Sunday, September 10, 2017

JE UNAIJUA HOJA KUBWA NA PEKEE YA WASABATO "SDA" KUHUSU KUSHIKA SABATO? SEHEMU YA NNE

Image may contain: sky, cloud, text, nature and outdoor
4. WANASEMA MUNGU ALISEMA HAWEZI KULIVUNJA AGANO LAKE NA HAWEZI KUBADILI NENO LILILOTOKA KINYWANI MWAKE
Kwahiyo wanasema Mungu aliweka agano na mwanadamu na agano hilo ni agano la Sabato na kwa kuwa Mungu alisema watu waishike Sabato basi hawezi kamwe kulibadili neno lake.
Wakinukuu maandiko yafuatayo Zaburi 89:34 na Kutoka 20:8-11. Majibu ni haya, ni muhimu kujua andiko hili la Zaburi 89:34 linazungumzia agano gani, kwa kuwa katika Biblia kuna maagano mengi ambayo Mungu alifanya na wanadamu kwa mfano;
Mungu alifanya agano na Nuhu na kizazi chake (Mwanzo 6:18, 9:9,11-12) Mungu alifanya maagano kadhaa na Ibrahim (kama mawili) na maagano hayo alifanya na Ibrahim na vizazi vyake yaani Isaka, Yakobo na watakaofuata. Agano la kwanza ni la kupewa Nchi ya Kanaani ambayo ndiyo Israeli (Mwanzo 15:18, Kutoka 2:24, Zaburi 105:8-11)
Agano la pili ni la kutahiriwa (Mwanzo 17:9-14). Sasa, Mungu aliposema “sitalihalifu agano langu” na "sitalibadili neno lililotoka kinywani mwangu" alikuwa anazungumzia nini?
Hapa alikuwa anazungumzia agano la Daudi, sio agano la Sabato angalia Zaburi 89:3-4,9-34-35) katika agano hilo na Daudi, Mungu hatalihalifu, na hatalibadili neno lililotoka mdomoni mwake alilosema kuwa amefanya agano na mteule wake Daudi, amemwambia Daudi, kuwa wazao wake atawafanya imara milele, na maneno yote yanayosemwa katika Zaburi 89:3-4,19-35 yanazungumzia agano la Daudi sio agano la Sabato.
USIKOSE SEHEMU YA TANO.
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW