Sunday, September 10, 2017

JE, KUJICHUA SEHEMU ZAKO ZA SIRI (PUNYETO) NI DHAMBI? (SEHEMU YA NNE)

Image may contain: food
Mpendwa:
Mungu alimuumba mwanamume na mwanamke wakiwa na uvutano wenye nguvu kati yao, na hakuna ubaya wa kutosheleza tamaa za ngono katika mpango wa ndoa. Kabla ya kufunga ndoa, huenda ukawa na tamaa kali za ngono. Hilo likitokea, usidhani kwamba wewe ni mtu mwovu au kwamba huwezi kuishi maisha safi. Unaweza kudumisha usafi wa kiadili ukiamua kufanya hivyo! Lakini ili ufanikiwe, utahitaji kudhibiti mawazo yako kuhusu watu wa jinsi tofauti. Unaweza kufanya hivyo jinsi gani?
Epuka kujifurahisha kwa mambo machafu. Bila shaka, haimaanishi kwamba sinema zote, au miziki yote ni mibaya. Hata hivyo, katika ulimwengu wa leo burudani nyingi zimekusudiwa kuamsha tamaa zisizofaa za ngono. Biblia inatoa shauri gani? “Acheni tujisafishe wenyewe kila unajisi wa mwili na roho, tukiukamilisha utakatifu katika kumwogopa Mungu.” (2 Wakorintho 7:1) Epuka kabisa burudani zote zinazoweza kuchochea tamaa zisizofaa za ngono.
UPO KUNDI GANI?
Uko wapi rafiki yangu? Nazungumza na wewe ambaye unafanya mchezo huo, bado unataka kuendelea nao au unatamani kuacha? Shika maneno yangu, kwamba ni HATARI kujichua, halafu weka nia ya kutaka kuacha huu utumwa, kisha vuta subira hadi wiki ijayo katika sehemu ya mwisho ambayo haitaacha kitu.
MFADHAIKO:
Mtu ambaye anaendekeza kazi hii, hupata mfadhaiko. Anayepata mfadhaiko, huwa mwepesi sana wa kuwa na matamanio kwa jinsia ya upande wa pili.
KUSHINDWA TENDO LA KAWAIDA
Mwenye mchezo huo, pamoja na uhodari wake wa kujifurahisha akiwa peke yake, anapokutana na mwenzi wake faragha, kazi inakuwa si ya kiwango cha kuridhisha. Kuna athari nyingi ambazo hujitokeza.
Kwanza, anakosa ujasiri, hayupo tayari kuandaliwa, kumuandaa mwenzake. Kishazoea kufanya kila kitu haraka haraka, tena kwa kutumia hisia zaidi kuliko uhalisia wa tukio lenyewe.
Anakuwa goigoi, anachelewa kuwa tayari, hata akiwa tayari anafika safarini mapema zaidi. Mbaya zaidi, akifika hawezi kuanza safari nyingine. Hata kama akianza, kuna uwezekano mkubwa wa kuishia njiani.
Baadhi yao, hubaki wakiwa baada ya wahusika wao kuwagomea katikati ya safari. Zipo athari nyingi zaidi ya hizo,
kutegemea na namna tatizo lilivyokomaa na aina ya jinsia.
Baadhi ya madhara ya Waathirika wa Upigaji Punyeto na Kujichuwa.
• Kupiga Punyeto Kunapelekea kufika mshindo kabla na bila kujijua na husababu matatizo ya Nguvu za Kiume.
• Kutokwa na manii usingizini bila kujijuwa.
• Maumivu ya mgongo.
• Punyeto usababisha udhaifu wa mwili.
• Kuwa na sura ya ujuvi.
• Udhaifu wa Macho, kutoona vizuri.
• Nywele Kutokuwa na Afya.
• Kupungua uzito chini ya kiwango.
• Uchovu na udhaifu wa mwili, wa mara kwa mara
• Kupata maumivi kwenye kinena.
• Maumivu kwenye mapumbu.
• Mbegu za uzazi kuwa dhaifu.
• Kutosikia raha ya mapenzi/jimai.
• Kupungua kwa hamu ya kula.
• Matatizo ya kusimamisha.
• Kupotea/kutosikia njege.
• Kufikia mshindo mapema, dakika moja hoi.
TUMEFIKIA TAMATI YA MADA YETU KUHUSU KUJICHUA SEHEMU YA SIRI.
JE, UPO TAYARI KUACHA MCHEZO HUU BAADA YA KUSOMA HII MADA?
INAWEZEKANA NA NJIA RAHISI NI KUOMBA KWA MUNGU AKUSAMEHE DHAMBI HII NA KUTOA HILI PEPO LA KUJICHUA.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

1 comment:

Unknown said...

Je kuna dawa yoyote kwa mpiga punyeto

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW