Wednesday, May 3, 2017

MUHAMMAD ALIMKUFURU ROHO MTAKATIFU NA KUTENDA DHAMBI ISIYOSEMEHEKA

Image may contain: text
Leo nitawajibu Waislam wote duniani kwa kutumia Biblia Takatifu kuwa Muhammad alimkufuru Roho Mtakatifu ambaye alihaidiwa na Yesu Kristo Bwana na Mwokozi wetu.
Bwana Yesu amesema kwamba: "...Kila dhambi na kila neno la kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho Mtakatifu hawatasamehewa." - (Mathayo 12:31)
Je! Nini maana ya KUMKUFURU Roho Mtakatifu?
Tukianza na neno KUFURU, maana yake ni: Kusema maneno yakumtukana Roho Mtakatifu ambaye ni Mungu au kufanya matendo yanayomtukana Roho Mtakatifu. Tukiendelea kusoma Mathayo 12:32 tunaona Bwana Yesu anasema kwamba:
"Naye mtu ye yote atakayenena neno juu ya Mwana wa Adamu atasamehewa, bali yeye atakayenena neno juu ya Roho Mtakatifu hatasamehewa katika ulimwengu wa sasa, wala katika ule ujao." (Mathayo 12:32)
Dhambi ya kumkana Roho Mtakatifu, ni dhambi ambayo haiwezi kusamehewa.
Kufuru dhidi ya Roho Mtakatifu haitasamehewa kwa wanadamu, Mathayo 12:31–32 (Marko. 3:29; Luka 12:10).
MUHAMMAD AMEMTUKANAJE ROHO MTAKATIFU?
"Kwa maana HAO WALIOKWISHA KUPEWA NURU, na KUKIONJA KIPAWA CHA MBINGUNI, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu, na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo, wakaanguka baada ya hayo, HAIWEZEKANI KUWAFANYA UPYA TENA HATA WAKITUBU; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na KUFEDHEHESHA kwa DHAHIRI." (Waebrania 6:4-6)
Tumeona hapo Biblia Takatifu imesema kuwa: "...wakaanguka baada ya hayo, HAIWEZEKANI KUWAFANYA UPYA TENA HATA WAKITUBU..." (Ebrania 6:6) ni kwa sababu wamefanya "...KUFEDHEHESHA kwa DHAHIRI." Wamezitukana kazi za Roho Mtakatifu ambaye ni Mungu kwa makusudi; dhambi hiyo ndiyo Yesu anasema kamwe haitasamehewa. Biblia Takatifu inazidi kusema kwamba:
"Maana, kama TUKIFANYA DHAMBI KUSUDI baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, HAITABAKI TENA DHABIHU KWA AJILI YA DHAMBI; bali kunakuitazama hukumu yenye kutisha, na ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao. Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma... Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano ALIYOTAKASWA KWAYO kuwa ni kitu ovyo, na KUMFANYIA JEHURI Roho wa neema?" (Waebrania 10:26-29)
UTHIBITISHO WA KWANZA:
Yohana 1 aya ya 32 inasema: Tena Yohana akashuhudia akisema, Nimemwona Roho akishuka kama hua kutoka mbinguni; naye akakaa juu yake "YESU".
Wote tunafahamu kuwa Muhammad hakuwa Mtakatifu na vile vile hakuwa anapaa kama ndege na alikuja miaka 600 baada ya Kristo, hivyo basi, ni dhahiri kuwa Roho Mtakatifu sio Muhammad ambaye alikuja miaka 600 baadae. Yohana hakuwai mwona Muhammad.
Waislam wanaposema kuwa Roho Mtakatifu ni Muhammad au Jibril, huko ni KUMKUFURU ROHO MTAKATIFU ambaye ni Mungu.
UTHIBITISHO WA PILI:
Yohana 1:33, [ Yohana Mbatizaji anaendelea kusema] "Wala mimi sikumjua; lakini yeye aliyenipeleka kubatiza kwa maji, huyo aliniambia, Yeye ambaye utamwona Roho akishuka na kukaa juu yake, huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu."
Yohana anaweka kiuwazi zaidi aya hiyo hapo juu kuwa Yesu ndie atakaye kuwa anabatiza kwa Roho Mtakatifu.
Kwa kifupi Yesu atamtuma ROHO ambaye ni Mwenye Nguvu ya Mungu na ni Mungu.
Je, Muhammad ni huyo Roho?
HAPANA KABISA, kwasababu Yesu aliwabatiza Wanafunzi wake na zaidi ya hapo, wafuasi wake walibatizwa kwa Roho Mtakatifu katika siku ya Pentekoste. Mda mchache baada ya Yesu kupaa kwenda kwa Baba yake Mbinguni, hivyo basi, na narudia tena, hii ilifanyika Miaka mia sita 600 kabla ya Muhammad kuzaliwa. Wanafunzi wa Yesu hawakubatizwa kwa kupitia Muhammad wala Waislam hawabatizi au batizwa.
Hivyo basi, Waislam kwa kumdhihaki Roho Mtakatifu ni KUFURU, na kumfanya Muhammad kuendelea na dhambi ya KUKUFURU ROHO MTAKATIFU.
UTHIBITISHO WA TATU:
Yohana 3 aya ya 5 inasema: Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.
Nauhakika hakuna Muislam duniani pote anayeweza kusema kuwa Muhammad anazaa, maana katika ya hapo juu Yesu anasema Mtu lazima azaliwe kwa Roho, JE, MUHAMMAD ALIZAA/ANAZAA?
Je, Waislam wanazaliwa kwa Maji na Roho? Naam teyari wamesha kufuru Roho Mtakatifu.
UTHIBITISHO WA NNE:
Yohona 3 aya ya 6 inasema: Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.
Hapa Muhammad anatupwa nje mara moja kwasababu ya haya maneno ambayo Yesu ameyasema, kwasababu
#1 Muhammad alikuwa binadamu, mbaya zaidi hivi sasa amekufa -marehemu.
#2 Kwasababu tena, Roho inazaa kwa kutumia Nguvu ya Mungu, ambaye ni Roho Mtakatifu. Huku kuzaliwa kwa Roho kulianza miaka 600 kabla ya Muhammad kuzaliwa.
UTHIBITISHO WA TANO:
Yohana 3 aya ya 8 inasema: Upepo huvuma upendako, na sauti yake waisikia, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda; kadhalika na hali yake kila mtu aliyezaliwa kwa Roho.
HAKUNA HATA MMOJA WETU ALIYE ZALIWA KUPITIA MUHAMMAD. Hivyo basi Muhammad anashindwa tena kuwa Roho ya Kweli na kuendelea kumkufuru Roho Mtakatifu.
UTHIBITISHO WA SITA:
Yohana 3 aya ya 34 inasema: Kwa kuwa yeye aliyetumwa na Mungu huyanena maneno ya Mungu; kwa sababu hamtoi Roho kwa kipimo.
Je, Muhamamd alikuwa hana kipimo?
Hapo tena Muhammad kashindwa maana alikuwa amepimiwa maneno tu na Allah wake. Muhammad alikiri kuwa yeye hajui Mungu atamfanya nini baada ya kifo, pale alipo ulizwa na watu, je, nini kitatokea baada ya kifo. Muhammad hakuwa "omniscient".
UTHIBITISHO WA SABA:
Yohana 4 aya ya 24 inasema: Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.
Mungu sio Muhammad, asante Mungu, kwa kuweka huu ukweli kuwa Roho Mtakatifu ni Mungu. Kumbe hata Jibril sio Roho Mtakatifu.
UTHIBITISHO WA NANE:
Yohana 6 aya ya 63 inasema: Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; maneno hayo niliyowaambia ni roho, tena ni uzima.
Muhammad hawezi kutoa uzima wa milele, ni kitu ambacho Mungu peke yake anaweza kukupa. Ndio maana tunajua kuwa Yesu ni Mungu, kwasababu, Yesu anatoa uzima wa Milele kwa wale wote wamwaminio.
UTHIBITISHO WA TISA:
Yohana 7 aya ya 39 inasema: Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.
Je, Muhammad atapewa kwa kila mtu ambaye anamwamini Yesu?
HAPANA KABISA, Quran inasema kuwa Ukimwanini Mwamad/
Allah basi umemwamini Allah. Hivyo Muhammad hawezi kuwa Roho ya Kweli, maana tunao Mwamini Yesu tumepewa Roho Mtakatifu na sio Muhammad ambaye amesha kufa.
UTHIBITISHO WA KUMI:
Yohana 14 aya ya 16,17, na 18 inasema: 16 Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; 17 ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu.
18 Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu.
Hizi aya zinapendwa sana na Waislam na wanapenda kuzitumia kama ushahidi wao.
Je, Muhammad aliishi na Mitume wa Yesu katika karne/Century ya kwanza?
HAPANA KABISA TENA KABISA. Muhammad hakuwepo wakati wa karne/Century ya kwanza pale Wafuasi wa Yesu walipo pewa huyo Roho Mtakatifu. Yesu alisema kwa Wanafunzi wake kuwa hata waacha YATIMA, Je, iweje Muhammad aliye kuja miaka 600 baadae awe na Wanafunzi wa Yesu katika karne/Century ya Kwanza?
UTHIBITISHO WA KUMI NA MOJA:
Yohana 14 aya ya 26. Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.
Hii aya Waislam hawaipendi kabisaa, kwasababu Yesu anasema KIUWAZI KABISA KUWA, ni nani huyu WAKILI wetu, NI WATATU KATIKA MUUNGANO MTAKATIFU. Huyu Roho Mtakatifu ana adhama zote za Baba na Mwana, HIVYO BASI, Muhammad tena ameshindwa vibaya sana hapa. Muhammad alikuwa Mtenda dhambi, huku Yesu hakuwai tenda dhambi hata moja.
UTHIBITISHO WA KUMI NA MBILI:
Yohana 15 aya ya 26 inasema: Lakini ajapo huyo Msaidizi, nitakayewapelekea kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia.
Kwa mara nyingine tena, hii ndio raha ya kufundisha katika context yake. Tumesoma katika aya hapo juu kuwa Yesu alisema nani ni Msaidizi wetu, na kwa undani zaidi, HAPA KWENYE HII AYA YA 26 Yesu anasema kuwa huyo Msaidizi ni Roho Mtakatifu.
Je, Muhammad aliishi wakati wa Mitume wa Yesu na kuwa msaidizi wao, HAPANA KABISA, inafahamika kuwa Muhammad alikuja miaka 600 baadae.
UTHIBITISHO WA KUMI NA TATU:
Yohana 16 aya ya 13 inasema: Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.
Muhammad tena ameshindwa hapa, maana hakunena na wala hakuwai sikia kutoka kwa Mungu, Yehova, bali kwa Jibril ambaye anadai kuwa alitumwa na Allah. Zaidi ya hapo, Muhammad hakutoa utabiri wa mambo yatakayo kuja. MUHAMMAD AMESHINDWA TENA KWA MARA YA KUMI NA TATU.
UTHIBITISHO WA KUMI NA NNE:
Yohana 16 aya ya 15 inasema: Na yote aliyo nayo Baba ni yangu; kwa hiyo nalisema ya kwamba atatwaa katika yaliyo yangu, na kuwapasheni habari.
Yesu anasema kuwa yote ya Baba ni yangu, je, binadamu wa kawaida anaweza kudai kuwa kila kitu cha Mungu Baba ni chake?
Hakika Yesu ni Mungu. ZAIDI YA HAPO, Yesu anasema kuwa huyo Roho Mtakatifu atatufundisha kuhusu YEYE/Yesu, wakati inafahamika kuwa Muhammad hakuwai fundisha kuhusu Yesu na wala Muhammad hakuwai sema kuwa Yesu ana Baba. Kumbe basi Roho Mtakatifu hawezi kuwa Jibril au Muislam bali ni Mungu mwenye adhama zote za Baba na Mwana.
UTHIBITISHO WA KUMI NA TANO:
YESU ANAWAPA ROHO MTAKATIFU WANAFUNZI WAKE
Yohana 20 aya ya 21 na 22 inasema: 21 Basi Yesu akawaambia tena, Amani iwe kwenu; kama Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawapeleka ninyi. 22 Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu.
AYA HAPO JUU IPO WAZI kabisa kuwa YESU ALIWAPA ROHO MTAKATIFU WANAFUNZI WAKE NA HAKUWAPA MUHAMMAD AMBAYE alikuwa bado HAJAZALIWA.
Hivyo basi, leo nimetoa USHAHIDI ZAIDI YA KUMI NA TAKO KUTOKA INJILI YOAHANA kuwa Muhammad ALIMKUFURU Roho Mtakatifu kwa kujifanye yeye ni Roho ya Kweli.
Katika huduma yake,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW