Friday, April 14, 2017

NIFANYE NINI ILI NIWEZE KUSHINDA TAMAA NA FIKRA ZA NGONO KILA SAA?

Image may contain: one or more people and text
Je, Unatatizo la kupiga Punyeto?
Nifanye nini ili niweze kudhibiti fikira chafu za ngono?
Mpendwa:
Mungu alimuumba mwanamume na mwanamke wakiwa na uvutano wenye nguvu kati yao, na hakuna ubaya wa kutosheleza tamaa za ngono katika mpango wa ndoa. Kabla ya kufunga ndoa, huenda ukawa na tamaa kali za ngono. Hilo likitokea, usidhani kwamba wewe ni mtu mwovu au kwamba huwezi kuishi maisha safi. Unaweza kudumisha usafi wa kiadili ukiamua kufanya hivyo! Lakini ili ufanikiwe, utahitaji kudhibiti mawazo yako kuhusu watu wa jinsi tofauti. Unaweza kufanya hivyo jinsi gani?
Epuka kujifurahisha kwa mambo machafu. Bila shaka, haimaanishi kwamba sinema zote, au miziki yote ni mibaya. Hata hivyo, katika ulimwengu wa leo burudani nyingi zimekusudiwa kuamsha tamaa zisizofaa za ngono. Biblia inatoa shauri gani? “Acheni tujisafishe wenyewe kila unajisi wa mwili na roho, tukiukamilisha utakatifu katika kumwogopa Mungu.” (2 Wakorintho 7:1) Epuka kabisa burudani zote zinazoweza kuchochea tamaa zisizofaa za ngono.
Je, unatatizo la kupiga Punyeto?
Vijana fulani hujaribu kupunguza tamaa ya ngono kwa kupiga punyeto. Lakini kufanya hivyo kunaweza kutokeza matatizo makubwa. Biblia inawahimiza Wakristo hivi: “Viueni viungo vya mwili wenu vilivyo duniani kwa habari ya uasherati, uchafu, hamu ya ngono, tamaa yenye madhara, na kutamani.” (Wakolosai 3:5) Kupiga punyeto ni kinyume kabisa cha ‘kuua hamu ya ngono.’ Kwa kweli, kupiga punyeto huchochea na kukuza hamu hiyo!
Kupiga punyeto kwaweza kukufanya kuwa mtumwa wa tamaa zako. (Tito 3:3) Hatua moja unayoweza kuchukua ili kushinda zoea hilo ni kuzungumza na mtu unayemtumaini. Mkristo aliyekuwa na tatizo la kupiga punyeto kwa miaka mingi anasema hivi: “Laiti ningeweza kupata ujasiri wa kuzungumza na mtu fulani kuhusu tatizo hilo nilipokuwa kijana! Kwa miaka mingi nilisumbuliwa na hisia za hatia, nazo ziliathiri sana uhusiano wangu na wengine, na zaidi ya yote, uhusiano wangu na Yehova.”
Ni nani unayeweza kuongea naye? Mara nyingi ingefaa kuzungumza na mzazi. Au huenda Mkristo mkomavu kutanikoni anaweza kukusaidia. Unaweza kuanza kwa kusema, “Ningependa kuzungumza nawe kuhusu tatizo linalonisumbua sana.”
Nifanye nini ili niweke kudhibiti fikira chafu za ngono?
Mtume Paulo alisema: “Naupigapiga mwili wangu na kuuongoza kama mtumwa.” (1 Wakorintho 9:27) Vivyo hivyo, huenda wewe pia ukahitaji kujitia nidhamu wakati mawazo yasiyofaa kuhusu watu wa jinsia tofauti yanapoingia katika akili yako. Mawazo hayo yakiendelea, jaribu kufanya mazoezi ya kimwili. Biblia inasema: “Mazoezi ya kimwili ni yenye faida kidogo.” (1 Timotheo 4:8) Kutembea kasi kwa muda au kufanya mazoezi ya kimwili kwa dakika chache kwaweza kukusaidia kuondolea mbali mawazo hayo yasiyofaa.
Zaidi ya yote, usipuuze msaada kutoka kwa Baba yako wa mbinguni. Mkristo mmoja anasema hivi: “Tamaa za ngono zinapoanza kuamka najilazimisha kusali.” Si kwamba Mungu atakufanya uache kupendezwa na watu wa jinsia tofauti. Lakini anaweza kukusaidia kuona kwamba kuna mambo mengine mengi unayoweza kukazia fikira zako.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW