Friday, April 14, 2017

PASAKA YA KALE ILIKUWA KUVULI CHA YESU

Image result for pasaka
Sehemu ya 3 na ya Mwisho:

PASAKA YA KALE ILIKUWA KUVULI CHA YESU

Mungu Mwenyezi alileta mapigo kumi juu ya Wamisri ili awaokoe Waisraeli kutoka utumwani. Pigo la mwisho lilikuwa mauti ya - ya wazaliwa wa kwanza wa Wamisri lilo wapa ushidi waisraeli kutoka nchini Misri (Kutoka 12:29-36); Wakristo nasi tunapata ushindi kwa kufufuka kwa Yesu na kuishinda mauti (Wakolosai 2:11-13)

Kusudi Waisraeli nao wasiuawe, Mungu aliwaamru wamchinje mwanakondoo na kutia damu yake penye miimo na miisho ya milango yao.(Kutoka 12:13); vivi hivyo Wakristo pia tunapo shiriki kula mkate na kukinywea kikombe cha mzao wa mzabibu kwa ukumbusho wa Yesu, tunakuwa na uzima ndani yetu. (Yohana 6:51-53)

• Baada ya kuwaokoa Waisraeli, Mungu aliwapa siku kuu ya kukumbuka walivyookolewa. Siku hii iliitwa "Pasaka" kwa sababu neno "pasaka" maana yake ni "kupita juu" (Kutoka 12:1-28, 43-48); Vivyo hivyo baada ya Yesu kutuokoa alitupa agizo la kumega mkate na kukinywea kikombe. (Mathayo 26:26-28; 1 Wakorintho 11:23-16; Matendo 20:7)

• Waisraeli walitumia mwana-kondoo kwa pasaka (Kutoka12:3-5); Bali Wakristo mwana-kondoo wetu ni Yesu (Yohana 1:29, 36), Yeye ndiye "Pasaka" wetu (1 Wakorintho 5:7).

• Waisreli waliamriwa kutwaa mwana-kondoo asiye na hila (Kutoka 12:5); kwetu sisi Wakristo Yesu ni mwana-kondoo asiye na hila (1 Petro 1:19)

• Waisraeli waliamriwa kutokuvunja mfupa wa Mwanakondoo wa Pasaka waliposhiriki kumla (Kutoka 12:46; Hesabu 9:12); Vivyo hivyo Yesu naye aliye Pasaka wetu hakuvunjwa mfupa.(Yohana 19:33, 36)
• Wayahudi walishiriki Pasaka pamoja na mikate isiyotiwa chachu wakikumbuka walivyokula jangwani (Kutoka 12:8, 15; Kumbukumbu 16:3); Wakristo pia tunashiri mikate isiyotiwa chachu tukikumbukwa mwili wa Kristo uliyoteswa kwa ajili yetu (Mathayo 26:26; 1 Wakorintho 11:23-24)

• Wayahudi waliokolewa kwa damu ya mnyama waliyoipaka milangoni, (Kutoka 12:7); Lakini Wakristo tunaokolewa na damu ya Yesu iliyomwagika kwa ajili yetu (Mathayo 26:28)

• Wayahudi walishiriki pasaka kila mwaka mara moja (Kutoka 12:2, 14); Bali Wakristo tunashiriki pasaka kila mara. (Matendo 20:7).

MUDA WA KUFA KWA MWANAKOONDOO WA PASAKA.

Katika Agano la Kale Mwanakondoo alitakiwa kuchinjwa jioni
Kut 12:6 “Tunzeni wanyama hao mpaka siku ya kumi na nne ya mwezi, ambapo lazima watu wa jumuiya yote ya Israeli wachinje wanyama hao wakati wa jioni..”

Katika Agano Jipya mwanakondoo aliuwawa jioni ili kutimiza taratibu za Pasaka
Mat 27: 45-50. 45 “Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa, nchi nzima ilikuwa giza. 46Mnamo saa tisa Yesu akalia kwa sauti kuu, ``Eli, Eli lama sabakthani?'' Yaani, ``Mungu wangu, Mungu wangu, mbona ume niacha?'' 47Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama hapo waliposikia haya walisema, ``Anamwita Eliya!'' 48Mmoja wao akaenda mbio akaleta sponji akaichovya kwenye siki akaiinua kwa mwanzi akamwekea mdo moni. 49Lakini wengine wakasema, ``Hebu tuone kama Eliya ata kuja kumwokoa.'' [Na mwingine akachukua mkuki akamchoma ubavuni, pakatoka maji na damu]. 50Yesu akalia tena kwa sauti kuu, kisha akakata roho.”

Marko 15:33-37 33 “Ilipofika saa sita, giza lilikumba nchi nzima kwa muda wa saa tatu. 34Ilipofika saa tisa, Yesu akalia kwa sauti kuu ``Eloi, Eloi lama Sabaktani?'' Yaani, ``Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?'' 35Baadhi ya watu waliokuwa wanasimama karibu waliposikia maneno hayo, walisema, ``Mnamsikia? Anamwita 

36Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sponji kwenye divai na siki, akaiweka kwenye ufito akamwinulia Yesu ili anywe huku akisema, ``Hebu tuone kama Eliya atakuja kumshusha kutoka msala bani!'' 

37Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho. 38Pazia la hekalu likapasuka vipande viwili kuanzia juu hadi chini.”

Luk 23:44-47. 44 “Ilikuwa kama saa sita mchana. Kukawa na giza nchi nzima mpaka saa tisa, 45kwa maana jua liliacha kutoa nuru. Pazia la Hekalu likapasuka katikati kukawa na vipande viwili. 46Yesu akapaza sauti akasema, ``Baba, mikononi mwako ninaikabidhi roho yangu.'' Baada ya kusema haya, akakata roho. 

47Mkuu wa maaskari alipoona yaliyotokea, akamsifu Mungu akasema, ``Hakika, mtu huyu alikuwa mwenye haki.'' 

Mat 1:21 Naye atamzaa mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yesu; kwa maana yeye ndiye atakayewaokoa watu wake kutoka katika dhambi zao.''

Ebr 9:11-14 “11Kristo alipokuja kama kuhani mkuu wa mambo mema ambayo tayari yamekwisha wasili, alipitia kwenye hema ya kuabudia ambayo ni kuu zaidi na bora zaidi na ambayo haikujengwa na binadamu, yaani ambayo si sehemu ya ulimwengu huu ulioumbwa. 12Yeye aliingia patakatifu pa patakatifu mara moja tu kwa wakati wote, akichukua, si damu ya mbuzi na ndama, bali damu yake mwenyewe, na hivyo kutupatia ukombozi wa milele. 13Kwa maana ikiwa damu ya mbuzi na mafahali na majivu ya ndama hunyunyizwa juu ya watu wachafu kidini ikawatakasa kwa kuwaondolea uchafu wao wa nje, 14 damu ya Kristo ambaye kwa njia ya Roho wa milele alijitoa mwenyewe kwa Mungu kama sadaka isiyokuwa na doa, itazisafisha dhamiri zetu zaidi sana kutokana na matendo yaletayo kifo, na kutuwezesha kumtumikia Mungu aliye hai.”

Ebr 9:24-26 24 “Kwa maana Kristo hakuingia kwenye hema ya kuabudia iliyotengenezwa na bina damu kama mfano wa hema halisi. Yeye aliingia mbinguni penyewe, ambapo sasa anatuwakilisha mbele za Mungu. 25Wala hakuingia mbinguni kujitoa mwenyewe mara kwa mara, kama kuhani mkuu ain giavyo Patakatifu pa Patakatifu kila mwaka na damu ambayo si yake. 26Ingekuwa hivyo, ingalimpasa Kristo kuteswa mara nyingi tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Lakini ilivyo ni kwamba ametokea mara moja tu kwa wakati wote, katika siku hizi za mwisho, ili atokomeze dhambi kwa kujitoa mwenyewe kuwa dhabihu.

Ebr 10:8-10 8Kwanza alisema, ``Dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa wala sadaka zitolewazo kwa ajili ya dhambi hukutaka, wala huku pendezwa nazo,'' ingawa hizi zilitolewa kwa mujibu wa sheria. 9Kisha akasema, ``Niko hapa, nimekuja kutimiza mapenzi yako.'' Anaweka kando ule utaratibu wa kwanza na kuanzisha utaratibu wa pili. 10Na kwa mapenzi hayo, sisi tumetakaswa kwa njia ya sadaka ya mwili wa Yesu Kristo alioutoa mara moja tu, kwa wakati wote”

Basi kama tulivyoona yakuwa Pasaka ya kale iliondolewa pamoja na taratibu zake na sasa Pasaka wa Wakristo ni Yesu .

Pasaka katika Agano Jipya, Yesu ndiye Mwanakondoo mwenyewe wa Pasaka asiye na ila wala waa.
Bwana wa Mbinguni akubariki. Nimatuimaini yangu kuwa utafikisha ujumbe huu kwa watu wa mataifa ili wamwamini Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo,ili waokolewe. Bwana akubariki sana.

Mwalimu Chaka wa Musa 

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW