Friday, July 14, 2017

AYA ZA SHETANI NDANI YA QURAN, SEHEMU YA PILI

Image may contain: text


Bukhari alikufa karibu na mwaka 870 BK (hata miaka mitatu baada ya vyanzo vitatu kati ya vinne vilivyoorodheshwa.) Wakati Muhammad alipoisema Sura ya Nyota, wapagani na Waislam walisujudu. (Bukhari juzuu ya 3 kitabu cha 19 na.173, uk.100 juzuu ya 3 kitabu cha 19, na.176, uk.101; juzuu ya 6 kitabu cha 60 na.385-386 uk.364-365; Abu Dawud juzuu ya 1 kitabu cha 2 sura ya 481 na.1401, uk.369). Wapagani hawasemekani kusujudu kwa ajili ya Muhammad kusema maneno mengine yoyote, ni kwa nini wakubaliane kiasi hiki na sura hii, hasa kwa vile Bukhari na Abu Dawud hawasemi kuwa hao wapagani waliwahi kuwa Waislam, na hii ilikuwa kabla ya vita na hawa wapagani wa Maka!
Pia, Sura 22:52 inasema, "Hatukuwahi kumtuma mtume au nabii Kabla yako, lakini, alipoumba nia, Shetani alimtupia (ubatili) kiasi kwenye nia yake: lakini Mungu atafuta kitu chochote (batili) ambacho Shetani anatupia ndani, na Mungu atafanya dhahiri (na kuthibitisha) Ishara Zake…"
Sura 17:73-75 inasema, "Na lengo lao lilikuwa kukujaribu na kukupeleka mbali na jambo tulilolifunua kwako, kuweka badala yake kitu tofauti kabisa kwa kutumia jina letu: (Kwa ajili hiyo), tazama! Watakuwa wamekufanya kuwa rafiki (yao)! Na je hatujakupa wewe, ungeweza kuelekea upande wao kiasi. Katika hali hiyo tulipaswa kukufanya uonje mara mbili (ya adhabu) kwenye maisha haya, na kiasi kama hichohicho mautini: na zaidi ya hapo usingepata mtu wa kukusaidia dhidi yetu!"
Kumbuka kwamba ingawa baadhi ya watu wanadai kuwa Sura 17:73-75 ilifunuliwa wakati wa "Kupaa kwa Nabii", Tabari na Ibn Sa’d waliandika kuwa Sura 17:73-75 ilifunuliwa karibu na wakati wa aya za Shetani. Waislam hata wana neno maalum la kunong’oneza kwa Shetani, ambalo matamshi yake yanafanana na "wiswas".
Mapingamizi Tisa ya Kiislam na Maitikio Yake
Pingamizi la 1 la Waislam: Watu wengine mbali ya hawa kumi na moja hawajaziongelea aya za Shetani. Baadhi ya wanazuoni wa Kiislam ambao hawakundika kuhusu aya za Shetani walkuwa Imam Muslim aliyeandika Sahih Muslim, Abu Dawud, Nas’ai, Ahmad bin Hanbal, and ibn Hisham.
Itikio: Kuna vitu vingi kwenye makusaniko ya Hadithi ambavyo havimo kwenye mikusanyiko mingine. Kwa mfano, Hadithi ndefu za Bukhari hazina mafundisho kuhuu sababu za kutoa zaka, adhabu ya kujilimbikizia vitu, na malaika wawili wanaomtembelea Muislam kila asubuhi kama yanavyopatikana kwenye Sahih Muslim juzuu ya 2 sura ya 371 na.2205, uk.484. Kama mfano wa pili, tunajua kuwa Ibn Hisham aliitumia Bukhari, lakini aliiacha sehemu inayohusu aya za Shetani. Kwenye nakala ya Ibn Hisham ya Ibn Ishaq, alisema aliondoa vitu alivyoona kuwa vibaya. Kama alijisikia aibu sana hata hakuweza kuziweka, huo sio uthibitisho kuwa hazikutokea.
Pingamizi la 2 la Waislam: Aya zinazodaiwa kuwa za Shetani haziendani sawa na sehemu nyingine ya Sura 53.
Itikio: Kumbuka kuwa sehemu ya sasa haikufuatia aya za Shetani, bali ilichukua nafasi zao. Pia nyakati zingine sehemu tofauti za Sura moja zilitolewa nyakati tofauti. Upande mmmoja, al-Wahidi alisema Muhammad alisema hadi maneno ya mwisho. Kwa upande mwingine, hatujui kuwa Sura yote ya Nyota (53) baada ya aya ya 22 iliandikwa wakati mmoja. Aya za 51-53 zinaonekana kuwa hazipo mahali ake kwani zinamongelea Muhammad mwenyewe.
Pingamizi la 3 la Waislam: Sura 53:19-21 inaweza kuwa ilikuwa mapema zaidi kuliko Sura zinazoongelea kunong’ona kwa Shetani.
Itikio: Tabari na ibn Sa’ad wanasema zilifunuliwa wakati mmoja na Sura 17:73-75. Hakuna mtu leo hii anayejua kwa uhakika wakati ambapo aya nyingi za Kurani ziliandikwa. Kwa upande mwingine, hata kama iliandikwa mapema haitaweza kukanusha maneno iliyoyasema. Kama Waislam wasahilina wanaiamini kabisa Kurani, ikiwa ni pamoja na Sura 17:73-75 na 22:52, watatakiwa kuamini kwamba Shetani anaongeza vitu kwenye Kurani. John Gilchrist, kwenye Muhammed and the Religion of Islam uk.120 anasema, "Hoja nyingine ni dhaifu kwa sababu hakuna ushahidi thabiti kuwa sehemu ya kwanza ya Surah 53 inaongelea miraj [kupaa kwa Muhammad] kulikotokea baada ya kuhamia Abyssinia. Kama ilivyokwishaonyeshwa, kuna uhakika wa kiasi kikubwa sana kuwa inaongelea moja ya ziara za mwanzo za Muhammad, ambazo Kurani yenyewe inaonyesha kuwa hazizidi mbili ambazo alizifanya wakati huduma yake ilipoanza. Kwa bahati mbaya inaonekana kuwa hoja zote za Waislam za uhalisi wa vipingamizi vya habari hii ni dhaifu."
Pingamizi la 4 la Waislam: Aya za Shetani zinapingana na mafundisho ya msingi kuwa kuna Mungu mmoja ambayo Muhammad alishikilia kufundisha.
Itikio: Muhammad hajawahi kuthibitishwa kushikilia kitu chochote kile. Kumbuka, Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 54 sura ya 10 na.490, uk.317; juzuu ya 4 kitabu cha 53 sura ya 38 kabla ya na.400, uk.266; juzuu ya 8 kitabu cha 53 sura ya 38 na.400, uk.267 inarekodi kuwa Muhammad alikuwa amerogwa na mwovu kwa kipindi fulani. Isitoshe waandishi wa maisha yake na watu wengine waliorekodi jambo hili walikuwa bado Waislam, kwa hiyo wana historia hawa wanathibitisha kuwa kulikuwa na watu kadhaa ambao walikuwa tayari kumfuata Muhammad hata kama alisema uongo.
Pingamizi la 5 la Waislam: Vifungu vingi kwenye Kurani vinasema Muhammad hakuweza kusema maneno yoyote yasiyokuwa kweli, na kwa ajili hiyo jambo hili haliendani na tafsiri kuwa Shetani anaingilia mambo. Kwa mfano,
Sura 10:15b: "Sema; Si kwa ajili yangu, kwa hiari yangu, kubadilisha hili: Sifuati kitu chochote isipokuwa kile kilichofunuliwa kwangu…"
Sura 41:42: "Hakuna uongo unaoweza kulikaribia kutokea mbele au nyuma yake: Limetumwa na Yeye Aliyejaa Hekima na Mwenye Kustahili Sifa zote."
Sura 15:9: "Tumeutuma, bila shaka, Ujumbe; na tutaulinda kwa hakika (dhidi ya uharibifu)."
Sura 60:44-46: "Kama (Mjumbe) angetunga neno lolote kwa jina letu, Tungemkamata kwa mkono wa kulia na kisha tungeikata ateri ya moyo wake"
Itikio: Kwa upande mmoja, inadaiwa kuwa Shetani, siyo Muhammad, alitunga aya za Shetani, na kulindwa kwa Kurani haukanushi kuingia kwa mafundhisho ya uongo na Mungu kuyarekebisha. Kwa upande mwingine, kama Muislam anatafsiri aya hizi kuwa zinafundisha kwamba hakuna kitu cha uongo kitakachoweza kuingia ujumbe wa nabii, hata kama aya za Shetani hazitahusishwa, jambo hili litakuwa kinyume na kunong’oneza kwa Shetani ambako kumeelezwa kwenye Kurani.
Pia, hii si mara pekee aya ya Kurani "inapotea kabisa" kwa sababu ilibatilishwa. Sahih Muslim juzuu ya 1 sura ya 244 na.1433, uk.329-330 ni Hadithi muhimu kwa sababu inaonyesha kuwa aya ilibatilishwa, bali baada ya kubatilishwa ilipotea kabisa. Hivyo ama:
a) Kurani kwenye mbao zenye maandishi [mbinguni] ilikuwa na toleo la awali, na toleo lililofuata lilitofautiana na mbao hizo. Kurani ya leo inatofautiana na mbao zenye maandishi za mbinguni.
b) Kurani kwenye mbao zenye maandishi za mbinguni zina toleo la baadaye, na toleo la awali linatofautiana nalo. Kwa hiyo maneno ya kwanza yalitolewa kama kiwakilishi cha mbao zenye maandishi za mbinguni wakati ukweli ni kwamba ilikuwa ni uongo.
Kipi ni kipi? Mbao za maandishi [mbinguni] kwenye Sura 85:20-22 hazidhaniwi kutengenezwa kwa puti ya kipumbavu.
Pingamizi la 6 la Waislam: Tabari anawezakuwa hakukusanya habari kiuhakiki.
Itikio: Ingawa hatuna ushahidi wa mada haya, waandishi wengine watatu wa maisha [ya Muhammad] pia waliandika jambo hili. Wawili kati yao waliandika kabla ya Tabari, kwa hiyo hata kama Tabari alionekana kutokuwa mhakiki, jambo hilo haliwezi kuathiri kitu chochote kwa kiasi kukubwa kwani bado tuna watu wengine watatu. Muislam anaweza kupenda kuona kuwa waandishi wote wa maisha ya Muhammad wanaonekana kuwa na dosari sana, lakini vyanzo mbalimbali vinaonyesha usahihi wao.
Pamoja na hayo, Tabari hakupokea vitu vyote bila kuvihakiki. Kwa mfano, kwenye juzuu ya 1, uk.532 anasimulia tamaduni nyingi za kiislam za Adam na Hawa alizojifunza kutoka kwa watu wenye Torati. Anazinukuu nyingi zake lakini anasema kuwa ana mashaka na uhakika wa hizi Hadithi. (Kutoka kwenye kitabu cha Barbara Freye Stowasser kiitwacho Woman in the Qur’an, Tradition, and Their Interpretation uk.28).
Pingamizi la 7 la Waislam wa Madhehebu ya Suni: Hadithi zenye uhakika hazilisemi jambo hili moja kwa moja.
Itikio: Bukhari juzuu ya 3 kitabu cha 19 sura ya 42 na.173, uk.100; juzuu ya 3 kitabu cha 19 sura ya 43 na.176, uk.101; juzuu ya 6 kitabu cha 60 sura ya 286-287 na.385-386, uk.364-365; Abu Dawud juzuu ya 1 kitabu cha 2 sura ya 481 na.1401, uk.369 zinaeleza hali waliokuwa nayo watu wa Maka walipokuwa wanasujudu waliposikia Sura 53. Ni vigumu kueleza tofauti kitu kilichokuwepo kuhusiana na sura hii kilichowafanya wapagani wasujudu kwa ajili ya sura hii, ikiwa hawakusujudu kwa ajili ya kitu kingine. Kurani yenyewe pia inasema kuhusu "kunong’oneza" kwa Shetani.
USIKOSE SEHEMU YA TATU

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW