Saturday, September 15, 2018

UNAYAJUA MADHARA YA KUSHIKA SHERIA YA SABATO?

Image may contain: one or more people, people standing, text and outdoor



1. Kushika sabato kuna mfanya mtu asiwe mwana funzi wa Yesu, bali mwanafunzi wa Musa, kwa kuwa torati ilikuja kwa mkono wa Musa na neema na kweli vilitolewa kwa mkono wa Yesu (Yohana 1:17).

2. Kushika siku ya sabato ni mafundisho manyonge na yenye upungufu, hivyo kumfanya mtu awe mwana wa Jehanamu mara mbili (Mathayo 23:15). Kitabu cha Wagalatia 4:9-10 Biblia inasema, “Bali sasa mkiisha kumjua Mungu, au zaidi kujulikana na Mungu, kwa nini kuyarejea tena mafundisho ya kwanza yaliyo manyonge, yenye upungufu, ambayo mnataka kuyatumikia tena? MNASHIKA SIKU, na miezi, na nyakati, na miaka.”

3. Kushika sabato, kunamfanya mtu kuwa chini ya laana. Na hii ni kwa sababu sabato ni sheria iliyo katika torati; na tunaposema torati, tunamaanisha amri kumi, sheria 613 na hukumu zake. Na ilikwisha kuandikwa kuwa mtu asiyeshika torati yote ni amelaaniwa; Galatia 3:10 tunasoma, “Kwa maana wale wote walio wa matendo ya sheria, wako chini ya laana; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika YOTE yaliyoandikwa katika kitabu cha torati, ayafanye.” Kristo ndiye aliyetukomboa kutoka katika laana ya torati (Wagalatia 3:13), na ndiyo maana ukimwamini Bwana YESU, ni lazima ufuate sheria ya Kristo (Wagalatia 6:2), na siyo sheria ya Musa. Kushika sabato (pumziko) siyo sheria ya Kristo, na Bwana Yesu na Baba yake waliipinga kama tunavyoweza kusoma katika Yohana 5:16-18, “Kwa sababu hiyo Wayahudi wakamwuudhi Yesu, kwa kuwa alitenda hayo siku ya sabato. AKAWAJIBU, BABA YANGU ANATENDA KAZI HATA SASA, NAMI NINATENDA KAZI. Basi kwa sababu hiyo Wayahudi walizidi kutaka kumwua, kwa kuwa HAKUIVUNJA SABATO TU, bali pamoja na hayo, alimwita Mungu Baba yake, akijifanya sawa na Mungu.” Swali ni hili, huyu Yesu liyeshika sabato na kuwafundisha watu leo washike sabato ni Yesu yupi?

4. Kushika sabato kuna mfanya mtu awe mwilini; na mtu anayeufuata mwili ni ngumu sana kumpendeza Mungu (Warumi 8:8), kwa kuwa hatoweza kushinda dhambi. Na ndiyo maana utaona mtu anashika sabato, lakini bado haogopi kwenda kwa waganga wa kienyeji, haoni ni makosa kubishana, haoni dhambi kufanya uasherati na uzinzi. Kwake kuinadi sabato ndiyo injili, kuliko kumnadi Bwana Yesu.

5. Kushika sabato kunatengeneza ngome ya kifarisayo ndani ya mtu; na madhara ya ngome hii ni kwamba, hata kama mtu akisikia ukweli kutoka kwa Mungu mwenyewe, bado mtu huyo hawezi kuusikia wala kuufuata ukweli huo. Ufahamu wa mtu unafungwa hata nuru ya wokovu isimzukie (2 Wakorintho 4:4), hivyo moja kwa moja mtu anakuwa amekata tiketi ya kwenda Jehanam ya moto.

6. Kushika sabato kunamfanya mtu awe mnafiki. Mtu mnafiki huwa na kawaida ya kutangaza sheria na kuitilia mkazo, lakini yeye mwenyewe haitendei kazi. Luka 13:15 Biblia inasema, “Lakini Bwana akamjibu akasema, Enyi wanafiki, kila mmoja wenu, je! Hamfungui ng’ombe wake au punda wake siku ya sabato katika zizi, aende naye kumnywesha?” Na ukweli ni kwamba hakuna mnafiki atakayeurithi ufalme wa Mungu.

Sasa baada ya kusoma na kuyafahamu madhara ya kushika Sabato, je, utaendelea kushika hiyo sabato na upatwe na madhara, au utajisalimisha kwa Yesu na kuwa huru?

Shalom,

Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13
 —

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW