mipango ya Shetani: "mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu." Mpango wa Shetani unajumuisha kukuza falsafa za uongo katika ulimwengu- falsafa ambazo zinamfunga macho asiyeamini kwa ukweli wa injili. Falsafa ya Shetani ni ngome ambazo watu wamefungwa, na lazima wawekwe huru na Kristo.
 
Kifungu "mungu wa ulimwengu huu" (au "mungu wa wakati huu") kinaonyesha kwamba Shetani ni mshawishi mkubwa kwa maadili, maoni, malengo, matumaini na maoni ya watu wengi. Ushawishi wake pia unahusisha falsafa za ulimwengu, elimu, na biashara. Mawazo, fikira, ujasusi na dini za uongo za ulimwengu ziko chini ya udhibiti wake na zote zimetokana na uongo wake na udanganyifu.
 
Shetani ni mungu wa ulimwengu huu (2 Wakorintho 4: 4)
 
Shalom,
 
Max Shimba Mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW