Friday, July 14, 2017

JINSI YA KUOMBA KWA IMANI, SEHEMU YA PILI

Image may contain: one or more people and text


Yesu alituambia tuwe na “imani kwa Mungu.” Hi inahusu mpango na kusudi la Mungu kwa maisha yako.
Yeye ni Mungu Mkuu, mwenye enzi. Imani yote ulimwenguni haiwezi kubadilisha makusudi yake yenye enzi. Watu walio na saratani wameamini kwamba Mungu angeponya magonjwa yao, ijapokuwa walikufa.
Waraka wa Kwanza wa Yohana 5:14 inafaa sana inapoeleza kwamba, “tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia.” Kifungu cha 15 kinatuhakikishia kwamba tukiomba (kwa imani) sawasawa na mapenzi yake, “tunazo zile haja tulizomwomba.”
Tunapofahamu mapenzi ya Mungu alivyotufunulia katika maandiko, basi tunaweza kudai hayo kama ahadi zake. Mungu tayari hutimiza mahitaji yetu kabla kutuahidi. Tunaweza kuishi au kufa kwa ahadi za Mungu.
Maombi ni kubadilisha ahadi za Mungu kuwa riziki kila siku.
Siguswi Mimi!
Wakati moja nilikaa Romania kwa majuma mawili. Nilifwatwa na maaskari makachero kila nilipoenda.
Wachungaji niliokuwa nikifanya kazi nao waliishi kwa kuhofia usalama wao. Nilimuuliza mmoja wa hao wachungaji wajasiri jinsi walivyoweza kulala usiku. Je, alihofia maisha yake? Akiwa na tabasamu kama ya malaika, alinijibu, “Mimi siwezi kuguswa. Ikiwa Mungu angali amenipa kazi ya kufanya, askari hawana
uwezo wa kunidhuru.” Nililengwalengwa na machozi. Nilihisi kuwa na aibu na kiburi. Nikakumbuka maneno ya Daudi, “BWANA ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? BWANA ni ngome ya uzima wangu, nimhofu nani?” (Zaburi 27:1).
Huyu mtu wa Mungu mpendwa alikuwa kama Danieli katika tundu la simba, lakini moyo wake haukuwa na hofu kwa sababu Mungu aliahidi kufunga midoma ya simba. Hebu tukumbuke hayo tunapoomba.
Tunahitaji kudai yote ambayo Mungu ameahidi katika neno lake kama riziki. Imani ni kumwamini Mungu kwa neno lake, na kumtarajia kutimiza yale amesema atatimiza.
Imani Ni Kutafuta
Je, kuna mambo unayoyatumainia, au kutamani, au kuota? Je, utafanyaje ili ndoto yako ikamilike?
Kwanza, ondoa yale ambayo si mapenzi ya Mungu, bali ni tamaa yako tu. Pili, amini ahadi rahisi kama vile Wafilipi 4:19; “Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachohitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.” Mungu hakuahidi kunipa mahitaji yangu yote; Ameahidi kunijazia kila
ninachohitaji. Waebrania inasema kwamba imani ni “bayana ya mambo yasiyoonekana.” Ikiwa unahitaji lililo la haki, utawezaje “kuona” bayana ya hitaji hilo unalolikusudia kutimizwa?
Riziki ya Mungu, Kimiujiza:
Nilikuwa ningali mgeni katika chuo kimoja, ambapo nilianza kuona Mungu akinipa riziki kwa njia ya miujiza. Nilihitajika kulipa kodi katika chumba nilichokuwa nikikaa pamoja na rafiki yangu mmoja.
Tulikosa hela ya kulipa kodi kwa muda wa mwezi moja. Je, kodi hii ingetoka wapi? Tuliacha kuangaikia jinsi ya kupata fedha hizo. Tukaanza kuomba, kama jaribio la mwisho. Nilikuwa kijana wa miaka 19 ambaye alikuwa na matarajio ya kuwa mhubiri. Nikaomba Baba yangu aliye mbinguni anipe kodi!
Wiki hiyo nilipata barua kutoka kwa Huduma Ya Misitu Ya Amerika. Barua hiyo ilikuwa na hundi ya kulipa kodi! Kwa kweli, hundi hiyo haikuwa ya kodi, bali ilikuwa yangu! Mwaka iliyopita, wakati wa kiangazi, niliitwa kuzima moto kule Oregon.
Tuling’ang’ana kuzima moto usiku na mchana. Sikufahamu
kuwa serikali hulipa watu kwa kuzima moto! Kwa hivyo, miezi mingi baadaye nikapata hundi kupitia posta. Ni juma hilo tu ambalo nilimwomba Mungu anitimizie hitaji ambalo lilikuwa ngumu!
Imani ni kuona mahitaji yako yakitimizwa. Tunapomwamini na kumwomba Mungu, atajiheshimu kwa kutimiza neno lake. Rafiki yangu Mkristo, hatupati kwa sababu hatuombi. Amini na kumwomba Mungu ili akutimizie. Tunaweza kupata yote tunayohitaji ikiwa tutaamini kwamba Mungu ameshatutimizia.
Shalom
USIKOSE SEHEMU YA TATU ====> Kuna vikundi viwili vya watu ambao wana imani aina mbili tofauti. Kikundi cha kwanza ni cha “kuona ni kuamini.”
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW