Tuesday, September 6, 2016

ALLAH SIO YEHOVA "YAHUH" ( يهوه ) MWENYEZI MUNGU (SEHEMU YA NNE)

Image result for MUSLIM KILLING CHRISTIANS
ALLAH AMEJAA VISASI WAKATI YEHOVA HANA VISASI NA AMEJAA UPENDO
ALLAH SIO YEHOVA "YAHUH" ( يهوه ) MWENYEZI MUNGU
(SEHEMU YA NNE)
Waislam wanasema kuwa, eti, Allah ni Mwenyezi Mungu ambaye ni Yehova wa kwenye Biblia, lakini nilipo soma Biblia na Quran kwa makini nikaona tofauti kubwa sana kati ya Allah na Yehova.
ALLAH ANAWAAMRISHA WAISLAM WALIPIZE VISASI:
{{Enyi mlioamini! Mmepewa RUHUSA YA KULIPIZA KISASI katika waliouawa – muungwana kwa muungwana, na mtumwa kwa mtumwa, na mwanamke kwa mwanamke. Na anayesamehewa na ndugu yake (yaani yule aliyeuliwa wake) basi ashikwe kulipa kwa wema, na yeye alipe (na kulipishwa) kwa ihsani. Hiyo ni tahfifu itokayo kwa Mola wenu na ni rehema. Na atakayeruka mipaka baada ya haya, basi yeye atapata adhabu iumizayo.}} [2:178]
{{Na malipo ya ubaya ni ubaya ulio sawa na (ubaya) huo; lakini anayesamehe na kusuluhisha ugomvi; ujira wake uko kwa Allaah; bila shaka Yeye hawapendi madhalimu. Na wale wanaolipiza kisasi baada ya kudhulumiwa, hao hakuna njia ya kulaumiwa. Bali lawama iko juu ya wale wanaodhulumu watu na wakawafanyia jeuri katika ardhi pasipo haki; hao ndio watakaopata adhabu iumizayo. Na anayesubiri na kusamehe (atalipwa wema wake). Bila shaka hilo ni katika mambo makubwa ya kuazimiwa kufanywa (na kila Muislamu).}} [42:40-43]
{{Mtakuwa nao uhai (mzuri) katika kulipiza kisasi enyi wenye akili, ili msalimike.}} [2:179]
YEHOVA ANASEMA KUWA USILIPIZE KISASI:
Walawi 19:15 Msitende yasiyo haki katika hukumu, usimpendelee mtu maskini, wala kumstahi mwenye nguvu; bali utamhukumu jirani yako kwa haki.
16 Usiende huko na huko katikati ya watu wako, kama mchongezi; wala usisimame kinyume cha damu ya jirani yako; mimi ndimi BWANA.
17 Usimchukie ndugu yako moyoni mwako; ni lazima kumkemea jirani yako, wala usichukue dhambi kwa ajili yake.
18 Usifanye kisasi, wala kuwa na kinyongo juu ya wana wa watu wako; bali umpende jirani yako kama nafsi yako; Mimi ndimi Bwana.
SASA BAADA YA KUSOMA USHAIDI ULIOTHIBITISHIKA HAPO JUU, JE WEWE MSOMAJI UTAMFUATA YEHOVA AMBAYE NI MWENYEZI MUNGU NA MWENYE UPENDO
AU
ALLAH ALIYEJAA CHUKI NA VISASI VIKUBWA VIKUBWA?
Allah anasema kuwa UA kama ni kwa ajili ya KISASI, SOMA HAPA CHINI:
{{Wala msiue nafsi ambayo Allaah amekataza (kuiua) isipokuwa kwa haki (Akahuhumu hakimu kuwa mtu huyo anastahiki kuuawa na akatoa amri ya kuuawa). Na mwenye kuuawa kwa kudhulumiwa, basi Tumempa nguvu mrithi wake (juu ya muuaji huyo, akitaka ataomba kwa hakimu kuwa amuuwe kama alivyomuuwa mtu wake na akitaka atamsamehe, na akitaka atamtoza kitu). Basi (huyo mrithi asifanye fujo katika kuua kwa ajili ya huyo mtu wake aliyeuliwa). Hakika yeye atasaidiwa (na Sharia maadamu anayo haki).}} [17:33]
Je, kuua si dhambi na kunapingana na amri kuu za Mungu ya USIUWE? Mbona Allah anaruhusu kuua? Je Allah anaye ruhusu kuua na Yehova anaye sema usiuwe ni yule yule?
Uchaguzi ni wako, kumfuata Allah anaye ruhusu wewe uwe muuwaji au Mwenyezi Mungu mwenye upendo na aliye kataza kuua.
Namaliza kwa kusema:
ALLAH SIO YEHOVA "YAHUH" ( يهوه ) MWENYEZI MUNGU
Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo
Max Shimba Ministries Org.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW