Sunday, September 10, 2017

JE, KUJICHUA SEHEMU ZAKO ZA SIRI (PUNYETO) NI DHAMBI? (SEHEMU YA KWANZA)

Image may contain: one or more people and text
Hili ni somo linalo tatanisha na kuwewesesha watu wengi, na labda naweza hata kuhukumiwa kuwa natumia lugha chafu, la hasha. Nilazima tujifunze kila kitu, maana msema kweli ni mpenzi wa Mungu.
KUJICHUA NI NINI HASA?
Kwa Kiingereza tendo hili linaitwa ‘masturbation’ likiwa na maana ya kupiga punyeto. Hapa nimetumia kwa ulaini kabisa; kujichua. Lugha nyepesi na rahisi kufikika kwa wengi ni kujiridhisha! Ni kitendo cha mtu kujichezea kimahaba huku akivuta hisia za mapenzi kwa mtu ambaye yupo mbali naye hadi anapomaliza haja zake.
Namna ya ufanywaji inategemea zaidi na jinsi ya mazoea. Wapo wanaotumia vifaa bandia (artificial) na wengine vifaa halisi kama aina mbalimbali za matunda ambazo zinafanana na sehemu pacha!
Wengine wanatumia njia wanazojua wenyewe, lakini wanaume wengi wanatumia sabuni lengo hapa ni moja tu, unatakiwa kufahamu kwamba namaanisha kujiridhisha
Unapoanza kubalehe, tamaa za ngono zinaweza kuwa zenye nguvu sana. Kwa sababu hiyo, huenda ukaangukia mazoea ya kupiga punyeto. Wengi husema kwamba si neno kufanya hivyo. “Hakuna mtu anayeumia,” wanasema. Hata hivyo, kuna sababu nzuri ya kuepuka mazoea hayo. Mtume Paulo aliandika: “Kwa hiyo, viueni viungo vya mwili wenu . . . kwa habari ya . . . hamu ya ngono.” (Wakolosai 3:5-Toleo la Ulimwengu Mpya) Kupiga punyeto hakuui hamu ya ngono bali kunaichochea. Isitoshe, fikiria yafuatayo:
Kupiga punyeto humfanya mtu kuwa mwenye ubinafsi. Kwa mfano, mtu anapopiga punyeto, anakazia fikira hisia zake mwenyewe za kimwili.
Kupiga punyeto humfanya mtu kuwaona watu wa jinsia tofauti kuwa vitu au vifaa vya kujitosheleza tu.
Badala ya kuamua kupiga punyeto ili kuzima tamaa za ngono, jitahidi kukuza sifa ya kujizuia. (1 Wathesalonike 4:4, 5) Ili ufaulu, kwanza kabisa Biblia inapendekeza ujiepushe na hali zinazoweza kuamsha tamaa ya ngono. (Methali 5:8, 9) Namna gani ikiwa umekuwa mtumwa wa zoea la kupiga punyeto?
Labda umejaribu kuacha lakini hujafanikiwa. Ni rahisi kukata kauli kwamba huwezi kubadilika, na kwamba huwezi kuishi kulingana na viwango vya Mungu. Hivyo ndivyo mvulana anayeitwa Pedro alivyojiona. “Niliporudia zoea hilo, nilihisi vibaya sana,” anasema. “Nilifikiri kwamba siwezi kamwe kusamehewa. Nilishindwa kusali.”
Ikiwa hivyo ndivyo unavyohisi, jipe moyo. Kuna tumaini. Vijana wengi, na watu wazima pia, wamefaulu kushinda mazoea hayo ya kupiga punyeto. Wewe pia unaweza kufaulu!
INAWEZEKANAJE KUJIRIDHISHA?
Ni rahisi sana kumaliza tendo la huba kwa kujifanyisha mwenyewe. Silaha kubwa inayotumiwa na waathirika ni
kuwavutia hisia watu wa jinsi pacha wakati tendo husika likiendelea kufanyika. Habari mbaya kwa watu wenye mchezo huu ni kwamba, kwanza wakishaanza, inakuwa vigumu sana kuacha.
Inashindikana kwa sababu ni jambo la aibu. Si rahisi kupata ushauri kutoka kwa watu maana ni aibu pia kumweleza rafiki yako juu ya mchezo huo. Kutokana na hilo sasa, kinachotokea ni kwamba ‘waumini’ wa mchezo huu wanaendelea kuwa watumwa kwa maisha yao yote. Hapa chini tutaona kwa undani jinsi tatizo hili linavyoumiza vichwa vya wengi.
Ni kweli hutaki kuwa mtumwa wa mchezo huu hatari? Zipo athari nyingi sana rafiki yangu ambazo nitazieleza
USIKOSE SEHEMU YA PILI
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW