Tuesday, October 18, 2016

KWANINI DINI YA UISLAM INARUHUSU KUKEKETA "KUTAIRIWA" WANAWAKE?


Ndugu msomaji,
Naanza kwa swali kwa Waislam:
Wapi kwenye Taurat au Zaburi au Injili panasema kuwa Wanawake wakeketwe?
Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anasema, “Itakapogusa [kitakapokutana] kilichotahiriwa kimoja kugusa kilichotahiriwa kingine, basi yapasa kuoga.” [Al-Bukhaariy].
Na amesema tena Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), “Vitakapokutana viwili vilivyotahiriwa, basi ni wajibu kuoga.” [Ibn Maajah 611].
Na vilivyotahiriwa viwili hapo makusudio ni sehemu ya ngozi inayokatwa katika utupu wa mwanamme na ile ya utupu wa mwanamke. Na ni ushahidi kuwa wanawake walikuwa wakitahiriwa. [Rejea Swahiyh Fiqhus Sunnah mj.1, uk.99].
Pia katika kauli nyingine ya Imaam Hanbal ni 'Makrumah' kwa Hadiyth ya Mtume aliposema, “...kata kipande kidogo na wala usimalize”, na Hadiyth “Khitaan ni Sunnah kwa wanaume na Pendezo kwa wanawake.” [Hadiyth hizi tumeeleza juu hukmu zake].
Sahih hadith moja inasema kuwa: Muhammad alikutana na mwanamke aliye kuwa anamkeketa msichana ndogo, Muhammad akamwambia "AONDOE kisimi 'clitoris' (clitorectomy) chote pamoja na sehemu ya 'labia minora', ambacho kinashonwa chote na kubakiza uwazi"
Au kuondosha kisimi 'clitoris' chote, 'labia minora' na sehemu ya kati ya 'labia majora', pamoja na sehemu yote ya kiungo cha mwanamke kushonwa na kubakizwa tundu dogo tu. Na utaratibu huu unahitaji kumfunga miguu mtoto kwa kiasi cha wiki tatu.
Huu ndio UISLAM unao fanya TOHARA kwa WANAWAKE ili kumfuraisha Mwanaume tu. Hakika hii ni chukizo kwa Mwenyezi Mungu.
Wapi kwenye Taurat au Zaburi au Injili panasema kuwa Wanawake wakeketwe?
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW