Sunday, September 10, 2017

JE UNAIJUA HOJA KUBWA NA PEKEE YA WASABATO "SDA" KUHUSU KUSHIKA SABATO? SEHEMU YA TATU

Image may contain: 1 person, standing and outdoor
3. MUNGU SI MTU HATA ASEME UONGO 
Wakinukuu andiko la Hesabu 23:19 kwa hiyo wanasema eti kwa kuwa Mungu alisema mtaishika Sabato (Kutoka31:16) basi ni lazima kuishika tu na kamwe Mungu hawezi kusema uongo akiagiza kuishika ni lazima iwe kushika, jibu la hoja hiyo ni hili. Ni kweli Mungu si mtu hata aseme uongo lakini ni lazima tuelewe Mungu ni mwamuzi wa yote,yeye ndiye mfanya sheria na pia ndiye muondoa sharia (Isaya 33:22) Mungu akiweka sheria halafu akaiondoa na kuiweka nyingine haimfanyi Mungu kuonekana muongo au haimaanishi kuwa Mungu kasema uongo.
Mungu aliye iweka sheria ya Sabato ya mwilini na ndiye mwamuzi wa kuiondoa na hakuna wa kumuuliza, vyote ni vyake yeye Mungu baada ya kuweka sheria ya Sabato ya mwilini au ya kupumzika Jumamosi akaahidi kuikomesha au kuisitisha au kuivunja (Hosea 2:11) na anatimiza kwa kuivunja (Yohana 5:2-9) kubeba mzigo siku ya sabato ilikuwa ni kuivunja Sabato (Yeremia 17:21) na huyu Yesu aliyevunja sabato ndiye aliye tuamuru watu wote duniani kumuiga Yesu katika yote ikiwemo na la kuvunja Sabato (Mathayo 11:29).
USIKOSE SEHEMU YA NNE
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW