Saturday, August 13, 2016

WAISLAM THIBITISHENI UWEPO WA ISA BIN MARYAM KWA VITABU VILIVYOKUWEPO KABLA YA QURAN NA KUZALIWA KWA MUHAMMAD

NDIO MAANA NAENDELEA KUSEMA KUWA, UISLAM NI DINI YA KUJITUNGIA, HAIKUWEPO WAKATI WA ADAM WALA MUSA WALA IBRAHIM
UISLAM NI FAKE [BANDIA]
Ndugu msomaji.
Tunaendelea kuufunua Uislam ambao ni dini ya kutengeneza na haikuwepo kabla ya kuzaliwa Muhammad.
Quran ambayo ilitengenezwa ili kuja kupinga Biblia ambayo ni Neno la Mungu, inadai kuwa eti, Isa bin Maryam ni Yesu. Nilipo fanya uchunguzi wa hali ya juu, nikagundua kuwa, jina la Isa halikuwepo kabla ya kuzaliwa Muhammad na kabla ya uwepo wa Allah aliyeumbwa na Muhammad.
Sasa basi, mimi nawaomba Waislam yafuatayo:
1. Mimi naomba mtuletee ushahidi unao weza kuthibitishika wa uwepo wa "Isa na jina la Isa bin Maryam" kwa kutumia vitabu vilivyo kuwepo kabla ya Quran na kabla ya kuzaliwa kwa Muhammad aliye muumba Allah.
2. Sina muda na aya za Quran. Maana Waislam mnakiri kuwa Injil iliteremshwa na Allah, hivyo basi Injil mnaweza itumia na iwe na jina la Isa.
3. Quran iliyokuja baada ya Injil siitaki. Hadith zilizo kuja baada ya Injil sizitaki. Mimi nataka mtumie vitabu vilivyo kuwepo kabla ya Quran na Muhammad kuzaliwa.
Sasa basi. Thibitisheni uwepo wa Isa kwa kutumia vitabu vilivyo kuwepo kabla ya (1) Quran (2) kabla ya Muhammad kuzaliwa (3) kabla ya Sahih Hadith za Muhammad.
Mkinipa huo uthibitisho basi leo nitasilimu na kuwa Muislam.
LAKINI NILIPO ANGALIA UWEPO WA YESU MUNGU MKUU AMBAO SIO WA KIDINI NILIPATA NAKALA NYINGI, ILA KUHUSU ISA BIN MARYAM ALIYE TUNGWA NA MUHAMMAD HAKUNA HATA NAKALA MOJA YA KIHISTORIA INAYO THIBITISHA UWEPO WAKE.
Huu ni uthibitisho wa Kihistoria wa uwepo wa Yesu Kristo ambaye ni Mungu Mkuu.
Tacitus (AD 55-120), mwana historia kutoka Roma aliandika kuhusu Yesu katika karne ya kwanza kwamba Yesu aliuwawa na Pontius Pilate. (Annals 15: 44).

Suetonius aliandika mwaka 120AD kuhusu jinsi Wayahudi walivyo mtafuta Yesu Kristo wakati wa Claudius Emeperor. Huu uthibisho upo vile vile kwenye Matendo 18: ambao ulitokea mwaka 49 AD.
Thallus, mwana Historia maarufu alindika takriban mwaka 52AD kuhusu kifo cha Yesu Kristo na ilinukuliwa na Julius Africanus katika mwanzoni wa karne ya 3.
Mara Bar-Serapion, mwandishi kutoka Siria baada ya kuharibiwa kwa Hekalu mnamo mwaka 70 AD alisema kuhusu kifo cha Yesu na alisema kuwa Yesu ni Mfalme.
Mwanahistoria wa Kiyahudi Josephus alielezea kuhusu kusulubiwa kwa Yesu chini ya Pilato katika kitabu chake cha Antiniquities kilicho andikwa takribani kati ya mwaka 93/94 AD.
Ndugu msomaji, umeona mwenye uthibitisho wa kihistoria kuhusu uwepo wa Yesu Kristo, LAKINI, baada ya kutafuta uwepo wa Isa Bin Maryam kabla ya kuzaliwa Muhammad na kabla ya Quran, historia imeshindwa kumthibitisha.
SASA BASI, KAMA KWELI UISLAM NI DINI YA MWENYEZI MUNGU, NA MWENYEZI MUNGU ANAJUA YOTE, WAISLAM TULETEENI UTHIBITSIHO WA KIHISTORIA AU WA KIIMANI KUHUSU UWEPO WA ISA BINA MARYAM KABLA YA KUZALIWA KWA MUHAMMAD AU KUANDIKWA KWA QURAN.
Narudia tena, mimi sina muda na aya za Quran zilizo kuja baadae na sina muda na hadith za Muhammad.
Uthibitisho wa Quran iliyokuja baada ya Injil siutaki. Hadith zilizo kuja baada ya Injil sizitaki. Mimi nataka mtumie vitabu vilivyo kuwepo kabla ya Quran na Muhammad kuzaliwa.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW