Wednesday, May 3, 2017

KISA CHA MAMA MSAMARIA.

Image may contain: cloud, night and text
Kulikuwa na mama mmoja msamaria, mama huyu alikuwa akiishi eneo la baridi kali..siku moja alipokuwa akiota moto ndani katika nyumba yake ya vioo ndipo akaona ndege kwa nje’,ndege huyu alikuwa katika hali ya kuelekea kufa kutokana na baridi ingawa hatimaye ndege huyo alitimiza hatua ya kwanza ya furaha ya mama huyo kwa kutua kwenye mti mkubwa ulioota nje ya dirisha dogo la nyumba yake, na ndipo mama huyu akachukua mti mwingine mrefu anaoutumia kuchochea moto ndani na kuupitisha kwenye dirisha hilo ili ukaungane na ule wa nje na kutengeneza daraja na hatimaye kumwezesha ndege huyo kupita na kuingia ndani ili kujinusuru’…lakini ndege huyo alipoona mti huo ukichomoza toka kwenye dirisha hilo alihofu kwa kufikiri kuwa huenda ni mtu anayetaka kumpiga ili hatimaye kumfanya kitoweo na kwasababu hiyo ndege huyo aliruka na kutokomea kwenye baridi zaidi na hatimaye akafa huko’
Tamko la mama msamaria, alibaki kusema:- Laiti kama ningelikuwa na uwezo wa kujimithilisha’ nikawa mfano wa yule ndege’ ningelimsogelea na kumwambia’ ndege wenzangu eeeeh twende mule ndani tujinusuru na baridi!!!!!!
Kisa hicho kinaweka mkazo na kutoa mwangaza juu umuhimu wa tendo hilo la Bwana Yesu kuvaa umbile la kibinadamu katika harakati za kumfikia na kumwokoa mwanadamu, ambapo tunaona jinsi ambavyo haikuwa rahisi kwa mama msamaria kufanikisha dhamili yake ya kumwokoa yule ndege kwa njia ya kutumia mti ambao kimsingi kwa ndege huyo ulikuwa ni kitisho.
Kumbuka kuwa endapo Bwana Yesu angelikuja katika halihalisi ya utumkufu wake wa Kimungu wanadamu wangelihofu na kuangamia kama ambavyo tunaweza kuliona hilo katika mifano kadhaa ya matukio katika Biblia, soma historia hii ya kipindi cha wana wa Israel kwa utulivu:-
Kutoka 19:11-12
wawe tayari kwa siku ya tatu; maana siku ya tatu Bwana atashuka katika mlima wa Sinai machoni pa watu hawa wote17 Musa akawatoa hao watu katika kituo, akawaleta ili waonane na Mungu; wakasimama pande za chini za kile kilima. 18 Mlima wa Sinai wote pia ukatoa moshi, kwa sababu Bwana alishuka katika moto; na ule moshi wake ukapanda juu kama moshi wa tanuu, mlima wote ukatetemeka sana.19 Na hapo sauti ya baragumu ilipozidi kulia sana, Musa akanena, naye Mungu akamwitikia kwa sauti.20 Bwana akaushukia mlima, juu ya kilele cha mlima; Bwana akamwita Musa aende hata kilele cha mlima; Musa akapanda juu. 21 Ndipo Bwana akamwambia Musa, Shuka chini, uwaonye watu wasije wakapasua njia waje kwa Bwana kutazama,kisha wengi miongoni mwao wakaangamia.
Katika andiko hilo tunaona historia hiyo ya kile kilichowapata wana wa Israel ambao kimsingi walitoa madai ya kutaka kuonana na Mungu, na katika tukio hilo la kushuka kwa Mwenyezi Mungu ili kujifunua kwao wa Israel wengi walikufa kutokana na Mungu huyo kuja katika hali ambayo hawakuweza kuikabili.
Swali! Je’ Mungu aje katika hali gani ili mwadamu aweze kuikabili?
- Aje katika hali ya ng’ombe!
- Au aje katika hali ya simba! Au hali gani?
Biblia inataja namna Mungu alivyojidhihirisha kwa Kristo katika hali ambayo mwanadamu aliweza kuikabili.
1Timotheo 3:16
Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu.
Hivyo maandiko hayo ya Biblia yantaja njia hiyo ambayo Mungu aliitumia kujidhihirisha kwa wanadamu yaani kwa kutwaa mwili wa kibinadamu ingawa haki yake ilijulikana katika ulimwengu wa roho.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW