Monday, February 15, 2016

MUHAMMAD AWAAMRISHA WAISLAM KUNYWA MIKOJO YA NGAMIA

Ndugu msomaji,
Huu ni MSIBA mkubwa sana kwa Waislam na Mtume wa Muhammad. Leo, Muhamamd kawa Daktari na kudai kuwa eti, MKOJO WA NGAMIA NI DAWA.
Soma:
Kwa mujibu wa Muhammad, watu waliteswa kwenye makaburi yao kwa sababu ya kujichafua na mkojo [wao wenyewe]. Bukhari juzuu ya1 kitabu cha 4 sura ya57 na.215 uk.141; Bukhari juzuu ya 1 kitabu cha 4 sura ya 57 na.217 uk.142.
Hata hivyo Muhammad aliwaamuru baadhi ya watu kumfuata mchungaji wake na kunywa maziwa na mikojo ya ngamia. Bukhari juzuu ya 7 kitabu cha 71 sura ya 6 na.589, 590 uk.398, 399 na juzuu ya 7 kitabu cha 71 sura ya 29 na.623 uk.418.
Muhammad pia alisema kuwa mkojo wa ngamia ni dawa nzuri. Ibn-i-Majah juzuu ya 5 kitabu cha 31 na.3503 uk.38.
Baadhi ya Waislam waliambiwa kunywa mkojo wa ngamia, waliishia kuwa waasi na kumuua mchungaji. Muhammad aliamuru wakatwe miguu na mikono yao na macho yao yachomwe. Sunan Nasa’i juzuu ya 1 na.308-309 uk.255-256. Tazama pia Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 52 sura ya 152 na.261 uk.162.
Hivi huyu kweli alikuwa Mtume wa Mungu? Mbona hatusomi hata sehemu moja kuwa Muhamamd alitumia neno la Allah kutibu watu?
Mbona Allah anatumia Mikojo kutibu watu, kwani Allah hana uwezo wa kuponya kwa jina lake?
Mbona Muhammad na Allah hawakuponya watu kwa jina la ALLAH?
Kwanini Muhammad alipo kula nyama yenye sumu hakunywa MIKOJO ya Mgamia ili kujitibu?
Kumbe kunywa mikojo ya ngamia ilikuwa ni sehemu ya NDUMBA ya Muhammad.
Kumbe Mikojo ya Ngamia inawafanya watu wawe vichaa.
HUU NI MSIBA MKUBWA SANA.
Soma kituko kingine cha Muhammad.
Muhammad na Maji Safi
Udhibiti wa afya kwa kuondoa maji machafu na takataka (Sanitation): Watu walipomuliza kuhusu kunywa maji ya kwenye kisima chenye nguo za hedhi, mbwa waliokufa, na vitu vyenye kunuka, Muhammad alisema kuwa maji ni safi kabisa na huwa hayachafuliwi na kitu chochote. Abu Dawud juzuu ya 1 sura ya 35 na.66-67 uk.16-17.
Muhammad alikuwa Nabii wa uongo na sio Mungu.
Waislam nawakaribisha kwa Yesu Mungu Mkuu.
Max Shimba
For Max Shimba Ministries

Sunday, February 14, 2016

MUHAMAMD AMESEMA SHETANI ANAISHI KWENYE PUA ZA WAISLAM WOTE NA NZI WACHAFU NI DAWA.

1. ETI, SHETANI ANAISHI KWENYE PUA YAKO
2. ETI NZI WACHAFU NI DAWA

Ndugu msomaji,
Huu ni msiba:
1. ETI, SHETANI ANAISHI KWENYE PUA YAKO
Shetani Puani Mwako?
"Abu Huraira alisimulia: Nabii alisema, ‘Kama mtu yeyote kati yenu akiamka toka usingizini na kutawadha [kaida ya kujitakasa], anapaswa kuosha pua yake mara tatu kwa kuingiza maji na kuyatoa kwa kuhema kwa sababu Shetani alikuwa kwenye sehemu ya juu ya pua yake usiku mzima."(1) Maelezo ya mwenye kutafsiri (1) yanasema, "Tunapaswa kuamini kuwa ni kweli kwamba Shetani anakaa kwenye sehemu ya juu ya pua ya mtu hata kama hatuwezi kuelewa kwa sasa, kwani jambo hili linahusika na ulimwengu usioonekana ambao hatujui lolote kuhusiana nao isipokuwa yale ambayo Mwenyezi Mungu ametuambia kupitia Mtume wake." Bukhari sura ya 4 kitabu cha 54 (Mwanzo wa Uumbaji) sura ya 10 na.516 uk.328.
Huu nu uongo mkubwa sana ambao Muhammad amesema katika umma yake.
[Moja]: Shetani hana uwezo wa kuwa kila mahali kwa wakati mmoja [omnipresence]
[Mbili]: Shetani ni roho na hana geographical location katika mwili wa bindamu.
[Tatu]; Labda Shetani anaishi kwenye pua za Waislam pekee. Maana ukimpokea Yesu na kujazwa na Roho Mtakatifu, Shetani hawezi kuwa anaishi kwenye pua yako kama anavyo ishi kwenye pua za Waislam wote.
2. ETI NZI WACHAFU NI DAWA
Kumwamini Muhammad Wakati Nzi Wanakuwepo:
"Abu Huraira alisimulia: Nabii alisema, ‘Kama nzi ameangukia kwenye kinywaji cha mtu yoyote kati yenu, na amchovye (kwenye kinywaji), kwani bawa lake moja lina ugonjwa na lingine lina tiba ya huo ugonjwa." Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 54 (Mwanzo wa Uumbaji) sura ya 16 na.537 uk.338. Tazama pia Abu Dawud juzuu ya 3 kitabu cha 21 (Kitabu cha Vyakula) na.3835 uk.1080.
"Abu Huraira alisimulia: Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema, ‘Kama nzi ameangukia kwenye chombo cha yoyote kati yenu, mtu huyo na amchovye huyo nzi (kwenye chombo) kisha amtupe, kwani kwenye bawa lake moja kuna ugonjwa na kwenye lingine kuna uponyaji (1) (kiuasumu), yaani tiba ya ule ugonjwa." Bukhari juzuu ya 7 kitabu cha 71 (Kitabu cha Dawa) sura ya 58 na.673 uk.452-453.
Maelezo ya mwenye kutafsiri 

(1) yanasema, "Katika taaluma ya uganga inafahamika sana siku hizi kwamba nzi hubeba vijidudu vinavyosababisha magonjwa [pathogens] kwenye baadhi ya sehemu za mwili wake kama alivyosema Nabii (karibu miaka 1400 iliyopita wakati ambapo binadamu walikuwa na ufahamu mdogo sana wa uganga wa kisasa.) Vivyo hivyo, Mungu aliumba vumbe na namna za utendaji vinavyoua hivi vijidudu vyenye kusababisha magonjwa mf. Kuvu ya penicillin (penicillin Fungus) huua vijidudu kama Staphalococci na vinginevyo. Hivi karibuni majaribio yaliyofanywa chini ya usimamizi yameonyesha kuwa nzi hubeba ugonjwa (pathagens) pamoja na viuasumu vya vijidudu hivyo. Kwa kawaida nzi anapogusa chakula kinachomiminika huathiri kimiminika kwa vijidudu vyake, hivyo ni lazima kumchovya ili aweze kutoa viuasumu vya vijidudu hivyo kwa lengo la kusawazisha vijidudu hivyo. Kuhusiana na somo hili pia niliandika kwa rafiki yangu kupitia kwa Dr. Muhammad M. El-SAMAHY, mkuu wa idara ya hadithi ya Chuo Kikuu cha Al-Azhar CAIRO (Misri) ambaye ameandika makala kuhusu Hadithi hii na kuhusiana na taaluma ya uganga amesema kuwa wataalamu wa vijidudu vidogo (microbiologists) wamethibitisha kuwa kuna chembe chachu zenye kukata kwa urefu zinazoishi kama vimelea ndani ya tumbo la nzi na chembe hizi chachu hujichomoza kupitia mishipa ya kupumulia ya nzi na kama mtu akimchovya nzi kwenye kimiminika, chembe hizi hupasuka kwenye kimiminika na vitu vilivyomo kwenye chembe hizi ni viuasumu vya vijidudu ambavyo nzi huvibeba."
Karibu madaktari wote, kama si Waislam, hudhihaki wakisika kuhusu kumchovya nzi kwa makusudi kwenye kinyaji chako.
Mungu awabariki sana,
Katika Huduma Yake,
Max Shimba Ministries Org.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2015. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

UKWELI KUHUSU UUNGU WA YESU

JE’ BWANA YESU ANAPATAJE KUWA MUNGU?
Baada ya kujipatia maarifa makini juu ya nafsi tatu Mungu mmoja;

Ni vyema sasa tukapiga hatua nyingine ya ufahamu kwa kuangalia swali hili makini ambalo kwa kiasi kikubwa pia huchanganya hisia za watu wengi katika ulimwengu wa imani, ambapo kile kinachoonekana kuwachanganya watu wengi hapa ni uelewa juu ya ukweli kuhusu chimbuko la Uungu wa Bwana Yesu na hivyo watu wengi kuhoji kuwa Yesu anapataje sasa kuwa Mungu?.
Ni wazi kuwa swali hili hasa hulenga kutafut kujua asili au chimbuko la  mamlaka ya Kiuungu ya Yesu anayotajwa kuwa nayo hasa kutokana na kile kinachoonekana kuwa Bwana Yesu alikuwa na mwonekano unaoonyesha kuwa huenda naye alikuwa na asili au chimbuko la dunia hii.
Hivyo ili kupata majibu ya msingi ya hili ni vyema kwanza tuanze na hoja juu ya asili ya Yesu na ndipo tunaweza kufunguka zaidi kiufahamu na kuelewa mengi zaidi juu ukweli kuhusu Uungu wa Yesu.

Ufahamu juu ya asili ya Yesu
Kile kilichoongeza upinzani mkubwa wa Mafarisayo na baadhi ya Wayahudi juu ya Uungu wa Yesu ni uelewa usiyo sahihi juu ya asili ya Yesu.
Ufahamu wa wengi kati ya Wayahudi uligotea katika dhana ya mwonekano wa ubinadamu wa Yesu na historia yake ya uzazi wa kidunia toka katika tumbo la Mariam, ambapo kama matokeo ya hili Wayahudi walisikika wakati fulani wakitamka:-

Yahana 6:42
Wakasema, Je! Huyu siye Yesu, mwana wa Yusufu, ambaye twamjua babaye na mamaye? Sasa asemaje huyu, Nimeshuka kutoka mbinguni?

Unaweza sasa kupata pichani  juu ya mzizi wa hoja hii, na ni kama tunavyoona katika nukuu hiyo ya kitabu cha Yohana kuwa hoja kuu ya Wayahudi ilikuwa ni kile walichoona kuwa haikuwa sahihi kwa Yesu kusema ameshuka toka mbinguni maana kile wao wanachojua ni kuwa alizaliwa na bi’Mariam na baba yake ni Yusufu kwahivyo asili yake ni duniani tu. 
Hivyo kwa hali hiyo iliwapa ugumu kukubali pale Yesu alipojitaja kuwa na asili ya mbinguni na kimsingi ndicho kilichokuwa chanzo kikubwa cha upinzani wao dhidi ya matamko ya Yesu.
Habu ona tena hoja ya Wayahudi pale Yesu alipoeleza uwepo wake wa milele’

Yohana 8: 56-58 

Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi.57 Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu? 58 Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.

Katika andiko hilo tena Wayahudi walipingana na Yesu kutokana na tamko lake lililoonyesha uhusiano wake na ukaribu na mzee Ibrahimu, kitendo ambacho kilifanya Wayahudi hao kumhoji kwa madai kuwa yeye ni kijana mdogo hasiyepata hata miaka hamsini anawezaje kuwa amemwona Ibrahimu?, na ndipo Yesu anajibu na kuwaambia bayana kuwa uwepo wake ni wa kabla ya Ibrahimu’ 58 Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.
Hivyo kwa mtazamo wangu binafsi ninaona kuwa tatizo la Wayahudi au wale wanaopinga Uungu wa Yesu kwasababu ya ubinadamu alokuwa nao au sababu ya kuzaliwa na Mariam tatizo lao kuu si hilo bali zaidi ni kutolewa kabisa msingi mzima wa asili ya Yesu kabla ya kuzaliwa kwake na Mariam.
Je’ Asili ya Yesu ni wapi?
Katika kujibu swali hili Bwana Yesu mwenyewe mara kadhaa aliwaelimisha Wayahudi juu ya ukweli kuhusu asili yake ili kuwasaidia kuondokana na dhana au mtazamo wa kumchukulia kama mtu mwenye asili ya kidunia na badala yake alitaka waone kuwa yeye alikuwako kabla ya kuja duniani kama mwanadamu kwa kusudi la ukombozi wa watu. Soma kwa makini maandiko haya:-

Yohana 8:23

Saturday, February 13, 2016

MUHAMMAD ALIKUWA ANAWAPIGA WAKE ZAKE - AISHA NA HAFSA

Ndugu msomaji,

Muhammad alikuwa na tabia ya kuwapiga wake zake, hususan Aisha na Hafsa.

SOMA KISA HIKI HAPA CHINI.

Sahih Muslim #2127:

Ilipokuwa zamu yangu kwa Nabii wa Allah kuwa nami usiku, aliingia na kugeuka, akavua joho lake na viatu vyake, na kuviweka karibu na miguu yake, na akajilaza kwenye kitanda mpaka alipo fikiria kuwa na mimi nimelala.

Basi akachukua joho lake taratiibu na kuvaa viatu vyake, na akafungua mlango na kutoka nje na kuufunga taratibu. Aisha akasema, na mimi nikajifunika kichwa changu, na kuvaa hijabu yangu na kujifunga nguo kiunoni mwangu, na baadae nikatoka nje na kumfuta Nabii wa Allah mpaka alipo fika Baqi.

Alisimama pale kwa muda mrefu. Na baadae akanyanyu mikono yake mara tatu, na baadae kurudi, na mimi vile vile nikarudi nyumbani. Alikuwa anatembea kwa haraka haraka, na mimi vile vile nilitembea kwa haraka haraka. Alikimbia, na mimi nikakimbia vile vile. Akaja nyumbani na mimi vile vile nilikwenda nyumbani, ingawa mimi nilkwenda kwa haraka kabla yake. Nilipo ingia tu na kujilaza kitandani, na Nabii wa Allah akaingia nyumbani, akasema: Hii ni nini, O' Aisha, mbona unahema sana? Nikamwambia, hakuna kitu. Akasema, Niambie au una mambo ya siri hautaki kuniambia.

Nikamwabia, Nabii wa Allah, baba na mama yangu wawe fidia kwako, halafu nikamwambia kila kitu bila kumficha kitu. Muhammad akasema, kumbe nilicho kuwa nakiona kwenye giza mbele yangu ilikuwa ni wewe? Nikamjibu, NDIO. Basi Nabii wa Allah, AKANIPIGA KWA NGUVU SANA KWENYE KIFUA CHANGU, na nilipatwa na maumivu makali sana. HALAFU AKASEMA, unafikiri Allah na Nabii wake wamekuonea?


Bukhari volume 8, #828

Amesema Aisha: Abu Bakr alikuja kwangu na akanipiga ngumi kwa nguvu sana na kusema, umewaweka watu kizuizini kwasababu ya mkufu wako. Lakini nilikuwa nimekaa kimya kama vile nimekufa, .......

Jamani, eti huyu ndie Nabii wa Allah. Hana jema zaidi ya kupiga wake zake, kisa, mke mtu kamfuata Baqi. Je, kama Muhmmad alicho kuwa anafanya ni jambo jema, kwanini aliondoka nyumbani kwake kimya kimya?

Kama kweli Muhammad hakwenda kufanya NDUMBA, kwanini alichukia pale alipo ambiwa kuwa Aisha na yeye alikuwa Baqi?

Hivi, kwanini MUHAMMAD ALIKUWA ANAPIGA WAKE ZAKE?

Hakika huyu hakuwa Nabii wa Mungu bali Allah mpinga Mungu.

Leo tumejifunza tena kuwa, kumbe katika Uislam, wanaruhusikwa kuwapiga wake zao. Huu ni MSIBA.

Max Shimba

For Max Shimba Ministries Org

Friday, February 12, 2016

QURAN INASEMA NINI KUHUSU YESU?



A. YAKIRI KUWA YESU NI MUNGU
B. YAKIRI KUWA YESU HANA DHAMBI
C. YAKIRI KUWA YESU ATAHUKUMU ULIMWENGU
D. YAKIRI KUWA YESU NI NENO LA MUNGU
Yafuatayo ni maswali amabyo Waislam wengi wamekuwa wakijiuliza, hivi Yesu ni nani kwenye Quran yao?
1. Yesu ni binadamu pekee aliye zaliwa kupitia Bikira na bila ya Baba wa kidunia. Hii ni sifa ya kipee ambayo hakuna Mtume au Nabii aliye nayo. 21. (Malaika) akasema: Ndio hivyo hivyo! Mola wako Mlezi amesema: Haya ni mepesi kwangu! Na ili tumfanye kuwa ni Ishara kwa watu, na Rehema itokayo kwetu, na hilo ni jambo lilio kwisha hukumiwa. 22. Basi akachukua mimba yake, na akaondoka nayo mpaka mahali pa mbali.
2. Masia Yesu ni tofauti na binadamu wote kwasababu yeye anaitwa “Kalimatullah” (NENO LA ALLAH)
Masia, Isa mtoto wa Maryam, Nabii wa Allah na Neno lake” (Sura The Women 171; Sura al Imran 40).
3. Isa alizaliwa kutokana na Roho ya Allah; kwa sababu hii, hakuhitaji Baba wa kidunia.
Masia, Isa Mwana wa Maryam, Nabii wa Allah na Neno Lake ni Roho kutoka kwa Mungu..
(Sura The Women 169).
4. Isa ni motto pekee aliye weza kusema akiwa mchanga Only Isa spoke while in the cradle
30. (Mtoto) akasema: Hakika mimi ni mtumwa wa Mwenyezi Mungu. Amenipa Kitabu, na amenifanya Nabii.
(Sura Miriam 19:30)
Zaidi ya hapo, Isa hakuitaji mtu yeyote yule kumfudisha kusoma wala kuandika.
13Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya BWANA, au kumfundisha kama mshauri wake? 14Ni nani ambaye BWANA ametaka shauri kwake ili kumwelimisha, naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa? Ni nani aliyemfundisha maarifa au kumwonyesha mapito ya ufahamu?
(Isaiah 40:1,13-14)
5. Isa alikuwa ni Nabii thabiti na hakuwa na dhambi au kosa lolote lile. Mitume wote walitenda dhambi, na dhambi zao zimesemwa kwenye Quran na Taurat. Isa hakuwa na dhambi.
45. Na pale Malaika walipo sema: Ewe Maryamu! Hakika Mwenyezi Mungu anakubashiria (mwana) kwa neno litokalo kwake. Jina lake ni Masihi Isa mwana wa Maryamu, mwenye hishima katika dunia na Akhera, na miongoni mwa walio karibishwa (kwa Mwenyezi Mungu). (Sura al Imran 45)
Vivle vile Al-Bukhari amefundisha kuwa Isa bin Maryam alikuwa ni mtu dhabiti na asiye an dhambi:
Shetani aligusa kila kiumbe wakati wa kuzaliwa kwake, ISIPOKUWA Yesu, Mtoto wa Maryam; Shetani alipo jaribu kumgusa alishindwa (Hadith of Sahih Bukhari Vol 4, Book 54)
6. Yesu hakuwa kama watu wengine, kwasababu Yesu aliweza kuumba Uhai kama Allah
49. Na ni Mtume kwa Wana wa Israili kuwaambia: Mimi nimekujieni na Ishara kutoka kwa Mola Mlezi wenu, ya kwamba nakuundieni kwa udongo kama sura ya ndege. Kisha nampuliza anakuwa ndege kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na ninawaponesha vipofu wa tangu kuzaliwa na wakoma, na ninawafufua maiti kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, na ninakwambieni mnacho kila na mnacho weka akiba katika nyumba zenu. Hakika katika haya ipo Ishara kwenu ikiwi nyinyi ni wenye kuamini.
(Sura al Imran 49)
7. Isa ni nabii pekee aliye weza kujua siri iliyo ndani ya nyoyo za watu.
49. Na ni Mtume kwa Wana wa Israili kuwaambia: Mimi nimekujieni na Ishara kutoka kwa Mola Mlezi wenu, ya kwamba nakuundieni kwa udongo kama sura ya ndege. Kisha nampuliza anakuwa ndege kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na ninawaponesha vipofu wa tangu kuzaliwa na wakoma, na ninawafufua maiti kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, na ninakwambieni mnacho kila na mnacho weka akiba katika nyumba zenu. Hakika katika haya ipo Ishara kwenu ikiwi nyinyi ni wenye kuamini.
. (Sura Al Imran 48)
8. Isa alifanya miujiza mikubwa mikubwa zaidi ya binadamu wote
Na ninawaponesha vipofu wa tangu kuzaliwa na wakoma …
(Sura Al Imran 48)
9. Isa alifufua watu kwa kutumia NENO
na ninawafufua maiti …
(Sura al Imran 48 & Sura The Table 110)
10. Isa ndie binadamu pekee aliye itwa Masiha “the Masih”
Masia, Isa Mwana wa Maryam, alikuwa Nabii wa Allah na Neno Litokalo kwake …
(Sura The Women 169)
Katika Taurat tunajifunza kuhusu asili hasili ya Masia:
5BWANA asema, “siku zinakuja, nitakapomwinulia Daudi Tawi lenye haki, Mfalme atakayetawala kwa hekima na kutenda lililo haki na sawa katika nchi. 6Katika siku zake, Yuda ataokolewa na Israeli ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa kwalo: BWANA Haki Yetu..
(Jeremiah 23:5-6)
11. Isa aligawana Mamlaka na Mungu
117. Sikuwaambia lolote ila uliyo niamrisha, nayo ni: Muabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi. Na mimi nilikuwa shahidi juu yao nilipo kuwa nao. Na ulipo nifisha ukawa Wewe ndiye Muangalizi juu yao. Na Wewe ni shahidi juu ya kila kitu
(Sura The Table 117)
12. Isa alikuwa ni Ishara ya Baraka kutoka kwa Allah
(Sura Miriam 20)
13. Isa alitoka ahadi ya maisha wakati wa siku ya ufufuo.
55. Pale Mwenyezi Mungu alipo sema: Ewe Isa! Mimi nitakufisha, na nitakunyanyua kwangu, na nitakutakasa na wale walio kufuru, na nitawaweka wale walio kufuata juu ya wale walio kufuru, mpaka Siku ya Kiyama. Kisha marejeo yenu yatakuwa kwangu, nikuhukumuni katika yale mliyo kuwa mkikhitalifiana
(Sura al Imran 55)
14. Isa atatoa hukumu kwa viumbe vyote;
El-Bukhari anasema kuwa:
Katika saa ya Mwisho, Isa Mwana wa Maryam atarudi na kuhukumu ulimwengu.
Leo nimekuonyesha kwa ushahid wa Quran na vitabu vya kiislam kuwa, hata Isa wao alifanya miujiza zaidi ya Allah na Mtume wake Muhammad.
Max Shimba Minsitries.

YESU ANAKIRI KWA MDOMO WAKE KUWA YEYE NI MUNGU. (SEHEMU YA PILI)

Ndugu Msomaji,
Leo nitaleta ushahidI zaidi wa Yesu akisema kwa mdomo wake kuwa yeye ni Mungu.
Waislam wamekuwa na tabia ya kusema na kuuliza, wapi Yesu kasema "Mimi Yesu ni Mungu" . Waislam wanasisitiza kuwa, lazima wapewe aya yenye maneno hayo. Leo kwa mara nyingine tena nitawapa aya ambayo Yesu anasema YEYE NI MUNGU.
YESU ANAJARIBIWA NA SHETANI.
Kwenye aya hapa chini, utasoma kuhusu Ibilisi alivyo mchukua Yesu na kwenda kumjaribu. SASA SOMA:
Mathayo 4: 5 Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu, 6 akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.
Kwenye hizo aya hapo juu, tumesoma kuwa Ibilisi anamjaribu Yesu, Ibilisi anasema kwa Yesu kuwa, ajitupe kutoka juu ya kinara, hilo lilikuwa ni jaribu la Ibilisi kwa Yesu. Ibilisi alitaka kuona kama Yesu atamsikiliza na kutenda hayo. Ingawa Yesu angewaza kujitupa kutoka huo mnara na kuwaamuru Malaika wake wangemchukua kutoka mikononi mwao, lakini KAMA ANGEFANYA HIVYO, basi angekuwa ametenda matakwa ya Shetani na kufuata maamrisho ya Shetani.
SASA SOMA NINI YESU ALIMJIBU SHETANI HAPA CHINI,
Mathayo 4: 7 Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.
YESU ANATOA JIBU AMBALO WENGI WENU HAMKUWAI LIFIKIRIA.
1. Kumbuka Ibilisi alikuwa anamjaribu Yesu.
2. Kumbuka kuwa katika hayo majaribu, walio kuwepo ni (a) Mjaribu ambaye ni Ibilisi na (b) Mjaribiwa ambaye ni Yesu.
SASA BASI, MJARIBIWA AMBAYE NI YESU ANAMJIBU MJARIBU-SHETANI KUWA USIMJARIBU BWANA MUNGU WAKO.
Maswali ya kujiuliza:
1. Kwanini Yesu alisema usimjaribu Bwana Mungu wako, huku tukifahamu kuwa anaye Jaribiwa ni Yesu?
2. Kwanini Ibilisi hakupinga madai ya Yesu kujiita "BWANA MUNGU", huku Ibilisi akifahamu kuwa anaye mjaribu ni Yesu?
3. Kwanini Yesu hakukataa kuitwa Mwana wa Mungu katika aya ya 6?
4. Kwanini Ibilisi alimuita Yesu Mwana wa Mungu?
MJARIBIWA AMBAYE NI YESU, ANAMWAMBIA MJARIBU-SHETANI kuwa USIMJARIBU BWANA MUNGU WAKO?
Kwanini Yesu anaye jaribiwa na Shetani alisema umsimjaribu "BWANA MUNGU" na hakusema kuwa usinijaribu mimi Yesu?
Nivigumu sana kupinga Uungu wa Yesu, maana hata Shetani aliye kuwepo zama kwa zama, anakiri kuwa Yesu ni Mungu , na zaidi ya hapo, anamuita Yesu kuwa ni Mwana wa Mungu "aya ya 6". Kwanini SHETANI HAKUMSHTAKI YESU kwa kujiita BWANA MUNGU?
Leo kwa mara nyingine tena nimejibu swali, wapi ilipo aya ambayo Yesu anasema yeye ni Mungu. Sasa swali langu kwa WAISLAM, je mpo teyari kumpokea Yesu aliye sema yeye ni Mungu?
SASA, nawakaribisha mje tujadili hii mada kwa utulivu na kwa kutumia aya za Biblia tu. Maana hicho ndicho kitabu pekee cha Mungu.
YESU KASEMA KUWA YEYE "BWANA MUNGU"
Mungu awabariki sana.
Max Shimba
For Max Shimba Ministries

SIUTAKI UISLAM KWASABABU UNARUHUSU KULA FISI NA MIJUSI


==================================================
Sayyidina Ibn Ammar (RA) alisema kuwa, siku moja alimuuliza Jabir Jbn Abdullah (RA) kuhusu uwindaji wa FISI. Alinijibu na kusema, inaruhusiwa kuwinda Fisi. Nilimuuliza, Je, tunaruhusiwa kula, na akanijibu kuwa Kula Fisi ni Halal (Inaruhusiwa kula Fisi).
Nikamuuliza tena, Je, Nabii wa Allah(SAW) aliruhusu kula Fisi? Jabir r alinijibu na kusema. NDIO, Nabii wa Allah aliruhusu kula Fisi.
[Abu Dawud 3801, T 1798, Ibn e Majah 3085, Ahmedl4456]
9- Kitabu cha HAJJ
MTUME MUHAMMAD ASEMA KULA NYAMA YA MIJUSI NI HALALSahih Muslim Kitabu 21, 4788 Idadi :
Ibn 'Umar taarifa kwamba kulikuwa na baadhi ya watu na Mtume wa Allah (amani iwe juu yake) miongoni mwa maswahaba wake alikuwepo Sad. Basi ililetwa nyama ya Mjusi na mwanamke miongoni mwa wake wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (amani iwe juu yake) alisema: Ni nyama ya mjusi. Hapo Nabii Muhammad alisema: Kuleni hiyo nyama ya Mjusi kwa kuwa ni halali…
Eti kula Nguruwe ni haram lakini wanakula Fisi na Mijusi
Karibu kwa Yesu aliye hai na Mungu Mkuu,
Mungu awabariki sana,
Katika Huduma Yake,
Max Shimba Ministries Org.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2015. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

UTHIBITISHO 10 KUWA YESU NI MUNGU

“Wahubiri wa injili” wa Kiislamu huwa wanapinga kuwa Yesu ni Mungu na unapowakatalia wanakwambia, “Lete andiko.”
Maandiko yapo mengi sana ndani ya Biblia juu ya ukweli kwamba Yesu ni Mungu. Ni mengi mno!
Ukishawapa andiko, wanabadilika na kusema, “Nataka maneno aliyoongea Yesu mwenyewe.” Kwa madai haya hata kwenye Qurana hawawezi thibitisha kuwa Allah Allah ni mungu, zaidi ya hapo, hata Utume wa Muhammad unakuwa kwenye njia panda, maana hakuna aya kwenye Quran Muhammad anasema mimi Muhammad ni mtume wa Mungu.
Hiki ni kigezo POTOFU na si cha kibiblia hata kidogo. Ukweli ni kwamba, Biblia YOTE ni Neno la Mungu. Haijalishi amezungumza Musa, Isaya, Yohana, Petro au Yesu mwenyewe. Imeandikwa:
Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu. (2Petro 1:21).
Hivyo, kudai kwao eti, “Nataka maneno aliyosema Yesu mwenyewe,” ni kigezo batili na kisicho na mantiki hata kidogo.
1. YESU ALIKUWEPO KABLA YA KUZALIWAUfuatao ni ushahidi wa kibiblia kwamba YESU KRISTO ni Mungu.
Yohana 8:58
Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye IBRAHIMU ASIJAKUWAKO, MIMI NIKO.
NIKO ni jina la Mungu peke yake. Tunakutana na jina hilo pale Musa alipoongea na Mungu na kutumwa kuwakomboa wana wa Israeli kutoka Misri. Imeandikwa:
Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n'nani? Niwaambie nini? Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO (Kutoka 3:13-14).
Mwanadamu yuko kwa sababu Mungu alisababisha awepo. Gari liko kwa sababu injinia au mbunifu alisababisha liwepo. Nyumba ipo kwa sababu fundi alisababisha iwepo. Lakini Mungu YEYE YUKO TU!! Hayupo kwa kusababishwa na yeyote! Ndiyo maana akasema MIMI NIKO AMBAYE NIKO! Yesu ni NIKO. Kwa hiyo, Yeye ni Mungu.
2. YESU NA BABA NI WAMOJAYohana 10:30
Mimi na Baba tu umoja.
Waislamu wana msemo wao kwamba eti, Yesu na Mungu ni wamoja katika malengo, si katika asili yao. Basi huwa nawauliza swali kuhusu aya ifuatayo ya Isaya, nao wanazimika na kukosa jibu:
Isaya 9:6
Maana kwa ajili yetu MTOTO amezaliwa, Tumepewa MTOTO MWANAMUME; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, MUNGU MWENYE NGUVU, BABA WA MILELE, Mfalme wa amani.
Aya hii iko wazi kabisa. anayetajwa ni Yesu kwamba Yeye ni Mungu mwenye nguvu.
Yohana 14:9
Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? ALIYENIONA MIMI AMEMWONA BABA; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba?
Maneno haya Yesu aliyasema baada ya kuulizwa swali lililo wazi kabisa, ambalo lilikuwa na lengo la kumjua MUNGU BABA! Imeandikwa: Filipo akamwambia, Bwana, UTUONYESHE BABA, yatutosha. Ndipo Yesu akajibu waziwazi: ALIYENIONA MIMI AMEMWONA BABA. Maana yake ni kuwa, “Mimi ndio Baba mwenyewe.”
3. YESU NI MWANZO NA MWISHOUfunuo 1:17 na Ufunuo 22:13
Mimi ni wa kwanza na wa mwisho
Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.
Ni Mungu TU ndiye mwenye uwezo wa kuwa wa kwanza na wa mwisho; Yesu ni Alfa na Omega. Kwa hiyo Yeye ni Mungu.
4. YESU NI NENOYohana 1:1
Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye NENO ALIKUWA MUNGU.
Andiko hili Waislamu hawalipendi kabisa. ni kwa sababu liko wazi mno. Yesu ni Neno; na Neno ni Mungu; hivyo, Yesu ni Mungu!
5. THOMASO AKIRI KUWA YESU NI MUNGU, NA YESU HAKUKATAA KUITWA MUNGUYohana 20:28
Tomaso akajibu, akamwambia, BWANA WANGU NA MUNGU WANGU!
Tomaso aliposema hivi, Bwana Yesu hakukanusha na kusema, “Mimi sio Mungu.” Badala yake: Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa umeniona, umesadiki; wa heri wale wasioona, wakasadiki. (Yoh 20:29).
Kama Thomaso alikuwa muongo, kwanini Yesu hakukataa kuitwa Mungu. Imani zote zinakiri kuwa Yesu hakufanya dhambi na hakuwa na dhambi.
6. DAMU YA YESU INAMAMLAKAMatendo 20:28
Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake MUNGU, ALILOLINUNUA KWA DAMU YAKE MWENYEWE.
Ni Mungu gani mwenye damu huyu? Jibu liko wazi. Huyu ni Yesu Kristo. Huyu ndiye aliyetoa uhai wake na kumwaga damu yake msalabani; na hapo ndipo alipoanzisha Kanisa.
7. KATIKA YESU, KILA KITU KILIUMBWAWakolosai 1:16
Kwa kuwa KATIKA YEYE VITU VYOTE VILIUMBWA, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake.
Katika Yeye Yesu vitu vyote viliumbwa. Ina maana kuwa vitu vyote vilitokana na Yesu; maana Yesu ni Neno la Mungu. Na tunajua kuwa Muumba wa vitu vyote ni Mungu; hivyo, Yesu ni Muumba – Yeye ni Mungu!!
8. KATIKA YESU, UNAKAA UTIMILIFU WA MUNGUWakolosai 2:9
Maana KATIKA YEYE UNAKAA UTIMILIFU WOTE WA MUNGU, kwa jinsi ya kimwili.
Sisi sote ni watu wasio wakamilifu. Tunaanguka tena na tena kwenye dhambi. Kwa hiyo, hakuna mwanadamu wa kawaida ambaye anaweza kujigamba kwamba yeye ametimia kama alivyo Mungu. Lakini katika Yesu “utimilifu WOTE wa Mungu unakaa.” Kwa nini? Kwa sababu Yeye ndiye Mungu huyohuyo.
9. YESU NI MUNGU PAMOJA NASI "EMMANUEL"1Timotheo 3:16
Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. MUNGU ALIDHIHIRISHWA KATIKA MWILI, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu.
Ni Mungu gani aliyedhihirishwa katika mwili? Jibu liko wazi. Ni Yesu Kristo peke yake.
10. YESU NI MUNGU MKUU NA MWOKOZI WETUTito 2:13
….tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa KRISTO YESU, MUNGU MKUU NA MWOKOZI WETU
Yesu Kristo ni Mungu Mkuu!!
Shida KUU ya Waislamu ni hii: Wanampima Mungu kwa vigezo vya kibinadamu. Mungu anasema: Tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa wote wenye mwili; je! Kuna neno gumu lo lote nisiloliweza? (Yer 32:27)
Jibu liko wazo. HAKUNA!
Lakini utakuta Waislamu wanauliza maswali ya ajabu sana. Eti, kama Yesu ni Mungu, wakati amekufa, nani alikuwa anaangalia dunia?
Hili ni swali linalofaa kuulizwa juu ya kiumbe. Kama tungesema kuwa mwanadamu fulani alikuwa amekufa, ndipo kuna mantiki kuuliza kwamba, wakati amekufa nani alikuwa anatunza familia yake? Maana hili ni swali linalohusu tabia za kibinadamu kwa kuwa mwanadamu hawezi kuwa mahali kuwili au zaidi kwa pamoja. MUNGU SI MWANADAMU! ANAWEZA YOTE – NA HASA MUNGU WA IBRAHIMU, ISAKA NA YAKOBO!
YESU NI MUNGU MILELE NA MILELE!!
HALELUYA!!
Tafakari
Hoji mambo
Chukua hatua!

Thursday, February 11, 2016

ALLAH KUPITIA MUHAMMAD AMEHARIMISHA KUVAA PETE YENYE DHAHABU


Ndugu msomaji,
Kuharamishwa uvaaji wa dhahabu kwa wanaume kumethibiti katika hadithi nyingi sahihi zilizopokelewa kutika kwa Mtume wa Allah –Rehema na Amani zimshukie.
Amepokea (riwaya) Imamu Bukhaariy, Muislam na Ahmad kwamba Mtume wa Allah “Amekataza (kuvaa) pete ya dhahabu”.
Imepokelewa kutoka kawa Ibn Abbaas-Allah awawiye radhi-kwamba Mtume wa Allah aliiona pete ya dhahabu kidoleni mwa mtu, akamvua na kuitupa (huku) akisema
“ Mmoja wenu analikusudia kaa la moto na kulivaa mkononi?” Mtu yule akaambiwa baada ya kwenda zake mtume “ Itwae pete yako unufaike nayo. Akawajibu Wallah hapana, kamwe sitaichukua ikiwa aliyeitupa ni Mtume wa Allah –Rehema na Amani zimshukie.” Muislam
Na katika jumla ya riwaya zilizopokelewa kwamba Mtume wa Allah –Rehema na Amani zimshukie amesema : “ Ye yote mwenye kumuamini Allah na siku ya mwisho basi asivae hariri wala dhahabu.” Al-musnad {Musnadul–Imam Ahmad}
Huu ni msiba kwa Waislam. Maana siku hizi hawa Waislam wanavaa nguo za harirti pamoja na pete ya dhabu. Ona picha ya Usma Bin Laden na yeye amevaa pete ya dhabu. Astgahfurillah.

Max Shimba Ministries Org

UHUSIANO NA KUFANANA KATI YA WASABATO NA MASHAHIDI WA YEHOVA

Wasabato "SDA" na Mashahidi wa Yehova wote wawili walianzia katika muamko ulio kuwa katika miaka ya 1800 ambao msingi wake ulikuwa ni unabii wa Miller. Mafundisho yao yalianzia kutoka kwenye huu utabiri wa Miller na unafanana katika mambo mengi.
Huu muamko ulianza kupitia utabiri wa kifalme katika mwaka wa 1844, na ulikuwa na waamini wachache sana, ambao wengi wao walitoka katika Makanisa ya Kiroho baada ya kufukuzwa huko kwa sababu ya kufuata utabiri wa Miller.
Baada ya kufukuzwa, walianza kufikiri jinsi ya kuazisha kanisa au mkusanyiko, ingawa hawakuwa na "Mfumo wa hilo kanisa", lakini walipata muamko mkubwa zaidia baada ya kupa ujumbe mwengine uliandikwa na Ellen G. White. Barua hii ya Ellen G. White ndio iliyo anzisha kanisa la Wasabato, na Mwaka 1860 ndio jina la "Seventh Day Adventist" lilichaguliwa na kuwa na kanisa la kwanza.
Mafundisho mengi ya MSINGI ya Wasabato ni yaleyale ambayo yanafundishwa na Mashahidi wa Yehova. Tofauti kubwa ni ile ya Wasabato kuamini kuwa Jumamosi ndio siku pekee ya kuabudu, wakati Mashahidi wa Yehova wao hawashikirii hiyo siku kuwa ni ya muhimu sana.
Wote hao wawili Wasabato na Mashahdi wa Yehova wanakata kushiri Vita ikiwa nchi ipo kwenye matatizo, ingawa wanakubali kufanya kazi za kijeshi ambazo sio za kivita, kama ambavyo Mashahdi wa Yehova walivyo goma kwenda kwenye Vita Kuu ya kwanza ya dunia.
KIFO: Wanaamini kuwa mtu "mwili, roho na nafsi" akifa basi hubakia kwenye kaburi.
Mwanzo 2: 1 Basi mbingu na nchi zikamalizika, na jeshi lake lote.
2 Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya. 3 Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya.
Ingawa, hakuna aya hata moja kwenye Biblia inayo sema Mungu alimwambia Adama aitunze siku ya Saba" SABATO" kila wiki. Lakini Wasabato wanashikiria kuwa hiyo ndio siku halali ya kusali.
1. Je, Adam alikuwa anafanya na au tenda dhambi kwa kutoa itunza Sabato?
2. Je, baba wa Imani, Ibrahimu, alikuwa anatenda dhambi kwa kuto itunza Sabato, ingawa hakuambiwa afanye hivyo?
3. Je, wana wa Israel walipo kuwa Misri, walikuwa watenda dhambi, maana sheria ya kutunza Sabato ilikuwa bado hawana?
YESU NI MALAIKA MIKAELI
Wote, Wasabato na Mashahidi wa Yehova wanaamini kuwa Yesu Kristo ndie Malaika Mkuu Mikaeli. Ingawa hakuna aya hata moja inayo sema hivyo.
ROHO MTAKATIFU
Wote, SDA-WASABATO na Mashahidi wa Yehova hawaamini kuwa Roho Mtakatifu ni Mungu. Mashahidi wa Yehova wanaami kuwa Roho Mtakatifu ni kama NISHATI FULANI,
Ellen G. White yeye anasema kuwa Roho Mtakatifu ni nguvu fulani ya Mungu, lakini amekataa kusema kuwa Roho Mtakatifu ni "Person" -mtu./Mungu kamili kama alivyo Baba yetu aliye Mbinguni na ana adhama/attributes zote za Mungu
KIFO NI KULALA KWA NAFSI
Wote, Wasabato na Mashahidi wa Yehova wanaamini kuwa kifo ni kulala kwa nafsi kaburini na hubakia kaburini mpaka siku ya kiyama.
JEHANNAM
SDA-Wasbato wanaamini kuwa kuna Jehannam lakini wenda dhambi hawata kaa huko milele bali kwa muda tu, huku Mashahidi wa Yehowa wanaamini kuwa Jehannam itawaangamiza watu mara moja, na hawato kuwepo tena.
Mahusiano yao mengini ni kuwa, Mwanzilishi wa Mashahidi wa Yehova Charles Taze Russell, aliingiza mafundisho ya Wasabato kuhusu siku ya mwisho. Wakati Russell alipo kuwa na miaka 23 alifundishwa mafundisho ya Nelson H. Barbour ambaye ni Msabato na kwamba Yesu atarudi bila ya kuonekana mwaka 1874, ingawa Msabato William Miller alidai hapo nyuma kuwa Yesu atarudi kwa mara ya pili mwaka wa 1843.
Wote wawili Russell na Barbour wanaamini kuwa Yesu alirudi bila ya kuoneka mwaka wa 1874 na kwamba katika "Spring" ya mwaka 1878 kutatokea kunyakuliwa kwa Kanisa. Kunyakuliwa kwa Kanisa kulipo shindikana kutokea, Barbour alikuja na utabiri mwengine "new light" na mafundisho mengine mengi kusaidia ujumbe wake, lakini Russell alikataa kuyakubali.
Russell ndio akajitoa kutoa Kanisa la SDA-WASABATO ambalo ndio lilianzishwa na Ellen G. White. Ilipo fika mwaka wa 1874 Russell alianzisha kikundi kinacho itwa Wanafunzi wa Biblia. Na Julai ya 1879 Russell alichapisha jarida la Watch Tower and Herald of Christ's Presence. Mwaka 1882 Russell alikana UTATU wa Mungu, na ilipo fika 1916 Russell alifariki.
Leo tumejifunza kuhusu kushabihana na kufanana kwa hawa wawili, Mashahidi wa Yehova na SDA- Wasabato. Wote hawa walianzia katika vuguvugu la mwaka wa
Mungu awabariki sana,
Max Shimba
For Max Shimba Ministries Org.

Ancient Jewish Wedding Ceremony: “No man knows the day or hour, only the Father”

  The Ancient Jewish Marriage Rite: A Detailed Exposition of Betrothal, Preparation, and Consummation Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological ...

TRENDING NOW