Wednesday, November 16, 2016

SHETANI LA ULAFI KATIKA UISLAMU


Ndugu msomaji,
Leo ningependa tujifunze kidogo kuhusu roho ya ulafi ambayo inawasumbuwa ndugu ztu katika Adam. Hebu tusome Biblia kama ushahidi.
Wafilipi 3: 19 mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao u katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani.
Walafi wao wamesha amua kuabudu chakula na mungu wao ni matumbo yao. Mtu mlafi akiona chakula, basi yeye hula kwa haraka haraka na kujaza tumbo lake mpaka anavimbiwa. Ulafi ni dhambi kama ilivyo sema kwevye Wafilipi hapo juu. Ulafi ni kuabudu tumbo.
Mithali 23: 20 Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo; Miongoni mwao walao nyama kwa pupa. 21 Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini, Na utepetevu humvika mtu nguo mbovu.
Watu wanao kula nyama kwa Pupa mpaka wanavimbiwa na kushindwa kutembea, hao wana roho chafu ya ulafi, na ni dhambi kuabudu chakula au kuwa mtumwa wa chakula au mtumwa wa tumbo lako.
Kuna dini fulani wao wanapo dai kuwa wanafunga siku thelasini, huwa wanabadilisha masaa ya kula na kula usiku kucha mpaka wanavimbiwa matumbo yao. Hiyo dini ni dini ya walafi na wanatenda dhambi, huku wao wakifikiria kuwa wanafunga kwa Allah wao.
Wagalatia 5: 16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.
18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.
19 Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
24 Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.
25 Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.
26 Tusijisifu bure, tukichokozana na kuhusudiana.

Kama Neno la Mungu linavyo sema kuwa, tusiwe na tamaa za mwili, maana mwili wetu ni hekalu la Mungu. Ikimaanisha kuwa Roho Mtakatifu anaishi ndani ya mwili wetu, na hivyo, ni vyema tuutunze. Ulafu ni roho kutoka kwa Shetani na kula mpaka kuvimbiwa ni dhambi na ni kuabudu chakula na matumbo yetu.
1 Wakorintho 6: 19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;
20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.
Basi mpendwa, usiongozwe na tamaa za mwili bali ongozwa na Roho aliye ndani yako.
Leo tumejikumbusha kuwa, Ulafi ni roho kutoka kwa Shetani na ni dhambi.
1. Kwanini Waislam wanakula usku kucha wakati wa mfungo wa Ramadhani?
2. Kwanini Allah amewaruhusu kula usiku kucha na kuwakalisha na njaa mchana kucha, je huko si kubadilisha masaa ya kula?
3. Mbona Yesu wa Biblia alipo funga, yeye hakula Daku?
Hakika kubadilisha masaa ya kula na kula usiku kucha ni ulafi, na ni dhambi mbele ya Mwenyezi Mungu.
Max Shimba Ministries

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW