Wednesday, July 19, 2017

JE, UNAIJUA TOFAUTI KUBWA KATI YA UKRISTO NA UISLAM?

Image may contain: 5 people, text


Kuna tofauti kubwa sana ya msingi katika ya Imani ya Ukristo na dini ya Kiislam. Kwenye hiki kijarida kifupi nitawawaekea hiyo tofauti.
Ukristo ni imani yenye msingi katika upendo, kwamaana Mungu ni upendo. Upendo ndiyo sifa kuu zaidi ya Mungu. Pia ndiyo sifa inayovutia zaidi. Tunapochunguza baadhi ya mambo yenye kupendeza ya sifa hii bora, tutaelewa kwa nini Biblia inasema kwamba “Mungu ni upendo.”—1 Yohana 4:8.
Uislam ni dini ya haki kama wanavyo kiri Waislam, huku ikifaamika kuwa haki inayo zungumzwa haijulikani na haki inaweza kupatikana hata Mahakamani kwa kuhonga. Kumbuka palipo na haki kuna haramu.
Sasa ni haki ipi ambayo ndio dini ya Uislam?
Surat An Nisaai 74. Basi nawapigane katika Njia ya Mwenyezi Mungu wale ambao wanao uza uhai wa dunia kwa Akhera. Na anaye pigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu kisha akauliwa au akashinda basi tutakuja mpa ujira mkubwa.
1. Je, Mungu gani huyu anaye tumia Mapanga kulazimisha watu kujiunga nae?
2. Je, Mungu gani huyo anaye uwa watu na kudai kuwa hiyo ndio njia ya kwenda Akhera?
HEBU TUANGALIE UKRISTO KIDOGO:
Kwa mfano, fikiria jinsi Mungu alivyoshughulika na Israeli ya kale. Hata baada ya kumiliki Nchi ya Ahadi, Waisraeli waliasi tena na tena. Mungu hakuwatupilia mbali mara moja licha ya kwamba matendo yao maovu ‘yalimhuzunisha.’ (Zaburi 78:38-41) Badala yake, kwa rehema na UPENDO aliwapa nafasi ya kubadili mwenendo wao. Aliwasihi hivi: “Sikufurahii kufa kwake mtu mwovu; bali aghairi mtu mwovu, na kuiacha njia yake mbaya, akaishi. Ghairini, ghairini, mkaache njia zenu mbaya; mbona mnataka kufa, Enyi nyumba ya Israeli?
Unaona tofauti ya Mungu wetu wa kwenye Biblia mwenye upendo na anaye kupa nafasi ya pili ya kutubu na yule Allah mwenye haki na kuuwa watu unapo vunja sheria yake?
Upendo (Mungu) hajilazimishi/haujilazimishi kwa mtu yeyote. Wale wanaokuja kwake wanafanya hivyo kwa kuitikia upendo wake. Upendo (Mungu) huonyesha upole kwa watu wote. Upendo (Yesu) alizunguka kote akifanya mazuri kwa watu wote bila upendeleo. Upendo (Yesu) hakutamani kitu cha wengine walikuwa nacho, aliishi maisha ya unyenyekevu bila kunung’unika. Upendo (Yesu) hakujivunia vile alivyo kuwa kimimwili, ingawa aliweza kumshinda nguvu kila mtu aliyekutana naye. Upendo (Mungu) haulazimishi unyenyekevu. Mungu hakulazimisha Mwnawe kunyenyekea, lakini kwa mubadala Yesu kwa pendo lake alimtii Babaye wa mbunguni. “Lakini ulimwengu ujue ya kuwa nampenda Baba; na kama vile Baba alivyoniamuru; ndivyo nifanyavyo. Ondokeni, twendeni zetu” (Yohana Mtakatifu 14:31). Upendo (Yesu) alitwaza/na huwaza yaliyo mazuri kwa matakwa ya wengine.
Waislam, tuambieni, ni haki ipi hii mnayo izungumzia kila siku?
AYA HAPA CHINI ZINATUPA PICHA KAMILI KUWA HAKI KATIKA UISLAM NI VITA NA KUMWAGA DAMU:
Surat Tawba 29. Piganeni na wasio muamini Mwenyezi Mungu wala Siku ya Mwisho, wala hawaharimishi alivyo harimisha Mwenyezi Mungu na Mtume, wala hawashiki Dini ya Haki, miongoni mwa walio pewa Kitabu, mpaka watoe kodi kwa khiari yao, hali wamet'ii
Surat Al Anfaal 38. Waambie wale walio kufuru: Wakikoma watasamehewa yaliyo kwisha pita. Na wakiyarudia basi imekwisha pita mifano ya wa zamani.
39. Na piganeni nao mpaka isiwepo fitna na mateso, na Dini yote iwe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Lakini wakiacha, basi hakika Mwenyezi Mungu anayaona wanayo yatenda.
Surat Tawba 5. Na ikisha miezi mitukufu basi wauweni washirikina popote mwakutapo, na washikeni na wazungukeni, na wavizieni katika kila njia. Lakini wakitubu, wakashika Sala, na wakatoa Zaka, basi waachilieni. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
Surat Al Baqaara 193. Na piganeni nao mpaka pasiwepo fitina, na Dini iwe ya Mwenyezi Mungu tu. Na kama wakiacha basi usiweko uadui ila kwa wenye kudhulumu
Surat Al Imran 84. Sema: Tumemuamini Mwenyezi Mungu, na tuliyo teremshiwa sisi, na aliyo teremshiwa Ibrahim, na Ismail, na Is-haak na Yaakub na wajukuu zao, na aliyo pewa Musa na Isa na Manabii wengine kutoka kwa Mola wao Mlezi. Hatubagui baina yao hata mmoja, na sisi ni wenye kusilimu kwake.
LAKINI KATIKA UKRISTO TUNASOMA:
Tibitisho kuu la upendo wa Mungu limeelezwa kwetu sisi katika Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
Upendo ni sehemu kuu ya Mungu. Upendo ni sehemu kuu ya tabia ya Mungu, na utu wake.
Mungu ni mfano mtakatifu wa upendo wa kweli. Cha kushangaza, Mungu amewapa uwezo wa kupenda vile anavyo penda, kupitia nguvu za Roho Mtakatifu wale wote watakaomkubali Mwanawe kama mwokozi wa maisha yao. (Yohana 1:12; 1Yohana 3:1, 23-24).
NAAM, MUNGU NI UPENDO NA ANATUPENDA NA HIYO NDIO TOFAUTI YA UKRISTO WENYE UPENDO NA UISLAM WENYE HAKI.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW