Saturday, May 20, 2017

KUFUNGA MAANA YAKE NINI?

Image may contain: 1 person, food
JE, KUFUNGA NI LAZIMA KWA MKRISTO?
Neno “KUFUNGA“ linatokana na neno la Kiyunani “NESTEVO“, ambalo nalo linatokana na maneno mawili ya Kiyunani “NE“ na “ESTHIO“. Neno “NE“ maana yake “BILA“ au “HAPANA“, Kiingereza “NO“ au “WITHOUT“. Neno “ESTHIO“ maana yake “KULA CHAKULA AU KINYWAJI“, Kiingereza “TO EAT SOLID OR LIQUID FOOD“. Neno “NESTEVO” sasa linaunga maneno hayo mawili ya Kiyunani ”NE” na “ESTHIO”, na lina maana “BILA KULA CHAKULA AU KINYWAJI CHOCHOTE”. Hivyo maana ya kufunga, ni “BILA KULA CHAKULA AU KINYWAJI CHOCHOTE”.
Nyakati za Biblia, watu walifunga kwa sababu mbalimbali zilizokubaliwa na Mungu. Baadhi yao walifunga kwa sababu ya huzuni au toba (1 Samweli 7:4-6), wengine walifunga ili kuomba mwongozo wa Mungu au ili wapate kukubaliwa naye (Waamuzi 20:26-28; Luka 2:36, 37), au ili kukaza fikira walipotafakari.—Mathayo 4:1, 2.
Kufunga kunastahili kufanyika kwa moyo wa unyenyekevu na nia ya furaha. Mathayo 6:16-18 yasema, “Tena mfungapo, msiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamna; maana hujiimbua nyuso zao, ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Amin, nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe ufungapo, jipake mafuta kichwani, unawe uso; ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.
Sheria ya Musa iliwaamuru Wayahudi ‘wazitese nafsi zao,’ yaani, wafunge mara moja kwa mwaka katika Siku ya Upatanisho. (Mambo ya Walawi 16:29-31; Zaburi 35:13) Mungu hakuwaamuru watu wake wafunge katika siku yoyote nyingine ila Siku ya Upatanisho.* Kwa hiyo, Wayahudi walioshika Sheria ya Musa walipaswa kufunga katika siku hiyo. Lakini kushika Sheria ya Musa si takwa kwa Wakristo.—Waroma 10:4; Wakolosai 2:14.
Kitabu cha Matendo Ya Mitume kimerekodi kuwa Wakristo walifunga kabla ya kufanya uamuzi wa maana (Matendo Ya Mitume 13:2, 14:23). Kufunga na maombi kila mara zimeambatanishwa pamoja (Luka 2:37; 5:33). Kila mara, angazo la kufunga ni kutokuwa na chakula. Badala ya lengo kuwa, kufunga ni kuyapeleka mawazo yako nche ya vitu vya dunia na kiukamilifu kumtazamia Mungu. Kufunga ni njia mojawapo ya kudhihirishia Mungu na sisi wenyewe kwamba hatutaki mchezo katika uhusiano wetu na yeye. Kufunga kunatuzaidia kupata mtazamo na kufanya upya tegemeo letu kwa Mungu.
Ijapokuwa Yesu alifunga kupatana na takwa la Sheria, hakuwa na zoea la kufunga. Aliwaambia wanafunzi wake jinsi ya kufunga kwa njia inayofaa, lakini hakuwaamuru kamwe wafunge. (Mathayo 6:16-18; 9:14) Kwa nini, basi, Yesu alisema kwamba wanafunzi wake wangefunga baada ya kifo chake? (Mathayo 9:15) Maneno haya si amri, bali yanamaanisha kwamba Yesu alipokufa wanafunzi wake wangekuwa na huzuni nyingi sana hivi kwamba wangepoteza hamu ya chakula.
MAMBO YA KUEPUKA WAKATI WA KUFUNGA:
Jambo moja ambalo mtu anayefunga anapaswa kuepuka ni kujiona kuwa mwadilifu. Biblia inatuonya tusiwe wenye “unyenyekevu wa kujifanya.” (Wakolosai 2:20-23) Mfano wa Yesu kumhusu yule Farisayo mwenye kiburi aliyejiona kuwa bora kuliko wengine kwa sababu alifunga kwa ukawaida, unaonyesha wazi kwamba Mungu anakataa mtazamo kama huo.—Luka 18:9-14.
Pia, haifai kuwaambia wengine kwamba umefunga, au kufunga kwa sababu mtu mwingine anakuambia ufunge. Katika andiko la Mathayo 6:16-18, Yesu alieleza kwamba kufunga ni jambo la kibinafsi, kati yako na Mungu, na hupaswi kuwaambia wengine kwamba umefunga.
Ni makosa kufikiri kwamba kufunga kunaweza kulipia dhambi. Ili tendo la kufunga likubaliwe na Mungu, ni lazima yule anayefunga atii sheria zake. (Isaya 58:3-7) Msamaha haupatikani kwa kufunga bali kwa toba ya kweli kwa Yesu Kristo. (Yoeli 2:12, 13) Biblia inakazia kwamba tunapata msamaha kwa sababu Mungu alionyesha fadhili zisizostahiliwa kwa kumtoa Kristo kuwa dhabihu. Haiwezekani kustahili kupata msamaha kwa sababu ya matendo kama vile kufunga.—Waroma 3:24, 27, 28; Wagalatia 2:16; Waefeso 2:8, 9.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW