Sunday, April 30, 2017

WALEENI WATOTO KATIKA NJIA YA KRISTO

Image may contain: 4 people, people smiling, text
Mithali 22:6 inasema; “mlee mtoto katika njia impasayo, naye
hataiacha, hata atakapokuwa mzee”.
Hivyo ni malezi ndiyo yafanyayo watoto kuwa wema au wabaya au watukutu, kumbuka huwezi kuwatenga watoto na jamii, nchi au dunia hii iliyojaa yote mema na mabaya Isipokuwa kwa kuwajaza nguvu ya kushinda majaribu ya dunia ambayo imo katika Neno la Mungu.
Torati 6:6-7. "Na maneno haya ninayokuamuru leo yata kuwa katika moyo wako nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii nakuyanena uketipo katika nyumba yako na utembeapo njiani na ulalapo na uondokapo."
Nidhamu ni namna yakuonyesha upendo kwa mtoto. Imeandikwa katika Mithali 13:24 "Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; bali ampendaye humrudi mapema."
Nidhamu njema humfunza mtoto Imeandikwa Mithali 29:15 "Fimbo na maonyo hutia hekima bali mwana aliyeachiliwa humuaibisha mamaye."
Sababu ya kumwathibu mtoto nikumfanya akuwe vema. Imeandikwa Waefeso 6:4 "Nanyi akina baba msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana."
Watoto hutoa matunda ya wazazi wao. Imeandikwa katika Kutoka 34:7 "Mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; Wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba zao, na wana wa wana wao pia hata kizazi cha tatu na cha nne."
Mungu ana tarajia matokeo gani kwa watoto? Imeandikwa katika Waefeso 6:1 "Enyi watoto watiini wazazi wenu katika Bwana maana hii ndiyo haki."
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW