Friday, July 14, 2017

KUOMBA NI KUZUNGUMZA NA MUNGU

Image may contain: one or more people and text


Kuomba ni kuzungumza na Mungu. Ni sehemu katika maisha yetu inayohusiana na mazungumzo baina yetu na Baba yetu wa Mbinguni. Ukristo, kwanza kabisa, ni uhusiano wa kibinafsi kati ya mwenye dhambi wa kawaida na Mungu wa ajabu. Uhusiano wowote kati ya mtu na mtu lazima uwe na mazungumzo!
Lazima kuwe na mawasiliano katika uhusiano ili kuufanya kuwa hai na yenye afya. Mungu ni Baba yetu, nasi ni wanawe. Jamii yetu ina shida ikiwa hatuwezi kuwasiliana kwa mazungumzao!
Kwa nini tunapaswa kuomba?
1. Kuomba huonyesha uhusiano wenye afya kati yetu na Mungu. Kila mwamini anapaswa kuwa na hamu ya kweli moyoni ya kutamani kuzungumza na Mungu. Mtu anapoomba mara kwa mara, atathibiti maisha yake ya maombi na hamu ya Mungu zaidi. Ikiwa uhusiano wako na Mungu ni nzuri, basi hamu ya kuongea naye itakuwepo. Baadaye tutazungumzia jnsi dhambi na uasi huharibu maisha yetu ya maombi.
2. Yesu alituamuru tuombe. “Akawambia mfano, ya kwamba inawapasa kumwomba Mungu siku zote, wala wasikate tamaa” (Luka 18:1). Tutakata tamaa ikiwa hatuombi “nyakati zote.” kuomba ni tendo la tamaa na utiifu. Tunapaswa kuomba hata kama hatuna hamu ya kuomba.
3. Kuomba ni tabia ya ufahamu wa Mkristo mwenye afya. Yesu daima alidumu ndani ya Baba yake katika maombi. Tunapaswa kukaa ndani yake na ndani ya neno lake ili maombi yetu yaweze kujibiwa (Yohana 15:7). Mungu anataka maombi yetu, kwa sababu ulimwengu unahitaji majibu yanayotolewa na Mungu.
4. Maombi hufungua milango ya nguvu zisizo za kawaida katika maisha yetu. Maombi yetu yanaweza kumshughulisha Bwana Yesu kutenda kazi katika ulimwengu wetu. Kuomba kwa uwezo kutamruhusu Mungu kutenda kazi ambayo kwa kawaida hawezi kutenda. Baadaye katika kitabu hiki utajifunza kuhusu nguvu za maombi na jinsi ya kufanya nguvu hizo kutumika!
Hebu tuvumbue “mambo ya kina” zaidi katika Neno la Mungu. Tunaweza kugawanyisha kweli hizi katika makundi ya maombi, vita vya kiroho, na maombezi. Hebu ingia na Yesu patakatifu zaidi kwa maombi na maombezi!
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW