Friday, September 9, 2016

KWANINI MUHAMMAD HAKUPIGWA BAKORA MIA KWA KOSA LA UZINIFU?


Katika aya hapa chini tutasoma kuwa adhabu ya mzinifu katika Uislam ni kupigwa bakora mia. Hebu soma aya kwanza:
QURAN 24:2, SURAT, AN-NOOR
Mzinifu mwanamke na mzinifu mwanaume, mtandikeni kila mmoja wao bakora mia. Wala isikushikeni huruma kwaajili yao katika huruma ya Mwenyezi Mungu. Ikiwa ninyi mnamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho. Na lishuhudie adhabu yao kundi la wauminh. ( mwisho wa kunukuu)
Sasa hebu endelea kusoma tabia ya Muhammad mtume wa allah hapa chini utagundua kuwa, kumbe Nabii wa Allah alikuwa mzinifu:
Siku moja mtume (s.a.w) Alikuwa Nyumbani kwa Mkewe Hafsa bint Umar, Hafsa akaenda kwa Baba yake kumjulia hali, Mtume (s.a.w) alimwita Mjakazi wake bibi Mariya Alqbitiyya, akawa nae Chumbani, Aliporudi Hafsa Akasema Maneno makali kwa Mtume juu ya tendo hilo (s.a.w) Mtume akasema nakuhakikishia Kuwa: Kuanzia Leo Sitamwingilia tena, mjakazi wako. (Tafsir Ibn Kathir J. 6 Uk. 367)
Muhammad mtume wa Allah kafumaniwa ugoni, lakini hatusomi kuwa alipigwa bakora mia yeye na kimada wake. Je, Muhammad yeye yupo juu ya sheria ya uzinifu?
HUDUD [1]. 604. Abu Ubayda, kutoka kwa Jaabir bin Zayd kasema, "Kupigwa mawe (kwa mwenye kuzini), na kutahariwa, na kustanji[2], na Sala ya Witri ni Sunna za lazima kutekelezwa (wajibu). Ama Sala ya witri imetokana na kauli ya Mtume (S.A.W.) alipowaambia Masahaba wake, “
Hakika wamekwisha pigwa muhuri wa Jehannam wale wote wanao zini kama Muhammad.
Kwanini Muhammad hakupigwa bakora mia kwa UZINIFU?
Kwanini Muhammad hakupigwa mawe kwa UZINIFU?
Hakika hii sio dini bali ni njia ya kwenda Jehannam.
Watakabahu
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW