Friday, April 14, 2017

AHADI ZAKE NI KWELI NA AMINA

Image may contain: sky and text
POKEA BARAKA TELE KUTOKA KWA YESU KRISTO MUNGU WETU MKUU.
Ngoja nikupe siri hii nzuri, zipo baraka nyingi sana za kiulinzi kutoka kwa Bwana zinazoambatana na wewe kumtumikia Mungu kwa njia ya kuwaambia wengine habari za huyu Yesu.
Mungu hutimiza ahadi zake. Imeandikwa katika 2Wakorintho 1:19-20 "Maana Mwana wa Mungu, Kristo Yesu aliyehubiriwa katikati yenu na sisi yaani mimi na Silwano na Timotheo hakuwa Ndiyo na siyo; bali katika yeye ni Ndiyo. Maana ahadi zote za Mungu zilizopo katika yeye ni Ndiyo; tena katika yeye ni Amin, Mungu apate kutukuzwa kwa sisi."
Kuwa na imani kwamba Mungu atatenda yale aliyoahidi katika neno lake (Waefeso 6:16)
Waefeso 6:16 inasema ‘zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu’.
Waebrania 11: 1 inatueleza kwamba ‘Imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo ni bayana ya mambo yasiyoonekana’.
Ndani ya Biblia zipo ahadi nyingi za Mungu kwako ambazo zinagusa kila eneo la maisha yako kiulinzi, baraka, uponyaji, afya njema, uzima, uzao, mafanikio nk. Ni jukumu lako kuzisoma na kuifunga imani yako hapo. Maana mara nyingi Shetani huwawekea watu mashaka juu ya Mungu wao na ahadi zake kwamba hatazitimiza. Kwa hiyo kama huzijui hizo ahadi ni rahisi sana kutekwa na fikra za Shetani. Hivyo ni jukumu lako kuhakikisha unaweka imani thabiti kwenye ahadi za Mungu katika maisha yako.
Shalom
Max Shimba Mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW