Saturday, August 13, 2016

MUHAMMAD ANADAI KUWA JUA LINATEMBEA NA LINASUJUDI KWA ALLAH ALIYEKAA KWENYE KITI CHA ENZI


1. Muhammad adai kuwa jua linamsujudia Allah.
2. Muhammad adai kuwa jua linatembea.
3. Muhammad adai kuwa jua linapumzika kwenye matope.
Ndugu zanguni,
Hakika hii ni dini iliyo jaa shaka na viroja. Bila ya kupoteza muda tuanze kusoma vitabu vya Wislam.
JUA LINAMSUJUDIA ALLAH:
"Abu Dhar alisimulia: Nabii aliniuliza wakati wa machweo ya jua, ‘Unafahamu mahali ambako jua linakwenda (wakati wa kuchwa)?’ Nilijibu, ‘Allah na Mtume wake wanafahamu vizuri zaidi.’ Alisema, ‘Linakwenda (yaani linasafiri) hadi linasujudu chini ya kiti cha enzi, na linapata kibali cha kusimama tena, na linaruhusiwa na kisha (muda utakuja ambapo) litakuwa linakaribia kusujudu lakini kusujudu kwake hakutakubaliwa …’" Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 54 sura ya 4 na.441 uk.283.
JUA LINATEMBEA MBINGU HADI MBINGU:
al-Tabari juzuu ya 1 uk.231 inasema, "Nilimuuliza Mjumbe wa Mungu [Muhammad] ‘[Jua] linazama wapi?’ Alinijibu: ‘Linazama mbinguni na kisha linachomoza kutoka mbingu kwenda mbingu nyingine hadi linachomoza kwenye mbingu ya juu zaidi, mbingu ya saba. Hatimaye, linapokuwa chini ya kiti cha enzi, linaanguka chini na kusujudu, na malaika wanaolisimamia wanasujudu pamoja nalo. Kisha jua linasema, Bwana wangu, ni wapi unakoniamuru nichomozee, ni upande ule nilikozamia au nilikochomozea?’
Aliendelea. Jambo hili ndilo (linalokusudiwa na) neno la Mungu: ‘Na jua: Hukimbilia mahali linapotakiwa kuwepo (usiku)’
linaposhikiliwa chini ya kiti cha enzi – ‘Jambo hilo limeamriwa na Yeye Mwenye Nguvu na Mwenye Kujua’ Bwana kwa mamlaka yake ya kifalme, Bwana ambaye ‘anavijua’ viumbe vyake. Aliendelea, Gabriel alileta kwenye jua vazi lenye kung’aa tokana na mwanga utokao kwenye kiti cha enzi, kwa kufuata vipimo vya saa na siku. Ni refu zaidi wakati wa majira ya joto na fupi zaidi wakati wa majira ya baridi, na lenye urefu wa wastani wakati wa majira ya kupukutisha majani na wakati wa majira ya kuchipua majani. [Mitindo ya majira ya kuchipua majani, kupukutisha majani na majira ya baridi!] Aliendelea. Jua huvaa vazi hio, kama mmoja wenu anavyovaa zavi lake. Kisha, huwa huru kuzunguka kwenye anga la mbinguni mpaka linapochomoza kutokea upande linaochomozea. … Njia hiyo hiyo hufuatwa na mwezi wakati wa kuchomoza kwake … Lakini Gabriel huuletea vazi kutoka kwenye mwanga wa miguunil. Hivi ndivyo neno la Mungu (linavyomaanisha) ‘Amelifanya jua kuwa angavu na mwezi kuwa mwanga.’"
HUYU MUHAMMAD wanaye dai kuwa alipasua Mwezi, anaendelea kusema uongo kuwa eti Jua linazunguka na kufika kwa Allah ili kusujudu?
MASWALI:
1. Kama Muhammad alishindwa kujua historia rahisi ya Jua?

2. Kama Muhammad anadai kuwa Jua na Mwezi vinatembea, kwanini tumwanini kuwa alitumwa na Allah?
MUHAMMAD ANAENDELEA KUSEMA UONGO NA KUZIDISHA SHAKA KWENYE QURAN
SASA MUHAMMAD ANASEMA KUWA JUA LINAZAMA KWENYE CHEMCHEM YA MATOPE
Dhu al-Qarnaiyn [Zul Qarnain] "alishuhudia kuzama kwa jua kwenye sehemu yake ya kupumzikia kwenye bwawa lenye ute mweusi na wenye harufu mbaya sana." al-Tabari juzuu ya 5 uk.173-174 (Tazama Sura 18:82-97).
al-Tabari juzuu ya 1 uk.234 pia inasema kuwa jua huzama kwenye chemchemi yenye matope. Msemo "yenye matope" ni hami’ah, unaomaanisha udongo mweusi wa mfinyanzi, lakini hamiyah ni neno lenye kufanana nalo linaloweza kumaanisha kitu cha moto. (Tazama rejeo la 442 chini ya uk.234).
Ndugu zanguni, hii dini ni Msiba ambao hauta isha mpaka kihama. Sasa Muhammad aliye dai kuwa alipasua MWEZI na kushindwa tuonyesha wapi vilipo vipande vya Mwezi alio upasua, anasema kuwa ETI Jua linazama kwenye tope. Huu kama si msiba ni nini?
Ndugu wasoamji leo nimeonelea kuwa, ni vyema tuendelee kumuumbua Allah na Muhammad maana wao wamejama shana na uongo kwenye dini yao.
Mungu awabariki sana.
Katika Huduma yake,
Max Shimba Ministries Org.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2015. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW