Saturday, May 13, 2017

ROHO MTAKATIFU NA KAZI ZAKE KWETU SOMO LA 5

Image may contain: one or more people, people standing, sky and text
NAWEZAJE KUJAZWA NA ROHO MTAKATIFU?
Baadhi ya wakristo hawawezi kupambanua kati ya "kujazwa na Roho Mtakatifu" na "Kuwa na Roho Mtakatifu" Ama wengine pia hufikiri" Kujazwa na Roho Mtakatifu" ni sawa na kuwa na "Karama za Roho Mtakatifu". Ni maombi yangu kwamba Mungu atatusaidia kuelewa maana halisi ya kujazwa na Roho Mtakatifu.
ROHO MTAKATIFU NI NANI?
Roho mtakatifu ni Mungu(Mungu nafsi ya tatu), Roho anapatikana kila mahali kwa wakati mmoja
( Matendo 5: 3-4) " 3 Lakini Petro akasema:“Anania, kwa nini Shetani amekupa ujasiri wa kuidanganyai roho takatifu na kujiwekea kwa siri kiasi fulani cha bei ya shamba? 4 Kabla ya kuuza je, haikuwa mali yako, na baada ya kuuza je,haikuendelea kuwa mikononi mwako? Kwa nini ukakusudia tendo kama hili katika moyo wako? Umedanganya, si wanadamu, bali Mungu."
KAZI ZA ROHO MTAKATIFU NI ZIPI?
Mwalimu, kiongozi, Fumbo ya siri za Mungu (1.Korintho 2:10)
"Kwa maana ni kwetu sisi Mungu ameyafunua kupitia roho yake, kwa maana roho huchunguza ndani ya mambo yote, hata mambo mazito ya Mungu."
Mtoa habari wa mambo yajayo, msemaji wa mambo ya Mungu, Mkumbushaji, Kutupa nguvu.
Huchunguza yote, mwombezi (Warumi 8:26)
"26 Vivyo hivyo Roho pia hujiunga kutoa msaada kwa ajili ya udhaifu wetu; kwa maana lile tatizo kuhusu tunalohitaji kusali hatujui, lakini roho yenyewe hutuombea pamoja na kuugua kusikotamkwa."
UNAWEZAJE KUJAZWA NA ROHO MTAKATIFU?
Kumtii MUNGU katika sheria zake
Moyo wote utawala wake unakuwa wa Roho mtakatifu, roho anakusaidia kuishi kwa neno
(Waefeso 5:18)
"Pia,msiwe mkilewa divai, ambayo ina upotovu ndani yake, bali endeleeni kujazwa na roho,"
Utajazwa kwa Maombi, maisha ya kulitafuta neno,maisha ya kunyenyekea, kutii.
(1 Samwel 15:21)
"Nao watu wakachukua kutoka katika nyara kondoo na ng’ombe, walio bora zaidi kati yao kama kitu kilichotengwa kwa ajili ya kuangamizwa, ili wamtolee Yehova,Mungu wako dhabihu katika Gilgali."
(Isaya 1:19)
"Ninyi mkionyesha utayari na kusikiliza,mtakula mema ya nchi."
(Yakobo 4:17)
"Kwa hiyo, ikiwa mtu anajua jinsi ya kufanya yaliyo sawa na bado hayafanyi, hiyo ni dhambi kwake."

Kinachozuia kujazwa na Roho Mtakatifu
Dhambi katika maisha ya muumini, hakuna kujazwa kama unadhambi (Waefeso 4 : 30)
"Pia, msiwe mkiihuzunisha roho takatifu ya Mungu, ambayo kupitia hiyo mmetiwa muhuri kwa ajili ya siku ya kuachiliwa huru kupitia fidia"
(1 Thesalonike 5:19)
"Msiuzime moto wa roho"
Kifungu cha maana katika kuelewa juu ya kujazwa na Roho Mtakatifu in Yohana 14:16, mahali ampapo Yesu anaahidi kukaa kwa Roho Mtakatifu kwa wakristo, na huyo atadumu si kwa muda. Ni kitu cha maana kutofautisha kati ya kukaa kwa Roho Mtakatifu na kujazwa na Roho Mtakatifu. Kudumu kwa Roho Mtakatifu aupo kwa baadhi ya wakristo, bali ni kwa Wakristo wote. Kuna sehemu nyingi katika Bibilia zinazo pongeza huu msimamo wetu.
Kwanza, Roho Mtakatifu ni zawadi iliyopewa Wakristo wote katika Kristo Yesu bila kupagua, na hakuna sheria za kutimiza ila tu ni kuwa na imani katika Kristo Yesu (Yohona 7:37-39).
Pili, Roho Mtakatifu unapokewa wakati wa kuokoka (Waefeso 1:13). Wagalatia 3:2 inasisitiza ukweli huu pia, kwa kusema kwamba kutiwa muhuri na kujazwa na Roho Mtakatifu ulitokea wakati wa kuokoka.
Tatu, Roho Mtakatifu unakaa kwa Wakristo milele. Wakristo wamepewa Roho Mtakatifu kama mtaji ama tibitisho la utukufu wao katika siku zijazo katika Kristo (2 Wakorintho 1:22; Waefeso 4:30).
Hili ni linganisho la kujazwa kwa Roho Mtakatifu ambao Waefeso 5:18 yazungumzia. Kikamilifu ni lazima tuzame katika Roho Mtakatifu ili atumiliki na katika hali hiyo atujaze. Warumi 8:9 na Waefeso 1:13-14 za sema kwamba anakaa kwa kila Mkristo, lakini anaweza kuhusunishwa (4:30), na kazi yake ndani yetu unaweza poa (1Wathesalonike 5:19). Wakati tunaruhusu haya kutokea hatuwezi kuhisi kikamilifu Roho Mtakatifu ukifanya kazi na nguvu zake ndani yetu.
Kujazwa na Roho Mtakatifu haimaanishi tendo la nche pekee; pia yamaanisha tendo la kimawazo ambalo latutia moyo kwa kila tendo tutendalo. Zaburi 19:14 yasema, “Maneno ya kinywa changu, Na mawazo ya moyo wangu, Yapate kibali mbele zako, Ee BWANA, Mwamba wangu, na mwokozi wnagu.”
Dhambi ndiyo huzuia kujazwa kwa Roho Mtakatifu, na kumtii Mungu ndio njia pekee Roho anaweza kutunzwa. Waefeso 5:18 yatwaamuru kwamba tujazwe na Roho Mtakatifu; bali si kwa kuomba ili tujazwe na Roho Mtakatifu ambayo itawezesha kukamilisha kujazwa kwa Roho. Ni utiifu wetu wa sheria za Mungu wawezesha Roho kufanya kazi kwa huru ndani yetu. Kwa sababu tumeadhirika kwa dhambi, ni vigumu kujazwa na Roho wakati wote. Wakati twatenda dhambi ni lazima tutubu papo hapo kwa Mungu na tufanye upya mkataba wa kujazwa na Roho na kuongozwa na Roho Mtakatifu.
FAIDA ZA KUJAZWA NA ROHO MTAKATIFU
Kutoufuata mwili , Hakuna kuufata mwili, kuhuishwa kwa miili yetu( Warumi 8 : 9 -10)
"Hata hivyo, ninyi hampatani na mwili, bali mnapatana na roho, ikiwa kweli roho ya Mungu inakaa ndani yenu. Lakini ikiwa mtu yeyote hana roho ya Kristo, mtu huyo si wake. 10 Lakini ikiwa Kristo yuko katika muungano pamoja na ninyi,mwili kwa kweli umekufa kwa sababu ya dhambi, bali roho ni uzima kwa sababu ya uadilifu. 11 Basi, ikiwa roho ya yule aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu inakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua KristoYesu kutoka kwawafu ataifanya pia miili yenu inayoweza kufa iwe hai kupitia roho yake inayokaa ndani yenu"
Ikiwa maisha ya dhambi yatatawala, na Roho Mtakatifu kuhuzunika na baadae kupoa. Mkristo hupoteza nguvu ya kushinda dhambi. Kwamba muumini anayeishi katika dhambi ni lazima kutubu kwa Mungu na kufanya upya mkataba ili kujazwa tena na Roho Mtalktifu.
"Kwa kuwa wote wanaongozwa na Roho wa Mungu, Hao ndio wana na Mungu" (Warumi 8:14)
Ukiwa na swali lolote au kitu kinakutatiza kuhusiana na Somo hili tafadhali andika au toa maoni yako hapa chini na wachungaji na viongozi wa dini watalijibu mara moja na haraka iwezekanavyo.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

1 comment:

Medard said...

GOD BLESS YOU MUCH FOR THE THOUGHT OF HOLY SPIRITY

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW