Tuesday, January 5, 2016

SINAGOGI SIO MSIKITI


SEHEMU YA KWANZA
Tunazidi kuchambua HOJA ZA MIHADHARA ya Kiislamu
LEO TUANGALIE SINAGOGI!!
Kwa miaka mingi afrika mashariki na kati kunakosemwa kiswahili kumetokea mafundisho ambayo ni mapotofu sana ya kukejeli, na lengo lao hasa ni kuangusha mwili wa Yesu kristo (kanisa) na mafundisho yake. Na kupitia mafundisho hayo wengi wameacha imani iliyo ya kweli nakufuata imani zingine ambazo mwisho wao ni mauti. Na hawa siyo wengine bali ni wahadhiri wakiislamu. Wao hudai kuwa wanafuata mafundisho ya Bwana Yesu. Unukuu aya hii mathayo 11:29-30 pale Yesu alisema jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo nanyi mtapa raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.
Pia wanasema Yesu aliingia kwenye sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake siku ya Sabato luka 4:16.kupitia kwa tendo hili la Yesu kwingia kwenye sinagogi , wahadhiri hawa wanadhai jambo ili linamfanya Yesu kuitwa muislamu. Tafadhali ndugu yangu ukitaka kujua ukweli fuatilia somo hili hadi tamati.. hii ni sehemu ya kwanza. Biblia ya Kiswahili katika maneno magumu imetaja kuwa Sinagogi ni msikiti wa Kiyahudu. hapa majamaa wanakesha!!
Historia ya sinagogi:
Ukitaka kujua mtu Fulani ni lazima uangazie mambo kadha wakadha ikiwemo historia yake, pasina historia ni vigumu watu kufahamu mambo yaliyofichika. Hivyo nimeonelea kuwa ni bora sana kuangazia historia ya sinagogi na chanzo chake. Jambo la msingi kwanza ni kujua maana ya sinagogi. Neno hili Sinagogi maana yake ni mahali pa watu kukutania. Sinagogi lilianzia pale wana wa Israeli walipokuwa utumwani kule Babeli kwa miaka sabini kulinga na unabii wa nabii Jeremia,jeremia 25:11-13.
baadaye nitaeleza tofauti ya Sinagogi na Hekalu.
Sababu ya wayahudi kuanzisha sinagogi ni hizi.
• kule utumwani hawengeweza kurudi kule Yerusalemu ambapo palikuwa na hekalu kwa minajili ya mambo ya ibaada. Kwa hivyo Wayahudi walitafuta jinzi ya kuendelesha ibaada na miandamo ya sikukuu zao.
• Kuendelesha utamaduni wao kama vile kutahiri mtoto wa kiume akiwa na siku nane kulingana na amri ya Mungu mwanzo 17:9-12
• Ili kuzingatia sheria za Mungu kufundishana habari za torati na manabii.
Uongozi
Sinagogi lilikuwa likianzishwa na wazee wapatao saba au kumu wa kiyahudi, kila sinagogi lilikuwa na viongozi wapatao wawili au zaidi. Na vyongozi hao huchaguliwa na wazee wa sinagogi. Katika karne ya agano jipya kulikuwepo masinagogi mengi sana yapatao 480 ambazo zilikuwa zikiingiwa na watu wa wamataifa mbalimbali ambao walikubali kufuata taratibu zote za dini ya kiyahudi.
Kazi ya sinagogi:
Malengo makubwa ya sinagogi yalikuwa kujikumbusha sheria na pia kuangalia utamaduni wao. Tusomapo Biblia na kuichunguza tunaona mambo yafuatayo;
Malaki 4:4
Ikumbukeni torati ya Musa, mtumishi wangu, niliomwamuru huko Horebu kwa ajili ya watu wangu Israeli wote naam, amri ya hukumu.
Mathayo 5:17
Yesu alifundisha hivi:- Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii la sikuja kutangua, bali kutimiliza
Hivyo basi kwa habari za torati na manabii wayahudi walikuwa wakifundisha watoto wao kwenye sinagogi. Matendo 15:21. kwa maana tangu zamani za kale Musa anao watu wahubirio mambo yake; katika kila mji husomwa kila sabato katika masinagogi.

SINAGOGI SIO MSIKITI

TUNAZIDI KUCHAMBUA HOJA ZA MIHADHARA ya Kiislamu
LEO TUANGALIE SINAGOGI!! Sehemu ya pili
Kama tulivyosema Neno SInagogi linatokana na Kigiriki συναγωγή sinagoge likimaanisha "mkutano"; ni tafsiri ya Kiebrania בית כנסת beit knesset yaani "nyumba ya mkutano".

Wayahudi hutumia pia neno la Kiyiddish "shul" (=shule) kutajia sinagogi.
Katika lugha ya kiebrania neno “ beit ” linamaana “ nyumba” ndio maana hata ukisoma bethsaida “ Nyumba ya mvuvi” au bethsania-Nyumba ya masikini. Bethlehemu, nyumba ya mkate. (Soma injili imetajwa sana majina haya )

Katika Israeli ya Kale (kabla ya maangamizi ya Yerusalemu mwaka 587 KK) inaonekana hakukuwa na sinagogi: walau halitajwi kabisa katika Agano la Kale.

Inaonekana ya kwamba masinagogi yalianzishwa baada ya hekalu ya Yerusalemu kubomolewa pamoja na kuanza uhamisho wa Wayahudi kwenda nchi mbalimbali.

Tangu kuharibiwa kwa Hekalu la Pili mwaka 70 Wayahudi wana masinagogi tu kufanyia ibada.
Neno hilo limetumiwa katika maana hiyo ya mukutano kwenye Septuajinti, yaani, tafsiri ya Kigiriki ya Maandiko ya Kiebrania. Lakini, baada ya muda neno hilo lilitumiwa kurejelea jengo ambapo watu walikutana kuabudu. Kufikia karne ya kwanza W.K., karibu kila mji ambao Yesu alitembelea ulikuwa na sinagogi; majiji yalikuwa na masinagogi kadhaa; jiji la Yerusalemu lilikuwa na masinagogi mengi.
Ukumbi wa sala huwa na sehemu zifuatazo:

• sanduku la Torati ni kabati au sanduku ambako hati za kuviringisha zenye mwandiko wa Biblia ya Kiebrania hutunzwa;
• taa inayoendelea kuwaka muda wote;
• meza ya msomaji ambako hati za torati hufunguliwa na kusomwa;
• mimbari ya mafundisho;
• kinara cha menorah chenye mishumaa 7 au 9.
Karibu na sanduku hilo, kulikuwa na viti vya mbele vilivyopangwa kuelekea kutaniko, navyo vilikaliwa na maofisa-wasimamizi wa sinagogi pamoja na wageni wowote waheshimiwa. (Mathayo 23:5, 6)
Hii ni tofauti ni Misikiti ya kiislamu isiyokuwa na Viti
Karibu na eneo la katikati la sinagogi palikuwa na jukwaa lililokuwa na kinara na kiti cha msemaji . Kwenye upande wa mbele, wa kushoto, na wa kulia wa jukwaa hilo, kulikuwa na viti vya washiriki wa kutaniko .
• Kwa kawaida, gharama za kuendesha shughuli za sinagogi zililipiwa na kutaniko. Michango ya hiari iliyotolewa na wote, matajiri kwa maskini, ilitumiwa kurekebisha na kudumisha jengo hilo
Bwana Yesu alipenda sana kufundisha kwenye hekalu na katika masinagogi walimokusanyika wayahudi.

“Sikuzote nilifundisha katika sinagogi na katika hekalu, ambapo Wayahudi wote hukusanyika.”—Yohana 18:20.

Hekalu katika Jerusalemu ( hekalu katika Uyahudi )
Kulikuwa na mahekalu mawili yaliyojengwa katika nyakati tofauti tofauti na watu tofauti tofauti ndani ya Yerusalemu.

Hekalu la kwanza lilijengwa na mtoto wa mfalme Daudi,Mfalme Suleimani. Lilijengwa mnamo mwaka 957 KK.

Hekalu hili likabomolewa na mfalme Nebukadreza II mnamo 586 KK.
Hekalu la pili,

Monday, December 28, 2015

TOFAUTI KUMI NA SABA (17) KATI YA YESU WA WAKRISTO NA ISA WA WAISLAM




Mara kwa mara, unaweza kuwasikia Waislamu wakisema kuwa Isa a.s. kama anavyotajwa ndani ya Qur’an tukufu, ndiye Yesu Kristo wa Nazareti, kama anavyotajwa ndani ya Biblia Takatifu. Wanafanya hivyo kwa kulinganisha baadhi ya aya zilizomo ndani ya Biblia Takatifu, na zile zilizomo ndani ya Qur’an. Kwa mfano, wanasema kwa mujibu wa Biblia mama yake Yesu Kristo anaitwa Mariamu. Wanasoma katika Injili ya Marko 6:3-4“Huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo, na Yose na Yuda na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? Wakajikwaa kwake” . 


Wanafananisha aya hiyo na ile iliyomo ndani ya Qur’an katika Suratul Al-Maidah, 5:75 “ Masih bin Maryam si chochote ila ni mtume tu……”,

Hoja nyingine wanayoitumia ni kusema kwamba eti jina Isa ni katika lugha ya Kiarabu. Jambo hilo siyo kweli. Kwa sababu katika lugha ya Kiarabu, Yesu anaitwa Yasu’a siyo Isa. Na ikumbukwe kuwa Biblia ndicho kitabu kilichotangulia kuwepo duniani miaka ipatayo 1500 kabla ya Qur’an.(Qur’an is a post Bible book).

Hoja yetu kwa Waislamu ni hii nani aliyebadilisha jina Yasu’a kuwa Isa?. Jina Yasu’a linashabihiana zaidi na Jina Yehoshua ambalo hilo ni katika lugha ya Kiebrania, na katika Kiyunani lugha iliyotumika kuandika Agano Jipya anaitwa Iesous (tamka Yesu) tafsiri ya maneno hayo kwa lugha ya Kiswahili ni Mwokozi.

Tunasoma hayo katika Math 1:21-23 “ Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana yeye ndiye atakaye waokoa watu wake na dhambi zao. Hayo yote yamekuwa ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa Nabii akisema Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi.”

Hoja yetu Je Isa a.s naye ni Mwokozi na Imanueli kama alivyo Yesu Kristo?.

Jambo jingine tunalopaswa kulizingatia tunapoangalia tofauti zao ni kuhusu mama zao. Mama yake Yesu Kristo ni Mariam anayetoka katika ukoo wa Yuda. Tunasoma hayo katika kitabu cha Mwanzo 49:10 “ Fimbo ya enzi haitaondoka katika Yuda, Wala mfanya sheria kati ya miguu yake,Hata atakapokuja Yeye, mwenye milki,Ambaye mataifa watamtii”.

Unabii huu umetimia kwa Yesu Kristo.Tunasoma hayo katika Waebrania 7:14 “Maana ni dhahiri kwamba Bwana wetu alitoka katika Yuda, kabila ambayo Musa hakunena neno lolote juu yake katika mambo ya ukuhani”

Lakini tusomapo habari za Isa, yeye mama yake anatoka ukoo wa Imrani. Ambaye ni baba yao Haruni, Miriamu na Musa. Tunayasoma hayo katika Suratul Al-Maryam 19:28 “Ewe dada yake Haruni. Baba yako hakuwa mtu mbaya. Wala mama yako hakuwa hasharati”.

fafanuzi unaoifafanua aya hii ya 19:28 uliyomo ndani ya Qur’an, tafsiri ya King Fahd uk. 405, unasomeka hivi “ This Harun (Aaron) is not the brother of Musa (Moses), but he was another pious man at the time of Maryam (Mary)”

Tafsiri “Huyu Harun siyo ndugu yake Musa, bali alikuwa ni mtu mwingine tu mcha Mungu, aliyeishi wakati wa kipindi cha Maryam”
Kwa mujibu wa Biblia, Haruni ni mtoto wa mzee Amran na mama yao anaitwa Yekobedi na kwao wamezaliwa watoto watatu Haruni, Miriam na mdogo wao Musa. Tunasoma hayo katika kitabu cha Hesabu 26:59 “Na jina la mke wa Amramu aliitwa Yokebedi binti wa Lawi ,ambaye alizaliwa kwake Lawi huko Misri; na huyo Yokebedi akamzalia Amram Haruni,na Musa,na Miriamu umbu lao”

Tofauti nyingine ni kuumbwa kwao: ISSA KAUMBWA. Qur’an Suratul Imran, 3:59 “ Bila shaka hali ya Isa kwa Mwenyezi Mungu ni kama hali ya Adam; alimwumba kwa udongo kisha akamwambia: “Kuwa”; basi akawa”

Lakini tusomapo kumhusu YESU, YEYE HAKUUMBWA BALI NI NENO LA MUNGU.

Yoh 1 : 1,14 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu naye Neno alikuwa Mungu……..Naye Neno alifanyika mwili akakaa kwetu…….”

Mika 5:2 “ Bali wewe, Bethlehem Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israel; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele”

Yoh: 8:58 “ Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahim asijakuwako, mimi niko”.

Zaidi ya hayo Biblia inatujulisha kuwa yeye ndiye Muumbaji mwenyewe

Yoh 1:3 “Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika chochote kilichofanyika”

Kol 1:16-17 “ Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana ; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake”


2) (A) ISSA A.S : BAADA YA KUONDOKA KWAKE, (KAMA WAISLAMU WANAVYOAMINI), HAJAWAHI KUTOKEA KWA NAMNA YOYOTE ILE.

Wednesday, December 16, 2015

UTAMU WA MAISHA YA NDOA

(Sehemu ya Kwanza)

NDOA NI NINI?Ndoa ni muungano kati ya mwanamke na mwanamume kuishi pamoja kama mume na mke muda wote wa maisha yao.
Kwa kuwa si kusudi letu kutafakari sheria za nchi zinasema nini kuhusu Ndoa, tungependa kujikita zaidi katika maana ya Ndoa kwa imani ya kikristo ambayo msingi wake unajengwa katika neno la Mungu. Hata hivyo tunapenda kuweka wazi kwamba Ndoa ni suala la kisheria, na ni muhimu sana kwa wanandoa kutambua kwamba zipo taratibu za kisheria zilizowekwa na serikali zinazosimamia masuala ya Ndoa. Kwa kuwa tumefanyika wana wa Mungu, mwenendo wetu na maisha yetu ya Ndoa yanaongozwa na imani yetu kwa Mungu na si sheria za kibinadamu.
Katika imani ya kikristo, Ndoa inaweza kutafsiriwa kama “AGANO KATI YA MWANAMKE NA MWANAMUME AMBAO WAMEKUSUDIA KWA HIARI KUAMBATANA NA KUISHI PAMOJA KAMA MKE NA MUME KWA SIKU ZOTE ZA MAISHA YAO.” Jambo la msingi kulitambua hapa ni kwamba Ndoa ya kikristo ni AGANO. Kuna tofauti kubwa kati ya kile kinachoitwa “AGANO” na “MKATABA” kimsingi agano ni zaidi ya mkataba kwa namna nyingi.
i) Wanaooana wawe wamekubaliana pasipo kulazimishwa na mtu.
ii) Ndoa ni ya mwanamke na mwanamume.
iii) Ni ndoa ya kudumu maishani.
Mpango na utaratibu wa MUNGU kwa wanandoa umewekwa wazi katika kitabu cha Mwanzo.
“Bwana MUNGU akasema si vema mtu huyu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufafana naye”. Mwanzo 2:18.
Hapa tunaona kuna suala la mamlaka katika ndoa, kwamba mke ni msaidizi.
“Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja”. Mwanzo 2:24.
Hapa tunaona kusudi la MUNGU katika suala la kuachana na kuambatana. Wanandoa wanatakiwa kuachana na wazazi wao katika maeneo matatu.
i) Kimwili – wawe na makazi yao wenyewe
ii) Kihisia – wategemeane na kutiana moyo na kusaidiana
iii) Kiuchumi – wajitegemee kwa mahitaji yao ya kila siku.
TUWE MAKINI, NDOA SI JAMBO LA MCHEZOKatika maisha ya mwanadamu, kuna mambo mawili yaliyo muhimu zaidi. La kwanza ni uamuzi wa kumfuataYesu na la pili ni uamuzi wa kuoa. Tafakari, kuoa si sawa na kununua shati. Ukilichoka na shati unaweza kununua nyingine lakini, huwezi kumwacha mke wako hata kama ukimchoka. Neno la Mungu linatuonya hatari ya kuoa mwanamke asiye mchaji wa Mungu; Twasoma: “Ni afadhali kukaa katika nchi ya nyika; kuliko na mwanamke mgomvi, mchokozi” (Mithali. 21:19). “Kutonatona daima siku ya mvua nyingi, na mwanamke mgomvi ni sawasawa; 16atakaye kumzuia huyo huuzuia upepo” (Mithali. 27:15-16). Zingatia: Pengine mtu atasema, “mchumba wangu ana imani tofauti, walakini tukioana nitamfundisha.”Lakini ikumbukwe mara nyingi, baada ya kufunga ndoa, watu hubadilika asitake kufundishwa tena.Tukumbuke mfalme Sulemani alikuwa na hekima kuliko wanadamu wote. Walakini, alipata hasara kubwa kwa sababu aliwapenda wanawake wageni wasio mcha Mungu na matokeo yake badala ya kuwafundisha imani yake, “yeye mwenyewe alinaswa na imani yao” (1Wafalme 11:1-4). Basi tujiulize, je sisi tunayo hekima kuliko Sulemani? Ni bora mtu amfundishe mchumba kabla hawajaoana na kuhakikisha kuwa ameamua kumfuata Bwana kwa moyo wake wote na si kwa sababu ya ndoa, ndipo atakapokuwa na amani na furaha katika ndoa yake. Tukumbuke faida moja wapo ya kuoa katika katisa ni kupata mke alifundishwa maadili na wanawake waliomtangulia; Twasoma: “Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wautakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wafundishao mema; ili wawatie – wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na uwapenda watoto wao; na kuwa wenye kiasi, kuwa safi,kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe, ili neno la Mungu lisitukanwe” (Tit. 2:3-5). Hivyo ni dhahiri kuna faida kwa mkristo kujipatia mke aliyefunzwa maadili ya ndani ya kanisa. Zingatia: Kuna baadhi ya watu wamevutwa sana na maumbile au mambo ya kimwili ya wachumba wao lakini Biblia inatukumbusha kuchunguza mioyo yao zaidi kuliko sura ya nje; Tasoma: “Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa” (Mithali. 31:30). “Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye; bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana” (Mithali 19:14). Je unazijua sifa za mke mwema? Mungu ameeleza peupe; Soma: (Mithali 31:10-31)
NDOA -TAASISI TAKATIFUNdoa yenye furaha na kuheshimika ni ile ambayo kila mmoja anafahamu na kutimiza wajibu wake katika ndoa kwa mujibu wa nafasi yake. Na hii ndio sharti la msingi kutupelekea kwenye ndoa yenye mafanikio.
i) Kumheshimu mwenzi wako kutokana na hadhi aliyonayo kama MUNGU alivyoagiza.
ii) Heshima inasaidia kutuepusha na ubinafsi na kuongozwa na hisia.
iii) Heshima katika ndoa inachochea mapenzi.
HATARI YA KUOANA NA ASIYE MCHAJI WA MUNGUKama tulivyojifunza hako juu hatari moja wapo ya kuoana na wasio wachaji wa Mungu ni kuishia kuvutwa na upotofu na kuanguka kiimani; Twasoma:”Kwa kuwa atamkengeusha mwanao mume asinifuate, ili wapate kuabudu miungu mingine; ndipo itakapowaka hasira ya Bwana juu yenu, naye atakuangamiza upesi” (Kumbukumbu 7:4). Na hayo ndiyo yaliyomapata Suleima kama tulikwisha kuoona; Soma tena: (1 Wafalme 11:1-4) Tukumbuke ikiwa tutaanguka katika uovu, mwisho wake utakuwa ni kutupwa katika hukumu (adhabu ya milele); Twasoma: “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uachafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui,ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayo fanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.” (Galatia 5:19-21) “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauwaji, na wazizi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili” (Ufunuo 21:8) “Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani hilo ziwa la moto. Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.” (Ufunuo 20:14- 15) Zingatia: Ndoa ni kifungo hivyo tukumbuke tunapoana hatuna ruhusa ya kuacha hata kama wenzi wetu ni wabaya vipi; Twasoma: “Lakini wale waliokwisha kuoana nawagiza; wala hapo si mimi, ila Bwana; mke asiachane na mumewe; lakini ikiwa ameachana naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena mume asimwache mkewe.” (1 Wakorintho 7:10-11) “Mwanamke hufungwa maadamu mumewe yu hai, lakini ikiwa mumwe amefariki, yu huru kuolewa na mtu ye yote amtakaye; katika Bwana tu.” (1 Wakorintho 7:39)
Hivyo ni dhahiri tunaaswa kuwa makini tunapo wachagua wenzi wetu, tukikumbuka ya kuwa kifungo cha ndoa ni mpaka kifo.
NDOA NI KUTOA1. Ndio sio mkataba wa kijamii bali agano la kiroho. Waefeso 5:31-33 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. Siri hiyo ni kubwa, ila mimi nanena habari ya KRISTO na Kanisa. Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe, wala mke asikose kumstahi mumewe.
Hapa tunajifunza
i) Ndoa ni fumbo la ajabu la kiroho linalowaunganisha watu wawili, mwanamume na mwanamke (mst.31)
ii) Ndoa ya kikristo inaliganishwa na uhusiano uliopo kati ya KRISTO na Kanisa (mst.32)
iii) Mpango wa MUNGU katika ndoa unahitaji upendo wa kujitoa sadaka kama KRISTO anavyofanya kwa Kanisa (mst.33)
2. Ndoa ya Kikristo ni kujitoa sio kupokea. Wafilipi 2:3-4 Msitende neno lolote kwa kushindana wala kwa majivuno, bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenzie kuwa bora kuliko nafsi yake mwenyewe. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.
Hapa tunajifunza
i) Kutokuwa wabinafsi
ii) Unyenyekevu
iii) Roho ya kutoa na kujitoa.
Wewe mume/mke, mahusiano yako na mwenzi wako yakoje? Unampenda mwenzi wako kama KRISTO anavyolipenda Kanisa lake? Kama wewe ni mmojawapo wa wasiofuata kielelezo cha KRISTO katika ndoa usijisikie vibaya kwani hakuna aliye mkamilifu. Hata hivyo wajibu huu haukwepeki kwani ni agizo la MUNGU na lazima kutii maagizo yake, kumpenda MUNGU kwa moyo waklo wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote na kwa nguvu zako zote. Na kumpenda jirani yako kama nafsi yao. Marko 12:30-31. Hivyo, hii ni nafasi yako ya kumwonyesha mwenzi wako upendo ambao wa muda mrefu ameukosa, upendo ambao KRISTO ameuonyesa kwa kanisa lake.
Max Shimba Ministries

KWANINI HAKUNA NGUVU YA UPONYAJI KATIKA UISLAM? MBONA KATIKA UKRISTO WATU WANAPONA KWA JINA LA YESU?

1. KWANINI JINA LA ALLAH HALINA UWEZO WA KUPONYA MAGONJWA?
2. ALLAH ASHINDWA KUMPONYA MUHAMMAD
3. MAOMBI YA JIBRIL YAGONGA MWAMBA
4. LAKINI JINA LA YESU LINAPONYA MAGONJWA YOTE
5. JE, UMESHA WAI ONA KUNA MKUTANO WA UPONYAJI KATIKA USILAM?

Ndugu msomaji,

Uponyaji ni nini?
Ni tendo la kiimani la kupokea uzima katika roho au mwili kwa njia ya kuombewa,kuwekewa mikono au kulisikia neno sahihi la Kristo Yesu. Tendo hili la kiimani humletea mwamini uzima wa kiroho na afya ya kimwili pale ilipopunguka,kumbuka~wengi walipoponywa udhaifu wa miili yao,waliponywa pia na roho zao.

Hivyobasi, kwanini Allah alipo mtuma Jibril kwenda kumuombea uponyaji Mtume wake Muhammad kwa ugonjwa uliosababishwa na kula sumu, maombi yao hayakufanya kazi?

Hivyo basi, uponyaji haufanywi na mtu awaye yoyote yule isipokuwa Mungu. Hata madaktari bingwa wao hawaponyi bali hutoa tiba tu, mwenye kuponya ni Mungu. Watumishi wa Mungu pekee ndio hufanyika kama daraja au chombo cha kuleta uponyaji ulioachiliwa na Bwana kwa muhusika mwenye kuhitaji.

HEBU SASA TUMSOME ALLAH NA JIBRIL KATIKA JARIBIO LAO LA KUMPONYA MUHAMMAD:
Ibn Sa'd Ukurasa wa 265
Aisha, Mke wa Mtume Muhammad alikuwa akisema, "Wakati Nabii wa Allah alipo kuwa anaumwa, Jibril alikuwa anamwombea Muhammad kwa Allah kwa kusema haya "Katika Jina la Allah ambalo litakuponya kutoka kila magonjwa na maumivu na kutoka kila wenye ubaya nawe na kila wanakuombea ubaya, utapona..

Je, jina la Allah liliweza kumponya Muhammad? Hebu tusome Sahih hadith kama ilivyo letwa na Al Bukhari:


MAJIBU YA MUHAMMAD BAADA YA KUOMBEWA UPONYAJI NA ALLAH/JIBRIL:
Bukhari's Hadith 5.713:
Imesemwa na 'Aisha:
Mtume Muhammad wakati alipo kuwa anaumwa na kuchukuliwa na kifo alikuwa akisema, O Aisha, bado nasikia maumivu makali sana kutokana na chakula nilicho kula kilicho kuwa na Sumu kule Khaibar, na wakati huu nasikia kama nyongo yangu inakatwa kutokana na ile Sumu niliyo kula.

Hivi Mungu anaweza kuomba na ashindwe? Mbona Allah na Jibril maombi yao ya uponyaji kwa Muhammad hayakufanya kazi?


SASA TUMSOME YESU WA KWENYE BIBLIA, JE ALIWEZA KUPONYA WATU?
“ Hata Yesu alipofika nyumbani kwa Petro, akamwona mkwe wa Petro, mamaye mkewe, amelala kitandani hawezi homa. Akamgusa mkono, homa ikamwacha; naye akaondoka, akawatumikia.” Mathayo 8:14-15

Biblia haituambii kwamba Bwana Yesu alimwombea huyu mama,bali tunachoweza kuona ni kwamba Bwana Yesu alimgusa mkono,homa ikamwacha. Mguso tu wa mtu wa Mungu ni dawa tosha,hata kama hakuomba sababu upako ungalimo ndani yake. Maana hata wakina Petro waliweza kuponya wagonjwa kwa kivuli chake tu,sababu ya upako. (Matendo 5:15)


UMUHIMU WA KUWEKA IMANI YAKO KATIKA JINA LA YESU KRISTO
“Basi Petro na Yohana walikuwa wakikwea pamoja kwenda hekaluni, saa ya kusali , saa tisa. Na mtu mmoja aliyekuwa kiwete toka tumboni mwa mamaye alichukuliwa na watu, ambaye walimweka kila siku katika mlango wa hekalu uitwao Mzuri, ili aombe sadaka kwa watu waingiao ndani ya hekalu. Mtu huyu akiwaona Petro na Yohana wakiingia hekaluni aliomba apewe sadaka. Na Petro, akimkazia macho, pamoja na Yohana, akasema, Tutazame sisi. Akawaangalia, akitaraji kupata kitu kwao. Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. KWA JINA LA YESU KRISTO WA NAZARETI, simama uende. Akamshika mkono wa kuume, akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikatiwa nguvu. Akaondoka upesi akasimama, akaanza kwenda …” (Matendo ya Mitume 3:1 – 8)

Ukifuatilia historia ya kilema huyu aliyeponywa utaona ya kuwa alikuwa hivyo tangu kuzaliwa, na alipopona alikuwa na umri uliopita miaka arobaini (Matendo ya Mitume 4:22).

Siri ya muujiza huu ilikuwa ni nini? Je! kilema huyu alipona kwa uweza wa Petro na Yohana au kwa uweza wa jina la Yesu Kristo?
Nauliza maswali haya kwa kuwa watu wengi wakimwona mtu anatumiwa na Mungu katika uponyaji wanaweka imani katika mtu huyo badala ya kuweka imani katika jina la Yesu Kristo.

Na ndivyo ilivyokuwa wakati kilema huyu alipopona, watu waliokuwa hekaluni waliwashangaa wakina Petro na Yohana kama vile kilema huyo alipona kwa uwezo wao. Petro alipoona hali hiyo, aliamua kuwaeleza watu hao ukweli ulivyo; alisema hivi;

“Basi (Yule aliyekuwa kilema) alipokuwa akiwashika Petro na Yohana, watu wote wakawakusanyikia mbio katika tao lile lililoitwa tao la Sulemani, wakishangaa sana. Hata Petro alipoyaona haya akawajibu wale watu, Enyi Waisraeli, mbona mnastaajabia haya, au mbona mnatukazia macho sisi, kama kwamba tumemfanya huyu aende kwa nguvu zetu sisi au kwa utauwa (utakatifu) wetu sisi?” (Matendo ya Mitume 3:11 – 12).

Petro alikuwa anafanya jambo muhimu hapa kwa kusaidia kubadilisha mawazo ya watu ya kufikiria kuwa uwezo uliomponya kilema ulikuwa ni wa Petro na Yohana ambayo haikuwa si kweli. Kama uwezo huu haukuwa wao, muujiza huu siri yake ni nini? Petro aliendelea kusema hivi;

“Mungu wa Ibrahimu na wa Isaka na wa Yakobo, Mungu wa Baba zetu, amemtukuza mtumishi wake Yesu ….. Na kwa IMANI KATIKA JINA LAKE, JINA LAKE LIMEMTIA NGUVU mtu huyu mnayemwona na kumjua; na imani ile iliyo kwake yeye imempatia huyu uzima huu mkamilifu mbele zenu ninyi nyote” (Matendo ya Mitume 3:13 – 16).

Hebu tafakari maneno haya ya Petro; “Na kwa IMANI KATIKA JINA LAKE JINA LAKE LIMEMTIA NGUVU MTU HUYU….” Wakina Petro na Yohana waliweka imani yao katika jina la Yesu Kristo. Walikuwa na uhakika mioyoni mwao kuwa siri ya miujiza imo katika jina la Yesu Kristo – ndiyo maana walipomkuta huyo kilema walimwamuru asimame kwa jina hilo!

Weka imani yako katika jina la Yesu Kristo ukitaka kuona ishara na miujiza ya Yesu Kristo maishani mwako na kwa wale unaowahudumia pia. Wakijua hili wanafunzi wa kwanza wa Yesu Kristo walipokatazwa “wasiseme kabisa wala kufundisha kwa jina la Yesu” na Anasi kuhani mkuu, waliomba wakasema; “…Basi sasa, Bwana, yaangalie matisho yao; ukawajalie watumwa wako kunena neno lako kwa ujasiri wote, ukinyosha mkono wako kuponya; ISHARA NA MAAJABU vifanyike kwa JINA LA MTUMISHI WAKO MTAKATIFU YESU” (Matendo ya Mitume 4:18,29 – 31)

Ni muhimu kuwaeleza na kuwakumbusha watu umuhimu wa kuweka imani zao katika jina la Yesu Kristo wakitaka kuona mkono wa Bwana ukiponya, ukifanya ishara na miujiza.

Ndugu msomaji, kwanini upoteze muda wako kwa waganga wa kienyeji au wapiga ndumba? Hebu liite Jina la Yesu aliye hai, maana anataka kukuponya magonjwa yako yote.

Kama unasumbuliwa na ugonjwa wowote ule, tafadhali wasiliana nasi kwa kupitia maxshimbaminsitries@gmail.com au tupigie simu (347) 770-4886. Haijalishi ni ugonjwa gani, wewe wasiliana nasi, na hakika Jina la Yesu litakuponya.

Max Shimba Ministries 2015

Monday, December 14, 2015

JINSI YA KUTOA PEPO WABAYA/CHAFU

Maana ya neno pepo linamaanisha, pepo mbaya, shetani, mwovu, mharibifu na mwangamizi. Hao ni malaika waliomuasi Mungu wakatupwa duniani. “Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na Yule joka (Shetani), Yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; Nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni. Yule joka akatupwa, Yule mkubwa, Yule wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.” Ufu 12:7-9.
1. Ili kutoa pepo, kuna mambo ambayo yanapaswa kuzingatiwa:
Ni lazima uwe na nguvu za Roho Mtakatifu.Tunaweza kujifunza kwa Yesu alivyoweza kutoa pepo kwa uwezo na nguvu za Roho. Imeandikwa, “…..awaaamuru pepo wachafu kwa uwezo na nguvu, nao hutoka.” Luka 4:36.
2. Kutoa pepo kwa jina la Yesu. Aliye na amri na mamlaka ya kutoa pepo ni mkristo ambaye amemwamini Yesu Kristo kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yake. “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo……” Math 16:17. Wale ambao bado hawajamwamini Yesu na kuokoka, Si vyema kujaribu kutoa Pepo kwa sababu hatatoka, vile vile wanaweza kushambuliwa na hao walio na Pepo, kama wale wana wa Skewa, Kuhani Mkuu.
“.....wakajaribu kutaja jina la Bwana Yesu juu yao waliopagawa na pepo wachafu, wakisema, Nakuapisha kwa Yesu, Yule anayehubiriwa na Paulo. Walikuwako wana saba wa mtu mmoja Skewa, Myahudi, Kuhani Mkuu, walifanya hivyo..... na yule mtu aliye pagawa na pepo wachafu akawarukia wawili, akawaweza, akawashinda, hata wakatoka mbio katika nyumba ile hali wa uchi na kujeruhiwa.” Mdo 19:13-16.
3. Kufanya maombi kila siku na wakati mwingine kufunga. Bila kufanya hivyo haiwezekani kwa neno lolote, ndio maana Yesu alisema “Lakini kwa namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.” Mat 17:21.
4. Kutoa pepo kwa imani. Unaweza kujifunza kwa wale wanafunzi wa Yesu waliposhindwa kumtoa pepo Yule kijana. Walishindwa kwa sababu ya upungufu wa imani. Wangekuwa na imani wangeweza kumtoa Yule pepo. “Kisha wale wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha wakisema, mbona sisi hatukuweza kumtoa? Yesu akawaambia kwa sababu ya upungufu wa imani yenu…..” Mat 17:19-20.
5. Kutoa pepo kwa amri na mamlaka. Unaamuru kwa jina la Yesu atoke naye hutoka. Tunaweza kujifunza kwa Mtume Paulo alivyomtoa pepo Yule kijakazi, akaamuru kwa kumwambia Yule pepo, “..…nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo mtoke huyu, Akamtoka saa ile ile.” Mdo 16:18.
6. Makosa yanayofanyika kwa wale ambao wanakemea pepo, kwa kuwaambia ninakuangamiza kwa damu ya Yesu, ninakuteketeza kwa moto, au ninakufunga. Kufanya hivyo ni kinyume na mamlaka ya Mungu aliyowapa watoto wake. Kwa sababu hiyo, Mungu hajatupa mamlaka ya kuwaangamiza, Kuwateketeza, wala kuwafunga. Bado pepo watakuwepo katika dunia hii kwa sababu wakati wao wakuhukumiwa na kuteswa haujafika. Ndio maana pepo walipomuona Yesu, “…..wakasema,Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?” Mat 8:23.
7.Wakati wa kumhudumia mwenye pepo si sahihi kuongea na mapepo na kuwaliza maswali wametoka wapi, nani akawatuma, ni kwa nini wanamtesa huyo mtu. Hatupaswi kumsikiliza shetani na mapepo yake kwa sababu wao ni waovu na waongo siku zote. “....Asemapo uongo husema yaliyo yake mwenyewwe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo” Yn 8:44. Yesu Krsto hakufanya hivyo ambaye ndiye kielelezo chetu katika utumishi, ijapokuwa alimwona yule mtu aliyekuwa amepagawa na kuteseka siku nyingi alimuuliza swali akitaka kujua jina lake, si jina la pepo.Badala yake pepo waliokuwa wamemtawala yule mtu walijibu wao ni jeshi. “Yesu akamwuliza jina lako nani? Akasema jina langu ni jeshi; kwa sababu pepo wengi wamemwingia”. LK 8:30.
Pepo atolewapo hutaka kurudi.
Pepo anapotolewa ndani ya mtu aliyempagawa huondoka na baadae hurudi na kuangalia kama anaweza kuingia tena.Ikiwa mtu huyo anaishi maisha ya dhambi huona nyumba ni chafu na kuingia."Pepo mchafu amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, aspate. Halafu husema, nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa. Mara huenda akachukua pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya". Mt12:43-45.

ZIJUE AHADI ZA MUNGU KATIKA MAISHA YAKO

Mungu hutimiza ahadi zake. Imeandikwa katika 2Wakorintho 1:19-20 "Maana Mwana wa Mungu, Kristo Yesu aliyehubiriwa katikati yenu na sisi yaani mimi na Silwano na Timotheo hakuwa Ndiyo na siyo; bali katika yeye ni Ndiyo. Maana ahadi zote za Mungu zilizopo katika yeye ni Ndiyo; tena katika yeye ni Amin, Mungu apate kutukuzwa kwa sisi."
Mungu hazirudishi ahadi zake au kuzibadilisha. Imeandikwa katika Zaburi 89:34 "Mimi sitalihalifu agano langu, sitalibadili neno lililotoka mdomoni mwangu."
Hakuna mojawapo ya ahadi za Mungu ambazo hazijatimika. Imeandikwa katika Yoshua 23:14 "Angalieni mimi nimekwenda njia ile waendayo watu wote wa ulimwengu...... Mungu wenu katika habari zenu yote yametimia kwenu hapana neno lo lote mlilopungukiwa."
Tumeahidiwa uzima wa milele. Imeandikwa katika 1 Yohana 2:25 "Nahii ndiyo ahadi aliyotuahidia, yaani uzima wa milele."
Mungu aweza kufanya mambo yasiyowekana. Imeandikwa katika Luka 18:27 "Akasema yasiyowezekana kwa wanadamu yawezekana kwa mungu." Tume ahidiwa moyo mpya na maisha mapya Imeandikwa Ezekieli 36:26 "Mimi nitawapa moyo mpya nami nitatia roho mpya ndani yenu nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama." Ametuahidi kutusamehe dhambi zetu. Imeandikwa katika 1Yohana 1:9 "Tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote."
Ametuahidi tunda la roho. Imeandikwa katika Wagalatia 5:22-23 "Lakini tunda la roho ni upendo, furaha amani, uvumilivu, utu wema fadhili uaminifu, upole, kiasi juu ya mambo kama hayo hakuna sheria."
Ametuahi kututoa katika hofu. Imeandikwa katika Zaburi 34:4 "Nilimtafuta Bwana akanijibu, akaniponya na hofu zangu zote."
Ameahidi wokovu. Imeandikwa katika Isaya 49:25, "... Kwa maana nitateta na yeye atetaye nawe, nami nitawaletea wana wako wokovu."
Ameahidi Roho mtakatifu Imeandikwa Luka 11:13 "Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho mtakatifu hao wamwombao?."
Atatutimizia mahitaji yetu. Imeandikwa katika Wafilipi 4:19, "Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu."
Hatatunyima lililo jema. Imeandikwa katika Zaburi 84:11 "Kwa kuwa BWANA, Mungu ni jua na ngao, BWANA atatoa neema na utukufu. Hatawanyima kitu chema hao waendao kwa ukamilifu."
Ametuahidi hekima. Imeandikwa katika Yakobo 1:5 "Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima na aombe dua kwa Mungu awapae wote kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa."
Mungu ametuahidi amani. Imeandikwa katika Isaya 26:3 "Utamlida yeye ambaye moyo wake umekutegemea katika amani kamilifu, kwa kuwa anakutumaini."
Mungu ametuahidi kutuepusha na majaribu. Imeandikwa katika 1Wakorintho 10:13 "Jaribu halikuwapata ninyi isipokuwa lililo kawaida ya binadamu; ila Mungu ni mwaminifu; hatawacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wakutokea ili muweze kustahimili."
Tumeahidiwa afya njema na tiba. Imo katika Biblia, Yeremia 30:17 "Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema BWANA..."

YESU NI MUNGU AMBAYE ANAPONYA MAGONJWA YOTE

Yesu alisema kwamba ishara moja itakayofuatana na waaminio ni kwamba wataweka mikono juu ya wagonjwa nao watapona (ona Marko 16:18).
[Yesu] Akawaambia, Enendeni ulimwengu mwote mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini atahukumiwa. Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya (Marko 16:15-18).
Mtumishi afanyaye watu kuwa wanafunzi, akiwa anaiga huduma kamilifu ya Kristo, hakika atatumia vipawa vyake kuendeleza huduma ya uponyaji wa Mungu katika eneo lake la ushawishi. Anajua kwamba uponyaji wa Mungu hukuza ufalme wa Mungu kwa njia mbili. Kwanza – miujiza ya uponyaji ni matangazo mazuri sana kwa Injili, kama mtoto yeyote anayesoma Injili au kitabu cha Matendo atakavyoelewa (ingawa watumishi wengi wenye madigirii makubwa wanaonekana hawaelewi). Pili – wanafunzi wenye afya njema hawazuiwi kufanya huduma kwa magonjwa binafsi.
Pia, mtumishi anayefanya wengine kuwa wanafunzi anahitaji kuwa makini kwa wale katika mwili wa Kristo wanaohitaji uponyaji, ila wana shida ya kupokea. Mara nyingi wanahitaji mafundisho ya taratibu na kutiwa moyo kwa upole, hasa kama wamefikia mahali pa kupingana na ujumbe wowote wa uponyaji. Mtumishi anayefanya wengine kuwa wanafunzi anakabiliwa na uchaguzi: anaweza kuepuka kufundisha kuhusu uponyaji wa Mungu moja kwa moja. Akifanya hivyo, hakuna atakayekwazika wala hakuna atakayeponywa. Au, anaweza, kwa upendo sana, kufundisha somo hilo na kudiriki kuwakwaza wengine huku akiwsaidia wengine kupokea uponyaji. Mimi binafsi nimeamua kufanya la pili, nikiamini kwamba ni kufuata mfano wa Yesu.
Uponyaji Pale Msalabani
Mahali pazuri pa kuanza kujifunza kuhusu uponyaji wa Mungu ni katika sura ya hamsini na tatu ya kitabu cha Isaya, ambayo huhesabika kuwa unabii kuhusu Masiya. Kwa njia ya Roho Mtakatifu, Isaya anaeleza vizuri sana juu ya kifo cha Yesu cha kujitoa dhabihu na kazi ambayo angetimiza msalabani.
Hakika ameyachukua masikitiko yetu, amejitwika huzuni zetu. Lakini tuimdhania ya kuwa amepigwa, amepigwa na Mungu na kuteswa. Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, alichubuliwa kwa maovu yetu. Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, na kwa kupigwa kwake sisi tumepona. Sisi sote kama kondoo tumepotea; kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe, na BWANA ameweka juu yake maovu yetu sisi sote (Isaya 53:4-6).
Kwa uvuvio wa Roho Mtakatifu, Isaya alitangaza kwamba Yesu alibeba huzuni na masikitiko yetu. Tafsiri nzuri ya lugha ya asili ya Kiebrania inaonyesha kwamba Yesu alichukua magonjwa na maumivu yetu.
Neno la Kiebrania huzuni katika Isaya 53:4 ni neno choli, ambalo pia linapatikana katika Kumbu. 7:15; 28:61; 1Wafalme 17:17; 2Wafalme 1:2; 8:8; na 2Nyakati 16:12; 21:15. Katika maandiko haya yote linatafsiriwa kama magonjwa au maradhi.
Neno masikitiko katika Kiebrania ni makob, ambalo pia linapatikana katika Ayubu 14:22 na 33:19. Pote hapo linatafsiriwa maumivu.

YESU NI MUNGU NA ANATAKA KUKUOKOA

Watu wengi wanaelewa kuwa Yesu alikuwa mtu ambaye aliishi Israeli miaka 2000 iliyopita. Takribani kila dhehebu ulimwenguni lamchukulia Yesu kama mwalimu mwema/nabii. Huku hayo mambo yakiwa kweli kuhusu Yesu, hayaangazii kabisa Yesu kwa ni nani, ama kuelezea jinzi au kwa nini Yesu aokoa. Yesu ni Mungu katika mwili wa binadamu (Yohana 1:1,14). Yesu ni Mungu, alikuja ulimwenguni kama mwanadamu wa kweli (1Yohana 4:2). Mungu alikuja akawa mwanadamu katika Yesu ili atuokoe. Hiyo yaleta swali lifuatalo: Ni kwa nini tunaitaji kuokolewa?
Yesu anawaokoa wale wote wanaopokea tuzo lake la wokovu. Yesu anawaokoa wale wote wanaomwamini katika dhabihu yake pekee kama fidia ya dhambi (Yohana 3:16; Matendo 16:31). Huku Yesu kama dhabihu ilikuwa kamilifu na yatosha kulipia dhambi zote za binadamu, Yesu pekee ndiye aweza kuokoa wale pekee wanaoipokea zawadi yake (Yohana 1:12)
Kama sasa unaelewa yamaanisha nini Yesu aokoa, na unataka kuweka imani kwake kama mwokozi wa maisha yako, akikisha kwamba unaelewa na kuamini yafuatayo, na kama hatua ya imani, nena maneno yafuatayo,
SALA YA TOBA
Inawezekana kabisa ya kuwa wewe unayesoma ujumbe huu hujaokoka - yaani hujampokea Yesu Kristo ndani ya moyo wako kama Bwana na Mwokozi wako. Lakini sasa umeona umuhimu wa kumpokea Yesu Kristo katika maisha yako.
Naamini Roho Mtakatifu ameweka fursa hii mikononi mwako kwa mpango maalum wa Mungu ili ufike mahali pa kutubu na kuokoka. Inawezekana kabisa, pia ya kuwa hujawahi kuambiwa juu ya umuhimu wa wewe kuokoka. Lakini napenda kukuambia ya kuwa ni mpango wa Mungu uokoke. Soma Wakolosai 1:13,14 na Yohana 1:12-14 na 1 Timotheo 2:3-6 na Warumi 1:16,17 na Yohana 3:7. Ni vigumu kuona baraka za Damu ya Yesu bila ya kuokoka.
Kwa hiyo kama unataka kuokoka - tafuta mahali palipo na utulivu, na usome kwa sauti sala ifuatayo: (ukiweza unaweza kupiga magoti unapoomba sala hii)
“Ee Mungu wangu ulie Mtakatifu. Ninakuja mbele zako. Mimi ni mwenye dhambi. Naomba unisamehe dhambi zangu zote nilizokukosea katika maisha yangu. Ninatubu kweli. Naomba damu ya Yesu Kristo iliyomwagika msalabani kwa ajili yangu initakase sasa katika roho yangu na nafsi yangu na mwili wangu.
Nimefungua moyo wangu. Bwana Yesu Kristo nakukaribisha ndani yangu. Ingia kwa uwezo wa Roho wako – uwe Bwana na Mwokozi wangu kuanzia sasa na siku zote. Ahsante kwa kunisamehe na kwa kuniokoa. Nimejitoa kwako nikutumikie katika siku zote za maisha yangu. Shetani hana mamlaka tena juu yangu katika jina la Yesu Kristo. Amina.
Ikiwa umesoma sala hii kwa kukusudia kabisa na kwa imani, basi wewe umeokoka na dhambi zako zimesamehewa na kusahauliwa na Mungu sawasawa na alivyoandika katika neno lake. Damu ya Yesu iko juu yako sasa.
Baada ya kuokoka
Unapoanza maisha haya mapya katika Yesu Kristo nakushauri mambo yafuatayo:
1.Zungumza na Mungu kwa maombi kila siku (Yohana 15:7)
2. Soma Neno la Mungu (Biblia) kila siku (Matendo ya Mitume 17:11)
3.Mruhusu Roho Mtakatifu akutawale (Wagalatia 5:16-25; Warumi 8:14-17)
4.Umtumaini Mungu kwa kila jambo katika maisha yako (1Petro 5:7; Zekaria 4:6)
5.Usiache kukusanyika na kushirikiana na wengine waliompokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wao kama wewe ili uimarike zaidi (Waebrania 10:25)
Ukipenda unaweza kuniandikia kwa anwani hii hapa chini juu ya uamuzi uliofikia leo wa kuokoka, ili tumshukuru Mungu pamoja, na tuzidi kukuombea; na pia, tukutumie maandiko mengine ya kukusaidia: maxshimbaministries@gmail.com
Max Shimba Ministries

UTHIBITISHO 12 KUWA ALLAH SIO MUNGU

Leo nitawapa Sababu 12 kwanini allah sio mungu.
1. ALLAH NI MUNGU ASIYE NA JINA KAMILI
Qr. 17 au surat Bani Israil 110 (Wana wa Israil)
Sema; muombeni (Mwenyenzi Mungu) kwa (jina la) Allah au muombeni (kwa jina la) Rahman. Kwa jina lolote mnalomwita (katika haya itafaa). Kwani ana majina mazuri mazuri………
2. ALLAH NI MUNGU MWENYE MAADUI AMBAO NI WAKRISTO NA WAYAHUDI
mungu wao ana maadui wake ambao ni wakristo na wayahudi
Qr. 4:51 na 57 (surat Al Maida)
Enyi mlioamini! Msiwafanye mayahudi na wakristo kuwa ni marafiki. Wao ni marafiki wao kwa wao. Na miongoni mwenu mwenye kufanya urafiki nao, basi huyo ni katika hao. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu wenye kudhulumu.
3. ALLAH NA WAISLAM WOTE KUINGIA JEHANNAM
Wafuasi wote wa Allah wanangojea moto wa jehanam kisha waokolewe waislam baadaye kutoka motoni
Qr. 19:70-72
Tena hakika sisi tunawajuwa vyema Zaidi wanaostahiki kuunguzwa humo Wala hapana yeyote katika nyinyi ila ni mwenye kuifikia.
Hiyo ni hukumu ya Mola wako mlezi ambayo lazima itimizwe. Kisha tutawaokoa wale waliomcha Mungu; na tutawaacha madhalimu humo hali wamepiga magoti motoni.
4. ALLAH ANAINGIA JEHANNAM WAKATI MUNGU WA BIBLIA HATA INGIA JEHANNAM
Allah wao ataionja jehanamu pia
Qr. 50 au Surat Qaf 30 (kuapa)
Siku tutakayoiambia Jahanamu, ‘Je! Umejaa?’ Nayo itasema ‘Je kuna ziada (zaidi? Naije tu!
Imesimuliwa na Anas kuwa: Mtume alisema watu watatupwa jahanamu, Naye Allah ataiuliza jahanamu akisema je umejaa nayo jahanamu itasema kwani kuna nyingine zaidi na ije tu? Mpaka Allah atakapo ingiza mguu wake nayo jahanamu itasema inatosha! Inatosha
5. ALLAH HANA UWEZO WA KUPONYA MAGONJWA WAKATI MUNGU WA BIBLIA ANAPONYA WAGONJWA!!
Kwanini Allah alipo mtuma Jibril kwenda kumuombea Muhammad ugonjwa uliosababishwa kula sumu, maombi yao hayakufanya kazi?
Ibn Sa'd Ukurasa wa 265
Aisha, Mke wa Mtume Muhammad alikuwa akisema, "Wakati Nabii wa Allah alipo kuwa anaumwa, Gibril alikuwa anamwombea kwa Allah kwa kusema haya "Katika Jina la Allah ambalo litakuponya kutoka kila magonjwa na maumivu na kutoka kila wenye ubaya nawe na kila wanakuombea ubaya, utapona..
Cha kushangaza, Allah na Jibril pamoja walishindwa kumponya Muhammad, huu sasa ni Ushahid tosha kuwa Allah hana uwezo wa kuponya bali ndie anaye tupia watu Magonjwa.
6. ALLAH NDIE HUWAPA WATU MAGONJWA

Contradictions in the Quran: A Theological and Textual Examination

Contradictions in the Quran: A Theological and Textual Examination By Dr. Maxwell Shimba, Shimba Theological Institute Introduction Muslims ...

TRENDING NOW