Sunday, September 10, 2017

JE, KUJICHUA SEHEMU ZAKO ZA SIRI (PUNYETO) NI DHAMBI? (SEHEMU YA PILI)

Image may contain: 1 person, text


CHANZO NI NINI HASA?
Wenye umri mkubwa au wa kati, huanza tabia hii mbaya hasa baada ya kuanza mchezo wa kuangalia video za kikubwa wakiwa peke yao. Kwa sababu wanachotazama kinahusisha msisimko wa mapenzi, basi bila kutarajia hujikuta ayari!
Hii inafanana pia na kwa watoto wa kike, vyanzo nilivyoeleza hapo juu pia husababisha kwa karibu sana.
Jambo la kushangaza ni kwamba, hakuna mdau wa mchezo huo ambaye amefundishwa jinsi unavyofanywa. Wengi wameanza wenyewe, tena wengine bila kujua nini kitakachotokea, lakini baada ya matokeo kuonekana, ndiyo
mwanzo wa kutopea huko.
Kwa vijana wa kiume, wengi huanza tabia hii wakiwa kwenye umri wa kubalehe. Mara nyingi hutokea asubuhi wakati wa kuamka, usiku wakati wa kulala au bafuni wakati wa kuoga.
Kwa kawaida, mtu anapokuwa katika sehemu ya utulivu kwa maana ya kupumzika, wakati mwingine mkono unaweza kutembea huku na huko kwenye mwili na mwisho wake bila kutegemea mhusika anajikuta ameshaingia kwenye mchezo huo.
Kama ilivyotajwa mapema, wale walio na mazoea ya kupiga punyeto mara nyingi hujiona kuwa wenye hatia. Bila shaka, ‘kuhuzunishwa kwa njia ya kimungu’ kunaweza kukuchochea ushinde mazoea hayo. (2 Wakorintho 7:11) Lakini kujiona kuwa mwenye hatia kupita kiasi kunaweza kuwa na matokeo mabaya. Kunaweza kukuvunja moyo sana mpaka utake kukata tamaa.—Methali 24:10.
Kwa hiyo, jaribu kuwa na usawaziko. Kupiga punyeto ni uchafu. Mazoea hayo yanaweza kukufanya uwe ‘mtumwa wa tamaa na raha za namna mbalimbali’ na kukufanya uwe na maoni yasiyofaa. (Tito 3:3) Hata hivyo, kupiga punyeto si upotovu wa kingono, kama vile uasherati. (Yuda 7) Ikiwa una tatizo la kupiga punyeto, usikate kauli kwamba umefanya dhambi isiyoweza kusamehewa. Siri ni kupinga tamaa ya kufanya hivyo na kutokubali kamwe kushindwa!
Ni rahisi kuvunjika moyo baada ya kurudia zoea hilo. Ukirudia, kumbuka maneno ya Methali 24:16: “Huenda mwadilifu akaanguka hata mara saba, naye hakika atasimama; lakini waovu watakwazwa na msiba.” Kujikwaa hakumaanishi kwamba wewe ni mwovu. Kwa hiyo, usikate tamaa. Badala yake, chunguza jambo lililofanya urudie zoea hilo, kisha ujaribu kuliepuka.
Tafakari kuhusu upendo na rehema za Mungu. Mtunga-zaburi Daudi, ambaye pia nyakati fulani alifanya dhambi kwa sababu ya udhaifu wake, alisema: “Kama vile baba anavyowaonyesha wanawe rehema, ndivyo ambavyo Mungu amewaonyesha rehema wale wanaomwogopa. Kwa maana yeye mwenyewe analijua vema umbo letu, akikumbuka kwamba sisi ni mavumbi.” (Zaburi 103:13, 14) Ndiyo, Mungu hukumbuka hali yetu ya kutokamilika na ‘yuko tayari kusamehe.’ (Zaburi 86:5) Kwa upande mwingine, anataka tujitahidi na kufanya marekebisho. Hivyo basi, unaweza kuchukua hatua gani ili kushinda zoea hilo?
USIKOSE SEHEMU YA TATU
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW